Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:- Katika kutekeleza azma ya Tanzania ya viwanda. Je, Halmashauri ya Momba inatarajiwa lini kujengewa kiwanda na cha aina gani?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuwa ya jumla kwa sababu swali nililouliza nilitaka nijue kama Momba kitapatikana kiwanda, kitajengwa au hakitajengwa. Kwa hiyo, jibu ni kwamba wananchi wa Momba huko mnakonisikia hamna kiwanda kitakachojengwa na Serikali ya Awamu ya Tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu ya Mheshimiwa Waziri yanaainisha kwamba jukumu la ujenzi wa viwanda ni la sekta binafsi, lakini kauli za Serikali na viongozi wa Serikali mitaani huko, kila siku statement ambazo wamekuwa wakizitoa ni kwamba Serikali inajenga viwanda. Ni kwa nini sasa Serikali isibadilishe kauli yake ikawaambia wananchi jukumu la kujenga viwanda sio la Serikali, Serikali kazi yake ni kuwezesha mazingira wezeshi kama ambavyo mmekuwa mkitamka hapa. Ninayasema haya kwa sababu tumekuwa tukisia hapa…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio nataka niulize kabisa kwamba kwa nini sasa wasibadilishe hiyo kaulimbiu kwa sababu mind set ya wananchi ni kwamba Serikali inajenga viwanda wakati ukweli ni kwamba Serikali haijengi viwanda?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali imejinasibu hapa kwamba inaweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi pamoja na wafanya biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ninachotaka nijue jitihada za Serikali juu ya hawa watu wa sekta binafsi kwa sababu moja kumekuwa na malalamiko, mazingira wezeshi kwa mfano huko Momba barabara mbovu, maji hayapatikana, umeme unayumbayumba, mitaji hakuna, riba zimekuwa zinapitiliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka nijue jitihada za Serikali kukabiliana na changamoto hizi ili hii sera ya viwanda iweze kuwa inatekelezeka.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo linalofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano si la kuamka na kufanya. Tunafuata Dira ya 2025, tunafuata Mpango wa Pili wa Miaka Mitano na tunafuata maelekezo ya Mheshimiwa Rais. Imeandikwa katika Mpango wa Pili wa Miaka Mitano kwamba Serikali jukumu lake ni kuweka mazingira wezeshi na kazi ya sekta binafsi ni kujenga viwanda. Sasa sisi Tanzania sisi Serikali ya Awamu ya Tano tunajenga viwanda sisi sekta binafsi sisi ni Serikali tunakwenda pamoja huwezi kutenganisha sekta binafsi na Serikali. Huyo anatengeneza mazingira wezeshi huyu anajenga. Huyu anachota maji, huyu anasonga ugali wote mnapika chakula. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Silinde rafiki yangu usisahau umeme wa Momba kama si Serikali, kama sio mimi nikiwa Naibu wa Nishati usingefika. Tumefyeka msitu, sasa ushukuru kwa kidogo ulichopata nije nikupatie kingine.

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:- Katika kutekeleza azma ya Tanzania ya viwanda. Je, Halmashauri ya Momba inatarajiwa lini kujengewa kiwanda na cha aina gani?

Supplementary Question 2

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikijinasibu kuwa ina mpango wa kujenga viwanda 100 kwa kila mkoa...
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikieleza kuwa ina mpango wa kujenga viwanda 100 kila mkoa na mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa na viwanda vingi tangu enzi za Mwalimu. Lakini hivi sana viwanda vingi vimekufa na vimegeuka kuwa ma-godown, mfano wa viwanda hivyo ni Kiwanda cha Komoa, Kiwanda cha Tanzania Leather Shoes, Kiwanda cha CERAMIC, Kiwanda cha U-nuts, sasa Serikali haioni kama kuna umuhimu wa kufufua viwanda vilivyokuwa ndipo ije na wazo la kujenga viwanda vipya. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza tunamshukuru kwa ufuatiliaji. Ni kweli Serikali iko serious kuona kwamba viwanda vingi vinajengwa Tanzania hasa katika kuongeza thamani mazao ya wananchi tulio nao jirani na viwanda hivyo kama ambavyo nimekuwa nikisistiza kila wakati viko katika ngazi za aina mbalimbali. Kuna viwanda vidogo sana, viwanda vidogo, viwanda vya kati na viwanda vikubwa. Kwa hiyo, wananchi wenye mitaji midogo wanao uwezo pia wa kuanzisha viwanda kulingana na hali inayowezekana.
Sasa suala la viwanda vya zamani ambavyo havifanyi kazi, kwanza tufahamu kwamba kiwanda kina tabia sawa sawa na binadamu. Kiwanda kinapokosa mazingira mazuri na wezeshi kinaweza kufa sawa na binadamu anavyokufa. Kwa hiyo, ni wajibu wetu sasa hivi kuhakikisha kuwa tunajenga mazingira wezeshi ikiwemo kupunguza au kuondoa kabisa vifo vya viwanda na hiyo ndiyo kauli mbiu na hiyo ndiyo jitihada inayofanyika ndiyo maana unakuta jitihada mbalimbali zinaendelea.
Kwa hiyo, Morogoro ni sehemu mojawapo ambayo tayari tumeshaitembelea na hivyo viwanda ambavyo unasema vimekuwa havifanyi kazi vizuri kama Leather Industries tayari tuko katika mchakato wa kuhakikisha kwamba makongano mbalimbali ya leather yanafanyika ili kuhakikisha viwanda hivyo vinakuwa vizuri na kuleta tija kwa Taifa. Na nizidi kuwaomba watanzania wengi msitishike, nimetembelea viwanda. Zaidi ya viwanda nilivyotembelea asilimia 90 vingi vinaendeshwa na sisi Watanzania wenyewe. Kwa hiyo, tujitoe hata sisi Wabunge tuanzishe viwanda kadiri inavyowezekana kulingana na mahitaji ya maeneo yetu.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:- Katika kutekeleza azma ya Tanzania ya viwanda. Je, Halmashauri ya Momba inatarajiwa lini kujengewa kiwanda na cha aina gani?

Supplementary Question 3

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa inayoongoza katika uzalishaji wa maembe. Mpaka jina la Unyanyembe likapatikana ni kutokana na uzalishaji wa hizo embe, lakini cha ajabu mkoa huo wa Tabora mpaka leo hauna kiwanda cha usindikaji wa maembe, hali inayopelekea maembe yanazagaa kila mahali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka niiulize Serikali ni kwanini haitaki kujenga Kiwanda cha Usindikaji wa Maembe Tabora?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba nirejee tena nazidi kuhamasisha Watanzania pamoja na Waheshimiwa Wabunge tuendelee kuwahamasisha wawekezaji katika maeneo hayo. Kwa mfano hapa Dodoma kuna Kiwanda kizuri cha Matobolo wanasindika maembe wanakausha na maembe hayo yanaweza kutumika kwa muda mrefu. Kwa hiyo, sisi tusisubiri kiwanda kije chenyewe ni lazima tuwahamasishe wadau mbalimbali hata sisi wenyewe tuweze kuwekeza ili kuhakikisha kuwa maembe hayo yanakaa muda mrefu.