Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Katika Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Njombe, Tarafa ya Lupembe, hususan Kijiji cha Madeke kinazalisha matunda aina ya nanasi, parachichi na matunda mengine, lakini hakuna soko la matunda hayo na hii ni kutokana na kutokuwa na kiwanda kikubwa cha matunda. • Je, Serikali inasaidiaje upatikanaji wa masoko ya mazao hayo? • Je, ni lini Serikali italeta kiwanda katika eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda hiki kilinunuliwa kwa shilingi milioni 100 mwaka 2013 na mwaka huo huo Waziri Mkuu, Mheshimiwa Pinda ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu alifungua hiki kiwanda na tangu alipofungua mpaka leo hii hakijazalisha hata tani moja. Je, ni lini Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Bisahara na Uwekezaji atakaa na Mheshimiwa Waziri wa Nishati, ili waweze kupeleka umeme haraka kwa kuwa, tatizo ni nishati?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili pia ni lini sasa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji ataongozana na mimi kwenda Madeke kujionea mwenyewe jinsi wananchi wale wanavyopoteza fedha nyingi/mabilioni ya fedha, kutokana na kukosa soko la kuuza haya mananasi na matunda mengine? Ahsante sana.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Hongoli kwa jitihada kubwa anayoifanya katika kufuatilia kiwanda hiki na tija kwa wakulima wa matunda ya eneo hilo, lakini vilevile nichukue nafasi hii ya pekee kabisa kumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Nishati kwa jitihada kubwa ambayo anaifanya katika kuhakikisha kwamba, umeme unapelekwa hasa katika maeneo ambayo tunatarajia kuwa na uzalishaji mkubwa na kuongea thamani katika matunda na eneo hili tayari tumeshafanya hayo mazungumzo.
Kwa hiyo, niseme tu kwamba, ni rai yangu kwa wadau wengi kuona kwamba, umeme wa REA unaoombwa katika vijiji kweli uwe na tija na hivi tufanye uzalishaji kwa sababu gharama za kupeleka umeme katika maeneo hayo ni kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, suala la kuongozana hiyo itakuwa ni bahati ya pili kwa sababu, bahati ya kwanza tayari Mheshimiwa Waziri wangu mwezi huu ulioisha wa tatu alishaenda mpaka Njombe na amejionea hali halisi na vilevile tunategemea kujenga shades kwa ajili ya viwanda vidogo pale Njombe.
Kwa hiyo, mimi sina taabu nitaenda, nakubali kwenda huko. Ahsante.

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Katika Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Njombe, Tarafa ya Lupembe, hususan Kijiji cha Madeke kinazalisha matunda aina ya nanasi, parachichi na matunda mengine, lakini hakuna soko la matunda hayo na hii ni kutokana na kutokuwa na kiwanda kikubwa cha matunda. • Je, Serikali inasaidiaje upatikanaji wa masoko ya mazao hayo? • Je, ni lini Serikali italeta kiwanda katika eneo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipatia nafasi, ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Tatizo lililopo Lupembe linafanana kabisa na tatizo lililopo Mtwara Mjini, viwanda vingi vimekufa ikiwemo Kiwanda cha Kubangulia Korosho cha Oram ambacho kilikuwa kinatoa ajira kwa wananchi wengi wa Mkoa wa Mtwara. Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua viwanda hivyo?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge, kupitia Sera yetu ya Uendelezaji wa Viwanda endelevu, sisi wenyewe kama nchi tuliona kwamba, masuala yote yanayohusiana na uzalishaji yaondoke sasa kwenye mikono ya Serikali iende katika mikono ya sekta binafsi. Jambo ambalo tunafanya sisi ni kuhakikisha kuwa tunaweka mazingira wezeshi kwa kuhakikisha kuwa ile miundombinu inayohitajika pamoja na uunganishaji wa taarifa na vikwazo vyote ambavyo vinawakabili hao wawekezaji viweze kutatuliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa korosho, kwanza tunashukuru kwamba kwa sasa hali ya korosho/bei ya korosho imekuwa ni nzuri, lakini sisi kama Taifa tusingependa tu kuuza korosho zikiwa ghafi. Kwa misingi hiyo, tunaendelea kufanya jitihada ya kuhakikisha kuwa viwanda mbalimbali vya korosho vinaimarishwa ili kuhakikisha kuwa tunapata tija katika zao hili.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Katika Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Njombe, Tarafa ya Lupembe, hususan Kijiji cha Madeke kinazalisha matunda aina ya nanasi, parachichi na matunda mengine, lakini hakuna soko la matunda hayo na hii ni kutokana na kutokuwa na kiwanda kikubwa cha matunda. • Je, Serikali inasaidiaje upatikanaji wa masoko ya mazao hayo? • Je, ni lini Serikali italeta kiwanda katika eneo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Ukerewe ni wazalishaji wakubwa wa matunda hasa machungwa na nanasi. Lakini wananchi wa Ukerewe wamekuwa hawafaidiki sana na matunda haya kwa sababu sehemu kubwa ya matunda imekuwa ikiharibika kwa sababu ya kukosa soko.
Je, Serikali iko tayari kusaidia upatikanaji wa kiwanda cha kusindika matunda haya ili wananchi wa Ukerewe wapate soko la uhakika wa matunda yao?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba bado tunayo changamoto katika usindikaji wa matunda. Na katika mtazamo wetu Tanzania tunajipanga zaidi katika huu ukuzaji wa viwanda hasa katika eneo la kilimo na manasi pamoja na machungwa ni mazao mojawapo ambayo yana changamoto. Jambo ambalo tunaliona sasa hivi ni kwamba iko haja ya kuunganisha taasisi zetu hasa katika kukuza teknolojia zitakazowezesha matunda yanapokuwa yamezalishwa, yasiharibike kiurahisi na kuyaongezea thamani.
Lakini vilevile nikuombe Mheshimiwa Mbunge ukiwa ni sehemu ya uhamasishaji pamoja na Serikali kuendelea kuwahamasisha wadau binafsi kwa ajili ya kuwekeza viwanda katika eneo hilo.