Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi unaoendelea katika Vituo vya Afya Ikuti, Wilayani Rungwe na Ipinda Wilayani Kyela utakamilika ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kupata huduma kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na jibu la msingi la Mheshimiwa Waziri bado kuna shida katika ujenzi unaoendelea pale Ipinda, nilikuwa nataka kujua Serikali imefuatilia gharama ya pesa ilizotoa na uhalisia wa majengo yanayojengwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ujenzi wa zahanati ni kitu kingine, lakini utendaji wa wafanyakazi ikiwemo madaktari ni shida hasa Zahanati ya Ikuti Rungwe na hapo Ipinda hakuna watendaji wa kazi. Ni lini Serikali itatoa wafanyakazi ikiwemo madaktari na hasa Madaktari Bingwa wa wanawake kusaidia wanawake wa Wilaya ya zahanati ya Ipinda lakini pia Zahanati ya Ikuti Wilaya ya Rungwe?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwakagenda kama ifuatavyo:-
Katika swali lake la kwanza anauliza iwapo Serikali imefuatalia kujua gharama iliyotumika na majengo ambayo yamejengwa. Majengo ambayo yanajengwa ni kwa mujibu wa ramani ambayo imetolewa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI na ni na suala ambalo matarajio yangu makubwa na Mheshimiwa Mbunge akiwa ni sehemu ya wananchi wa Halmashauri ile ni vizuri akatuambia ni sehemu ipi ambayo anadhani kwamba haridhiki, lakini mpaka sasa hivi ninavyoongea hata Mbunge wa Jimbo hajaleta malalamiko yoyote kwamba labda kuna ubadhilifu katika ujenzi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili anaongelea juu ya suala zima la upatikanaji wa wataalam, suala la kujenga majengo jambo moja na suala la wataalam jambo la pili, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni nia ya Serikali kuhakikisha pale tunapomaliza ujenzi na wataalam wapatikane kwa mujibu wa Ikama na jinsi mahitaji yanavyopatikana.

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi unaoendelea katika Vituo vya Afya Ikuti, Wilayani Rungwe na Ipinda Wilayani Kyela utakamilika ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kupata huduma kwa wakati?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza sina budi kushukuru vyombo vya ulinzi na usalama hasa Kibiti tunalala usingizi.
Swali langu la nyongeza Kituo cha afya kibiti hasa kinazidiwa kutoa huduma, je, Serikali ina mpango gani wa kuijengea Kibiti Hospitali ya Wilaya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli huko uhitaji mkubwa sana na kituo cha afya kilichopo kimezidiwa, naomba nimuondoe mashaka Mheshimiwa Mbunge na nimuhakikishie miongoni mwa hospitali 67 zinazotarajiwa kujengwa ni pamoja na Wilaya yake, kwa hiyo, wakae mkao wa kula Serikali inatekeleza ili kuondoa shida kwa wananchi. (Makofi)

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi unaoendelea katika Vituo vya Afya Ikuti, Wilayani Rungwe na Ipinda Wilayani Kyela utakamilika ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kupata huduma kwa wakati?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu nilipata ahadi kutoka Wizara hii kwamba kutapelekwa hela za ujenzi kituo kile cha Mchombe katika Jimbo la Mlimba kiliwekwa katika mpango wa Serikali na kilipata zile grade ambazo zinafaa kupewa pesa ili kuboresha Kituo cha Afya cha Mchombe ambapo kinahutubia kata zisizopungua 10. Je, na katika mpango uliopita hakuna hela iliyopelekwa, mimi tu mfuko wa jimbo nilipeleka hela kidogo kwa ajili ya kusaidia…
Je, ni lini sasa Wizara ya afya itapeleka pesa za kuimarisha Kituo cha Afya cha Mchombe ndani ya Jimbo la Mlimba?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Susan Kiwanga swali lake la nyongeza juu ya ahadi ambayo anasema ilitolewa, sina uhakika juu ya ahadi hiyo, lakini kama ahadi hiyo imetolewa kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba nimuhakikishie hivi karibuni ni kama nilivyojibu swali la nyongeza jana la Mheshimiwa Mipata kuhusiana na kituo chake cha afya Kasu kuna matarajio ndani ya mwezi huu kuna pesa ambazo zitapatikana kwa ajili ya vituo vya afya visivyopungua 25.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sina uhakika kama katika hivyo 25 na yeye ni miongoni mwa hivyo ambavyo vinaenda kupelekewa pesa.