Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Zahanati nyingi za Vijiji vya Mkoa wa Kigoma katika wilaya zote zina upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya na baadhi ya zahanati hazina Waganga hivyo huduma zinatolewa na Manesi Wasaidizi tu:- Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa afya wa kutosha katika maeneo hayo ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu kuna upungufu mkubwa wa Madaktari na Wauguzi, Muuguzi mmoja anahudumia wodi moja akiwa peke yake hali inayosababisha azidiwe na shughuli. Wagonjwa wanawalalamikia Wauguzi kwamba hawawahudumii lakini ni kutokana na kuzidiwa na kazi nyingi. Je, ni lini Serikali itapeleka Waganga na Wauguzi ili kumaliza tatizo liliko katika Wilaya ya Kasulu? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, katika Mkoa wa Kigoma kuna kambi tatu za wakimbizi. Wilaya ya Kasulu kuna Kambi ya Nyarugusu, Wilaya ya Kakonko kuna Kambi ya Mtendeli na Wilaya ya Kibondo kuna Kambi ya Nduta. Wagonjwa wanapozidiwa katika kambi mbili ya Mtendeli na Nduta katika Wilaya ya Kibondo na Kakonko, wale wa Nduta hupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kibondo na wale wa Mtendeli hupelekwa katika Kituo cha Afya cha Kakonko. Je, ni lini Serikali, kwanza, itapeleka pesa za kumalizia Hospitali ya Wilaya katika Wilaya ya Kakonko na kupeleka Wauguzi na Madaktari? Pili, katika Wilaya ya Kakonko ni lini nao watapelekewa Waganga na Wauguzi wa kutosha ili kumaliza matatizo yaliyopo katika hospitali hiyo? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) :
Mheshimiwa Spika, katika jibu langu la msingi nimekiri upungufu wa waganga pamoja na watumishi wa afya kwa ujumla wake. Pia nimeeleza jinsi ambavyo katika bajeti ya 2018/2019 walivyoomba kupatiwa Waganga 1,667.
Mheshimiwa Spika, lakini ni nia njema ya Serikali ya kuhakikisha kwamba huduma ya afya inatolewa. Nimepata nafasi ya kwenda Kasulu na tatizo ambalo nimekutana nalo pale Kasulu ni pamoja na kutokuwepo vituo vya afya vya jirani ili hospitali ya wilaya iwe na sehemu ya kupumulia. Katika utaratibu mzima wa Serikali wa kuhakikisha kwamba huduma ya afya inapatikana ya kutosha. Miongoni mwa wilaya 67 ambazo zinaenda kupata hospitali za wilaya, Wilaya za Kigoma zitakuwepo ikiwa ni pamoja Uvinza, Buhigwe pamoja na Kasulu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama hiyo haitoshi, Kakonko kuna Kituo cha Afya kinaitwa Gwamanumbu na Lusesa nao wanaenda kupata kituo cha afya ambacho kina hadhi ya kuweza kufanya operesheni. Hii yote kwa ujumla wake unaona jinsi ambavyo Serikali ina nia njema ya kuhakikisha kwamba afya kama jambo la msingi linaenda kupatiwa ufumbuzi.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Waziri wa Utumishi na Utawala bajeti yake imesomwa jana na sisi TAMISEMI pamoja na uhitaji wetu kibali cha ajira tunapata kutoka kwao. Naamini katika maombi haya ya wahudumu pamoja na Waganga 1,667 tutapata wa kutosha na tutaenda kupunguza huo uhaba wa watumishi.
Mheshimiwa Spika, yeye mwenyewe ni shuhuda kwamba kuna mashirika ambayo yamekuwa yakishirikiana na Serikali kwa sababu suala la wakimbizi huwezi uka-predict kwamba watakuja wangapi. Naamini kwa ushirikiano ambao umekuwa ukioneshwa hakika huduma ya afya itaenda kuboreshwa na tatizo hili litapungua.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Zahanati nyingi za Vijiji vya Mkoa wa Kigoma katika wilaya zote zina upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya na baadhi ya zahanati hazina Waganga hivyo huduma zinatolewa na Manesi Wasaidizi tu:- Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa afya wa kutosha katika maeneo hayo ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A.J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Katika Kamati yetu ya huduma za jamii ni wazi kwamba tuna upungufu wa watumishi wa afya takribani 48%. Katika zoezi hili la uhakiki vituo vingi vya afya vimefungwa, hali inayosababisha akinamama wengi wajawazito kuendelea kufariki na hata takwimu zinaonesha kwamba wanaokufa ilikuwa 400 na zaidi kati ya vizazi 100,000 leo tunaongelea zaidi ya wanawake 500 na zaidi katika vizazi 100,000.
Mheshimiwa Spika, ni kwa nini sasa Serikali haiajiri wakati Madaktari wako kibao na watumishi hao wako nje ya ajira? Ni kwa nini Serikali haiajiri wakati watu wetu wanaendelea kufariki? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) :
Mheshimiwa Spika, tumekiri juu ya upungufu wa wataalam wa afya lakini pia ni ukweli usiopingika kwamba unapoajiri implication yake ni suala la bajeti. Naamini kabisa kwa upungufu huu tulionao na idadi ya watumishi katika kibali ambacho kimetoka wanaoenda kuajiriwa ni pamoja na Madaktari. Naomba tuvute subira tupitishe bajeti hii wengi wa wale wanaoenda kuajiriwa itakuwa ni Madaktari ili kupunguza tatizo hili kubwa tulilonalo.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Zahanati nyingi za Vijiji vya Mkoa wa Kigoma katika wilaya zote zina upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya na baadhi ya zahanati hazina Waganga hivyo huduma zinatolewa na Manesi Wasaidizi tu:- Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa afya wa kutosha katika maeneo hayo ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, naomba nimuulize swali dogo tu la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, matatizo yaliyopo huko Mkoani Kigoma yapo pia katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, kuna uhaba mkubwa wa watumishi, vituo vya afya na zahanati wakati mwingine vina mtumishi mmoja. Je, Serikali iko tayari sasa baada ya kuajiri kuleta watumishi katika Halmashauri ya Itigi? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, katika wale watumishi watakaokwenda kuajiriwa hakika tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba sehemu ambayo kuna upungufu mkubwa ikiwa ni pamoja na jimbo lake tunawapeleka.
Mheshimiwa Spika, wakati Mheshimiwa Susan anaongea, aliongelea kuhusiana na baadhi ya vituo kufungwa na sisi Wabunge ni mashuhuda Mheshimiwa Waziri wa Utawala Bora alitoa tamko tukiwa humu ndani ya Bunge kwamba kama kuna eneo lolote Mbunge anajua kwamba kituo kimefungwa kwa sababu ya kukosekana watu wa kutoa huduma pale apeleke maombi ili isitokee hata sehemu moja eti tumefunga kituo kwa sababu hakuna mtu wa kutoa huduma ya afya kwa eneo husika.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niendelee kuwasihi Waheshimiwa Wabunge kama kuna maeneo ambayo tumejenga na Mheshimiwa Bobali alisema jana, ni fursa hii tuhakikishe kwamba hakuna kituo cha afya hata kimoja au zahanati yetu hata moja ambayo inajengwa ikakamilika ikaacha kutumika eti kwa sababu hakuna watu wa kutoa huduma.

Name

Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Zahanati nyingi za Vijiji vya Mkoa wa Kigoma katika wilaya zote zina upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya na baadhi ya zahanati hazina Waganga hivyo huduma zinatolewa na Manesi Wasaidizi tu:- Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa afya wa kutosha katika maeneo hayo ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. RUKIA AHMED KASSIM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Hospitali ya Benjamin Mkapa ni kubwa, nzuri na ya kisasa ambayo inatumika kuwahudumia wananchi wa Dodoma, wanafunzi wa UDOM pamoja na sisi Wabunge, lakini ina tatizo kubwa sana la Madaktari pamoja na watumishi wengine. Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Madaktari ni kidogo sana.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambayo ndiyo mamlaka ya kusimamia Hospitali ya Benjamin Mkapa, inatambua kwamba tuna changamoto ya Madaktari Bingwa.
Mheshimiwa Spika, sasa hivi tumeweka mikakati ya kuainisha mahitaji ya Hospitali ya Benjamin Mkapa pamoja na Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na tutafanya mgawanyo kwa kuangalia yale maeneo ambayo yana Madaktari wa ziada na kuwapeleka katika Hospitali zote za Rufaa za Mikoa, ikiwa pamoja na Hospitali ya Benjamin Mkapa.
Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, katika mwaka huu wa fedha tumefadhili masomo ya Madaktari Bingwa 125 katika fani ambazo hatuna katika Hospitali za Rufaa za Mikoa, ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Benjamin Mkapa. Pindi Madaktari hao watakapomaliza watakuwa posted katika hospitali hizi.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Zahanati nyingi za Vijiji vya Mkoa wa Kigoma katika wilaya zote zina upungufu mkubwa sana wa watumishi wa afya na baadhi ya zahanati hazina Waganga hivyo huduma zinatolewa na Manesi Wasaidizi tu:- Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa afya wa kutosha katika maeneo hayo ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya vijijini?

Supplementary Question 5

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza naomba niishukuru Serikali kwa kuitupia sekta ya afya jicho la pekee katika Jimbo langu la Ulanga. Kituo cha Afya cha Lupilo karibu kinakwisha, sasa wananchi wa Ulanga wategemee nini katika huo mgawo? Siyo kwamba Madaktari ni wachache tu lakini ni pamoja na kuwa na watumishi wa afya wasio na sifa. Ulanga inakusikiliza sasa hivi Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Ulanga limepewa kipaumbele sana kwenye sekta ya afya, hilo naishukuru Serikali, hicho ndiyo kipaumbele cha Mbunge wao, kipaumbele cha kwanza afya, cha pili afya, cha tatu afya. Shida kubwa iliyopo ni watumishi wachache, Mheshimiwa Waziri katika majibu yake haya ya kugawa watumishi wa afya wananchi wa Ulanga wanamsikiliza sasa hivi anawaambia nini?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kwanza, naomba nitangulie kupokea shukrani anazozitoa, lakini naomba nimhakikishie nia ya Serikali ni kuhakikisha kwamba vituo vya afya na zahanati zetu zote zinafanya kazi iliyokusudiwa kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Spika, litakuwa ni jambo la ajabu tukamilishe kituo cha afya kizuri halafu kisiwe na watenda kazi. Katika wilaya ambazo zitapata watendaji kwa maana ya wahudumu wa afya pamoja na Waganga, nimhakikishie kwamba wale wenye sifa ndiyo ambao watapelekwa kwake, kwa hiyo, wananchi wategemee mambo mazuri kuhusiana na suala zima la afya.