Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa maporomoko ya Ntomoko Wilayani Kondoa?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maporomoko ya Ntomoko ni janga kwa wananchi wanaoishi kandokando ya maporomoko haya. Wananchi wa Wilaya ya Chemba vijiji kumi na vijiji vitatu vya Wilaya ya Kondoa wamesubiri mradi huu kwa muda mrefu sana na fedha zilishatolewa zaidi ya bilioni mbili kwa ajili ya kukarabati mradi ule, watumishi ambao walizembea mradi ule hawajachukuliwa hatua yoyote. Wananchi wanateseka na hakuna jibu lolote linaloonesha kwamba hivi vijiji vitapata maji hivi karibuni.
Je, watumishi waozembea na wakapoteza zaidi ya shilingi bilioni mbili na kufanya mradi huu ukasimama wamechukuliwa hatua gani?
Swali la pili, mradi huu umekwishatembelewa na viongozi wengi na tumekwishachangia mara nyingi na Wabunge wa maeneo yale mimi na Mheshimiwa Juma Nkamia na Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji sasa hivi hatueleweki kwa wananchi.
Je, kuna mkakati gani wa haraka wa kuwapatia wananchi wa vijiji vile maji ili wasiendelee kuhangaika kwa sababu hata DUWASA wenyewe hawajapata fedha kwa ajili ya ule mradi? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WA WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda nimpongeze Mama yangu Felister Bura kwa namna ya kipekee anavyowapigania wananchi wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa ambalo nashukuru sana ni taarifa ambayo amenipa kama Naibu Waziri wa Maji, nataka nimhakikishie fedha za Serikali haziliwi bure. Kama kutakuwa na watumishi ambao kwa kuzembea au kwa maksudi fedha zile zimepotea, tutafanya mawasiliano ya haraka na watu wa Kondoa katika kuhakikisha hatua za haraka zitachukuliwa kwa watumishi wale ambao wamefanya uzembe wananchi waweze kupata taabu.
Swali lake la pili, amesema huu ni mradi wa muda mrefu sana nataka nimuhakikishie sisi ni Wizara ya Maji na jukumu letu ni kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama yenye kuwatosheleza na ndiyo maana tumeahidi kwamba katika bajeti hii ya mwaka 2018/2019 tumeshatenga fedha ili katika kuhakikisha mradi ule uweze kukarabatiwa kwa haraka ili wananchi wake waweze kupata majisafi salama na ya kuwatosheleza. Ahsante sana. (Makofi)

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba kumfahamisha Mheshimiwa Felister Bura kwamba kuna hatua za dharura ambazo tunaendelea nazo, tunachimba visima katika vijiji vyote eneo la Kondoa na tumeshaanza na visima 15 ili wananchi waendelee kupata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)