Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. ANTHONY C. KOMU (K.n.y. MHE. ZITTO Z. R. KABWE) aliuliza:- Mnamo tarehe 26 Julai, 2017, Mawaziri wa Uchukuzi wa Uganda, Burundi, Congo DRC na Tanzania walifanya mkutano katika Manispaa ya Ujiji-Kigoma na kuazimia kuwa kuanzia Januari, 2018, Bandari ya Kigoma itakuwa bandari ya mwisho kwa bidhaa ya Burundi na Mashariki ya DRC (Kigoma Port of Destination CIF Kigoma). Pamoja na Azimio hilo, mradi wa Bandari ndogo za Ujiji na Kibirizi zilipaswa kujengwa na kuiwezesha miradi kama ya Ujiji City-Great Lakes Trade and Logistics Centre:- Je, Serikali mpaka sasa imefikia hatua gani ya kiforodha na kibandari kuiwezesha CIF-Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. ANTHONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba bandari hii au mradi huu ni wa muhimu na utaleta nafuu kubwa sana kwa wananchi wa Kigoma, naomba Serikali iwaambie watu wa Kigoma, kwa kuwa mradi huu umeshachelewa sana, imetenga kiasi gani kwa bajeti inayokuja kwa ajili ya kuhakikisha sasa mradi huu unaanza mara moja? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kule Moshi tuna tatizo kama hili la Kigoma, tuna Stendi ya Kimataifa inapaswa kujengwa pale na Benki ya Dunia iko tayari kutoa fedha. Nataka nijue kutoka Serikalini, ni lini kibali kitatoka kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi hiyo li tuweze kunufaika na huo msaada kutoka World Bank?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kazi inayofanyika sasa hivi kama nilivyoeleza katika jibu la msingi ni kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kazi hiyo ikishakamilika wale ndiyo watatupa gharama zinazostahili kufanya kazi husika na ndipo tutakapojua tunatumia gharama gani katika ujenzi wa hiyo sehemu ambayo Mheshimiwa Mbunge anaifuatilia.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili kuhusu stendi, nikiri kwamba umuhimu wa kuwekwa stendi hiyo ni mkubwa sana kwa sababu ni kweli Benki ya Dunia imeonesha nia ya kufadhili. Hata hivyo, bado Serikali inaendelea na majadiliano na Benki ya Dunia kuangalia namna nzuri itakayofanya ili kuhakikisha ujenzi wa stendi hiyo unafanyika. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. ANTHONY C. KOMU (K.n.y. MHE. ZITTO Z. R. KABWE) aliuliza:- Mnamo tarehe 26 Julai, 2017, Mawaziri wa Uchukuzi wa Uganda, Burundi, Congo DRC na Tanzania walifanya mkutano katika Manispaa ya Ujiji-Kigoma na kuazimia kuwa kuanzia Januari, 2018, Bandari ya Kigoma itakuwa bandari ya mwisho kwa bidhaa ya Burundi na Mashariki ya DRC (Kigoma Port of Destination CIF Kigoma). Pamoja na Azimio hilo, mradi wa Bandari ndogo za Ujiji na Kibirizi zilipaswa kujengwa na kuiwezesha miradi kama ya Ujiji City-Great Lakes Trade and Logistics Centre:- Je, Serikali mpaka sasa imefikia hatua gani ya kiforodha na kibandari kuiwezesha CIF-Kigoma?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Swali hili lina umuhimu wa pekee kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma na napenda nimuulize swali moja dogo Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Bandari za Ujiji na Kibirizi unakwenda sambamba na ujenzi wa Bandari ya Nchi Kavu ya Katosho ambayo tayari Serikali imeshalipa fidia kwa wananchi wale. Napenda kujua, je, ujenzi wa Bandari ya Nchi Kavu ambayo tayari Serikali imeshalipa fidia wananchi wale unaanza lini maana sasa ni takribani mwaka mmoja tangu wananchi wale wamelipwa fidia? Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe shukurani za dhati kwa jinsi anavyojitahidi kupigania bandari za mkoa ambao anatokea. Ni kweli kwamba wakati huu mchakato wa usanifu wa kina na upembuzi yakinifu ukiwa unaendelea tayari Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari imekwishatangaza tenda kwa ajili ya kuanza ukarabati wa gati katika eneo la Kibirizi na Ujiji pamoja na Ofisi ya Meneja wa Mkoa wa TPA ili vyote viende sambamba kwa tenda moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la Katosho nalo limeingizwa katika package ya peke yake ya kuanza kujenga sakafu kubwa ili treni inapopita pale kabla ya kufika kituo cha mwisho cha Kigoma iweze kuanza kushusha mizigo ambayo itakuwa inaweza kusafirishwa kwenye nchi jirani na maeneo ya mikoa ya jirani ikiwemo Kigoma. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. ANTHONY C. KOMU (K.n.y. MHE. ZITTO Z. R. KABWE) aliuliza:- Mnamo tarehe 26 Julai, 2017, Mawaziri wa Uchukuzi wa Uganda, Burundi, Congo DRC na Tanzania walifanya mkutano katika Manispaa ya Ujiji-Kigoma na kuazimia kuwa kuanzia Januari, 2018, Bandari ya Kigoma itakuwa bandari ya mwisho kwa bidhaa ya Burundi na Mashariki ya DRC (Kigoma Port of Destination CIF Kigoma). Pamoja na Azimio hilo, mradi wa Bandari ndogo za Ujiji na Kibirizi zilipaswa kujengwa na kuiwezesha miradi kama ya Ujiji City-Great Lakes Trade and Logistics Centre:- Je, Serikali mpaka sasa imefikia hatua gani ya kiforodha na kibandari kuiwezesha CIF-Kigoma?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Tarehe 5 Agosti, 2017 wakati Rais alipokuja kuweka jiwe la msingi la bomba la mafuta pale Chongoleani-Tanga, tarehe 6 alizundua Kiwanda kipya cha Saruji cha Kilimanjaro na alinipa nafasi ya kuongea kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilimtaka Mheshimiwa Rais kupitia Serikali ya Awamu ya Tano kufanya categories za mizigo katika bandari zetu. Nataka kujua, mpango ule umeishia wapi kwa sababu Bandari ya Tanga sasa hivi inafanya kazi chini ya kiwango na hata vifaa vya kisasa vya kuteremsha makontena ya fourty feet hakuna, Waziri ananiambiaje?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, CHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama Mheshimiwa Mbunge ni mfuatiliaji mzuri nadhani atakuwa shahidi kwamba sasa hivi Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari imekwishaanza marekebisho na matayarisho ya kupanua Bandari ya Tanga. Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba Bandari ile ya Tanga inakwenda sambamba na wingi wa mizigo ambayo inategemewa kuanza kupatikana kupitia ujenzi wa bomba la mafuta la Hoima. Kwa hiyo, namwomba tu Mheshimiwa Mbunge asiwe na mashaka kuna utekelezaji wa upanuzi wa Bandari ya Tanga unaoendelea na wakandarasi wako pale wameshaanza kazi hiyo. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.