Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- (a) Je, Mabaraza ya Wazee katika Mahakama za Mwanzo yapo kwa mujibu wa sheria? (b) Mahakama ya Mwanzo Kizuiani hulipa posho za Wazee wa Baraza kiasi cha shilingi 5,000 kila wanapomaliza shauri. Je, kwa nini sasa yapata miezi tisa wazee katika Mahakama ya Mwanzo Kizuiani hawajalipwa posho zao?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa posho ya shilingi 5,000 kwa kila shauri ni ndogo sana ukilinganisha na wakati uliopo kuwalipa hawa wazee. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea posho hawa wazee wa Mahakama za Mwanzo shilingi 5,000 ni ndogo sana? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa wazee wanakuwa kwenye Mahakama kwa muda mrefu sana kusikiliza mashauri hayo. Je, Serikali haioni haja sasa kubadili mfumo wa malipo, badala ya kuwalipa kwa miezi mitatu au minne kwa mkupuo, wawalipe kwa mwezi hadi mwezi yaani kwa mwezi mmoja mmoja? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali lake la kwanza la ongezeko la posho kutoka shilingi 5,000 kwanza kabisa nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba wazee hawa wanafanya kazi kubwa kuisaidia Mahakama katika kufikia maamuzi na sisi kama Serikali tunatambua mchango wao mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba siwezi kutoa commitment ya Serikali hapa kuhusiana na ongezeko la hii fedha lakini pindi bajeti itakaporuhusu basi tunaweza tukaona namna ya kuweza kusaidia katika kuboresha eneo hili la kipato kwa wazee hawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la pili la malipo ya mwezi kwa mwezi badala ya mkupuo. Kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ni kwamba inafanyika hivi pia kwa ajili ya kupata kumbukumbu sahihi. Lakini vilevile pia inatokana sana na upatikanaji wa fedha kwa wakati kulingana na bajeti, tunalipokea wazo la Mheshimiwa Mbunge na Serikali tutaona namna ya kuweza kulifanyia kazi.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:- (a) Je, Mabaraza ya Wazee katika Mahakama za Mwanzo yapo kwa mujibu wa sheria? (b) Mahakama ya Mwanzo Kizuiani hulipa posho za Wazee wa Baraza kiasi cha shilingi 5,000 kila wanapomaliza shauri. Je, kwa nini sasa yapata miezi tisa wazee katika Mahakama ya Mwanzo Kizuiani hawajalipwa posho zao?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Ukonga kwa sasa lina wakazi wanaokaribia 700 na tuna Mahakama ya Mwanzo moja tu pale ya Ukonga na kulikuwa na mpango mwaka jana kujenga Mahakama nyingine mpya ya Mwanzo kule Chanika. Kwa hiyo, ningependa kujua kupitia Mheshimiwa Naibu Waziri kama mpango huo wa kujenga Mahakama nyingine mpya pale ili kupunguza msongamano mkubwa kule Ukonga ukoje? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa Serikali wa mwaka 2017/2018; 2018/2019; 2019/2020 ni kuendelea kuongeza Mahakama nyingi za Mwanzo na Wilaya ili wananchi wengi waweze kupata huduma kwa wakati. Katika Mahakama ambazo zimeorodheshwa, pia Mahakama ambayo ni katika jimbo la Mheshimiwa Waitara ni kati ya Mahakama ambazo zilikuwa zimeainishwa katika wakati ujao wa fedha ili kuona namna ya kuweza kulishughulikia suala hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu hivi sasa chini ya Wizara ya Katiba na Sheria utaratibu ulioanzishwa sasa hivi ni ujenzi wa Mahakama kwa kutumia teknolojia rahisi sana ya moladi ambayo imerahisisha sana kujenga Mahakama nyingi kwa wakati mfupi.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge anaweza pia, kuwasiliana na mimi ili kuangalia katika orodha ya ujenzi wa Mahakama zile, Mahakama zake za Ukonga zimepangiwa mwaka gani wa fedha.