Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa (ambulance) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka takribani majimbo manne?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Handeni inahudumia karibia majimbo manne; na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekubali hili ni suala la dharura haoni kwamba kuna umuhimu wa sisi kupata ambulance badala ya kutumia haya magari ya kawaida ambayo muda mwingi vifo hutokea njiani kwa sababu sio magari special ya kusafirisha wagonjwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba uko uhitaji mkubwa sana wa gari la wagonjwa na pia ni ukweli usiopingika kwamba uwezo wa Halmashauri kuweza kununua gari jipya kwa sasa hivi ni mdogo sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kulitambua hilo ndiyo maana Halmashauri ya Handeni imetuma ombi maalum Wizara ya Fedha ili kuomba gari la wagonjwa liweze kununuliwa. Naamini hali ya bajeti ikitengemaa ombi lao litaweza kujibiwa na wagonjwa waweze kupata gari ambalo litakuwa linamudu kwa mazingira ya Wilaya ya Handeni.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa (ambulance) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka takribani majimbo manne?

Supplementary Question 2

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Lulindi nilitaka nimuulize Mheshimiwa Waziri kwamba kwa kuwa Kituo cha Afya cha Nagaga kilichopo katika Jimbo la Lulindi, Wilayani Masasi liliungua moto miaka mitano iliyopita. Je, Serikali haioni umuhimu sasa katika mgao huu wa magari yaliyopatikana kupeleka katika Kituo cha Afya cha Nagaga ili huduma za afya ziendelee kuboreka? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli uko uhitaji mkubwa sana wa magari ya wagonjwa. Kama ambavyo Serikali ingependa yote tukaweza kuyatatua kwa mara moja, lakini pia ni ukweli usiopingika kwamba bajeti hiyo kwa sasa haiwezekani kwa wakati mmoja tukatekeleza yote hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge ajue nia njema ya Serikali ndiyo maana katiak orodha ya Wilaya zile 27 ambazo zinaenda kujengewa Hospitali za Wilaya ni pamoja na Wilaya yake. Kwa hiyo, aelewe dhamira njema ya Serikali na kadri uwezo utakavyokuwa unajitokeza hakika hatutawasahau.

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa (ambulance) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka takribani majimbo manne?

Supplementary Question 3

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jiografia ya Jimbo na Halmashauri ya Wilaya ya Msalala wewe unaifahamu lakini pia hata Mheshimiwa Kandege anaifahamu kwamba vituo vya afya vimejengwa sana na wananchi na hivi sasa tuna vituo vya afya vitatu, cha Isaka, Ngaya na Bugarama. Lakini vituo vyote hivi havina gari la wagonjwa na kwa Halmashauri nzima gari ambalo linafanya kazi ni gari moja tu. Wananchi wamefanya kazi kubwa na wanaamini Serikali yao pia inaweza ikawashika mkono.
Kwa hiyo, nilitaka kujua Mheshimiwa Waziri unawaahidi nini wananchi hawa angalau kuwapatia gari angalau kwenye kituo kimoja katika hivi vitatu nilivyovitaja?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna Halmashauri za kupigiwa mfano na kama kuna Wabunge ambao wanatakiwa wapongezwe ni pamoja na Mheshimiwa Maige. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni katika Halmashauri ambazo wamejenga vituo vya afya vingi, hongereni sana. Pia nimuombe Mheshimiwa Maige kwa kushirikiana na Halmashauri yake, natambua uwezo mkubwa wa Halmashauri yake hakika wakiweka kipaumbele kama ni suala la kununua gari hawashindwi na wengine wataiga mfano mzuri ambao wao wanafanya na hasa katika own source zao ambao wanapata mapato mazuri ni vizuri katika vipaumbele wakahakikisha wananunua na gari la wagonjwa kwa ajili ya kusaidia wananchi wa Msalala.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa (ambulance) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka takribani majimbo manne?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale yenye kata 20 na kituo kimoja cha aya haina gari ya wagonjwa. Shida tuliyonayo ni kubwa sana ukizingatia mtawanyiko wa kata zetu zile pale Wilaya ya Liwale mwenyewe Mheshimiwa Naibu Waziri ni shahidi, umefika, umeona jinsi shida ya Wilaya ya Liwale ilivyo juu ya kupata gari la wagonjwa. Ni lini sasa Serikali itatupatia gari la wagonjwa katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Liwale? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika fursa nikiwa nahudumu katika nafasi ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais, TAMISEMI nimepata nafasi ya kwenda Liwale na tukakutana na Mheshimiwa Mbunge katika kazi nzima ya kujenga kituo cha afya na muitikio wa wananchi wa Liwale ni mkubwa sana katika kujitolea katika shughuli za maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie kwa spirit niliyoiona na hakika na mapato ambayo wanapata kutokana na zao la korosho na wakasimamia vizuri kabisa mapato ya kwao na kituo kile cha afya kikikamilika hitaji la kwanza la wananchi naomba nimuagize Mkurugenzi katika vipaumbele vyake vya kwanza ni pamoja na kuhakikisha kwamba wananunua gari la wagonjwa kwa sabbau wezo upo, pesa zikisimamiwa vizuri, kulikoni kuishia kugawana kama posho hakika uhitaji mkubwa wa gari la wagonjwa wafanye kama kipaumbele.