Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mtwango, Mninga na Makungu?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa vile kwenye Jimbo la Mufindi Kusini Wilaya ya Mufindi, tuna ujenzi wa hospitali ambayo ni kubwa sana.
Je, Wizara ya TAMISEMI mnaweza mkatusaidia kupata ramani ambayo ni standard kwa ajili ya kujenga hospitali pale Jimbo la Mufindi Kusini?
Swali langu la pili, kama alivyoeleza kwenye majibu yako kwamba tuna ujenzi mkubwa sana pale Malangali Kituo cha Afya. Kwanza naishukuru Serikali kwa kutupatia zile milioni 400; lakini kile kituo cha afya tunategemea kifunguliwe na mtu mkubwa sana. Je, Naibu Waziri uko tayari kutuunganisha na Waziri Mkuu aweze kufika pale Malangali kufungua kile kituo cha afya ili kianze kufanya kazi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kuipongeza Halmashauri kwa kazi nzuri waliyofanya kuhakikisha kwamba kituo cha afya kile kinakamilika na ni miongoni mwa vituo vya afya ambavyo vimejengwa kwa ustadi mkubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya suala la ujenzi wa hospitali ya Wilaya hitaji lake kubwa ni upatikanaji wa ramani, naomba nimhakikishie kwamba Wataalam wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI pamoja na Wataalam Wizara ya Afya, wako mbioni kukamilisha ramani ambazo zitatumika katika ujenzi wa Hospitali za Wilaya hizo 67 ikiwemo ya kwake ya Mufindi. (Makofi)
Swali lake la pili anaomba Ofisi ya Rais, TAMISEMI imuunganishe uwezekano wa Mheshimiwa Waziri Mkuu kuwa miongoni mwa watu watakaoenda kuzindua kituo chake cha afya. Naomba nimhakikishie utaratibu unaandaliwa chini ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutaanza vituo 44 vyote vile ambavyo vimejengwa na kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunatarajia pale Mheshimiwa Rais kwa nafasi yake na jinsi atakavyoridhia kutakuwa na uzinduzi ambao utafanyika nchi nzima tukianzia na hivyo vituo 44; sina uhakika sasa kwa nafasi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kama ataweza kwenda kuzindua kwake. (Makofi)

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mtwango, Mninga na Makungu?

Supplementary Question 2

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nishukuru Serikali kwa jitihada zake za ku-support ujenzi wa vituo vya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika jimbo langu la Kwela tunavyo vituo vya afya ambavyo vimeanza kujengwa toka mwaka 2004 na wananchi wamejenga mpaka jengo la OPD kukamilika, lakini vituo hivyo mpaka sasa vimesimama kwa sababu havijapata fedha tena. Vituo hivyo ni Kituo cha Ilemba, Kahoze na Muze.
Je, ni lini Serikali itatoa fedha ku-support wananchi juhudi zao?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anauliza ni lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kumalizia vituo vya afya ambavyo vimeanzishwa na wananchi muda mrefu.
Kwanza naomba nimtaarifu kwamba nia njema ya Serikali ya kuhakikisha kwamba huduma ya afya inafika kila mahali ikiwa ni pamoja na Wilaya yake, katika hospitali 67 ambazo zinaenda kujengwa za Wilaya na Wilaya yake ni miongoni mwa hospitali ambazo zitaenda kujengwa. Hiyo ni nia njema ya Serikali kuhakikisha kwamba huduma inapelekwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na hivyo vituo vyake kama nilivyojibu kwenye swali la msingi pale pesa inapopatikana hakika naomba nimhakikishie na hii itakuwa miongoni mwa vituo vya afya ambavyo vitaboreshwa ili viweze kutoa huduma tunayoitarajia.(Makofi)