Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE N. RUGE aliuliza:- Upatikanaji wa vifaa vya walemavu ni mdogo sana lakini gharama zake ni kubwa sana hali inayofanywa walemavu kushindwa kumudu, kwa mfano mguu bandia mmoja unauzwa shilingi milioni mbili. Je, ni lini Serikali itatoa agizo la kufutwa kodi za vifaa hivyo kama ilivyo katika nchi nyingine na kwa kuzingatia kauli mbiu ya Serikali ya kumkomboa mnyonge?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili ya nyongeza.
Swali langu la kwanza, natambua halmashauri zetu zote Tanzania zinatakiwa kuwapatia asilimia mbili vikundi vya ujasiriamali vya watu wenye ulemavu. Swali langu, je, ni kiasi gani cha pesa kilitolewa kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa vikundi vya watu wenye ulemavu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunapoelekea kwenye uchumi wa viwanda Serikali imewaandalia mazingira gani watu wenye ulemavu ili waweze kushiriki moja kwa moja kwenye uchumi huo kwa kupata fursa ya ajira, fursa ya kujiajiri kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo na fursa ya kupata masoko kwa ajili ya bidhaa zao? Ahsante.

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Catherine Ruge kama ifuatavyo, nikianza kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi na nzuri na majibu mazuri aliyoyatoa leo Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tukiendelea na hotuba ya Bajeti ya Waziri Mkuu jana suala hili la asilimia 10 katika mifuko ya Halmashauri za Wilaya ilijitokeza. Ninaomba nikubaliane na maelekezo ama kauli ya Serikali iliyotolewa na Waziri wa TAMISEMI jana kwamba maeneo yote yanayohusiana na asilimia 10 yatatolewa maelezo katika bajeti itakayoanza leo inayohusu Ofisi ya Rais, TAMISEMI na hivyo tutaweza kuwa na maelezo fasaha.
Lakini la pili, kuhusu namna nzuri ya kuwafanya watu wenye ulemavu kuingia nao katika uchumi wa viwanda, kama tulivyotoa maelezo jana wakati tunahitimisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, suala hili ni suala la kisheria liko ndani ya sheria ya watu wenye ulemavu namba tisa ya mwaka 2010. Kwa hiyo, sisi sasa tunachokifanya ni kusimamia sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe tu kutoa rai kwa watu wote na wawekezaji wote ambao wanaanzisha viwanda katika nchi yetu ya Tanzania kuona kwamba wenye ulemavu nao wanaouwezo wa kutoa mchango katika ujenzi wa taifa kupitia auchumi wa viwanda hivyo basi wawape fursa kwa kuzingatia sheria ambayo tuko nayo na sisi kama Wizara tutaendelea kusimamia kuona jambo hili linatekelezwa.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE N. RUGE aliuliza:- Upatikanaji wa vifaa vya walemavu ni mdogo sana lakini gharama zake ni kubwa sana hali inayofanywa walemavu kushindwa kumudu, kwa mfano mguu bandia mmoja unauzwa shilingi milioni mbili. Je, ni lini Serikali itatoa agizo la kufutwa kodi za vifaa hivyo kama ilivyo katika nchi nyingine na kwa kuzingatia kauli mbiu ya Serikali ya kumkomboa mnyonge?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Sambamba na ufutwaji wa kodi wa vifaa vya watu wenye ulemavu, je, ni lini Serikali itawagawia bure walemavu kwenye kaya maskini vifaa vya uhafifu hauoni kwa watu wenye ulemavu wa macho?

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. STELLA I. ALEX): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitoa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu kadri vinavyokuwa vinapatikana, kwa hiyo, hili ambalo ameliuliza dada yangu Sophia nimhakikishie tu kwamba Serikali itaendelea kutoa vifaa hivi. Hata hapa, muda mfupi uliopita kama wiki mbili/ tatu/mwezi mmoja uliopita tumekuwa na hilo zoezi la kugawa vifaa hivi saidizi. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kufanya hivyo kupitia bajeti zake lakini pia kupitia wadau mbalimbali wanajitokeza kusaidia kundi hili la watu wenye ulemavu (Makofi).