Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- Kuna ongezeko la bidhaa bandia na zisizo na viwango zinazoingizwa nchini, miongoni mwa bidhaa hizo ni pembejeo za kilimo, madawa ya mifugo, dawa za binadamu, vyakula, vinjwaji, vifaa vya nyumbani na kadhalika. (a) Je, ni hasara gani imepatikana kwa mwaka mmoja uliopita kutokana na bidhaa hizo kuingizwa nchini na kutumiwa na wananchi? (b) Je, ni hatua gani zinachukuliwa kukomesha bidhaa hizo kuingia nchini hasa maeneo ya vijijini ambako uelewa wa watumiaji ni mdogo na maafisa wadhibiti ni wachache?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante; nashukuru kwa majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali mawili ya ufafanuzi. Kwa kuwa tumeshuhudia kwenye luninga wakiteketeza vifaa hivi na wanaoingiza kupata hasara, Je, ni hatua gani zaidi zinazochukuliwa kwa wale wanaoingiza ili kukomesha hali hii?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa vifaa bandia havitoki tu nje ya nchi, vingine vinatengenezwa humu humu nchini. Mimi naomba kujua ni hatua gani zinazochukuliwa na Serikali ili kukomesha kabisa vifaa hivyo, vikiwemo viatilishi, pembejeo za kilimo, vipodozi vya kina mama, na hata vingine ambavyo si rahisi kutamka hapa hadharani? Naomba kujua. (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI):
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza nakiri na amekubali jibu kwamba kweli vile vifaa vinateketezwa na yeye mwenyewe ameona; lakini ni hatua gani zinachukuliwa sasa kwa wale ambao wameshikwa na hizo bidhaa bandia.
Mheshimiwa Spika, ni kwamba, tunazo sheria nchini, yule anayeshi kwa na vifaa bandia ni kwamba anapata stahili kulingana na sheria. Wakati mwingine wanatozwa faini na pengine inaweza hata zaidi ya hiyo akapewa adhabu stahiki.
Mheshimiwa Spika, lakini la pili amesema kwamba hivi vifaa bandia sio kwamba vinatoka nje ya nchi tu, kuna vingine vinatengenezwa humu ndani. Kwa mfano, kama vipodozi wapo watu wanachanganya vipodozi na wamewaathiri sana wale ambao wanatumia.
Mheshimiwa Spika, hatua zinazochukuliwa ni pamoja na kufunga viwanda vile ambavyo havijasajiliwa na mara nyingi hivi vitu ambavyo vinafanywa ambavyo havipo katika viwango vinafanywa na viwanda bubu. Kwa hiyo, Serikali inafanya ukaguzi, kama tulivyojibu katika swali la msingi ili kuhakikisha kwamba hawa wote wanaofanya hivyo wanakamatwa na wanapewa adhabu stahiki kwa mujibu wa sheria na viwanda vinavyojihusisha na hivyo tayari vinafungwa ili kuhakikisha kwamba suala hilo haliendelei. Vilevile pia nimeongea na Mheshimiwa Waziri akasema kwamba wanatarajia kuleta sheria itakayotoa adhabu kali zaidi hasa kwa hawa watu ambao wanatengeneza vitu bandia.

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- Kuna ongezeko la bidhaa bandia na zisizo na viwango zinazoingizwa nchini, miongoni mwa bidhaa hizo ni pembejeo za kilimo, madawa ya mifugo, dawa za binadamu, vyakula, vinjwaji, vifaa vya nyumbani na kadhalika. (a) Je, ni hasara gani imepatikana kwa mwaka mmoja uliopita kutokana na bidhaa hizo kuingizwa nchini na kutumiwa na wananchi? (b) Je, ni hatua gani zinachukuliwa kukomesha bidhaa hizo kuingia nchini hasa maeneo ya vijijini ambako uelewa wa watumiaji ni mdogo na maafisa wadhibiti ni wachache?

Supplementary Question 2

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa vifaa vya bandia kwenye maduka sasa hivi siyo siri tena, hata ukienda wanakwambia kuna hiki hapa ambacho ni dhaifu, kuna hiki hapa na bei pia ni tofauti. Kwa hiyo si kwa njia ya vichochoroni hata madukani vipo na vinauzwa halali kabisa.
Je, Serikali haioni, kuruhusu kuwepo kwa bei aina mbili/tatu kwenye kifaa kimoja dukani ni kuruhusu kuwepo kwa vifaa bandia kihalali kitu ambacho tunapiga marufuku katika nchi yetu?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI (K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI):
Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri ni kweli, unakwenda dukani unakutana na hiyo hoja. Na hoja yenyewe inakuwa kwenye kukata mapato kwenye TRA, na ndio maana juzi juzi hapa, kama umeongea na wafanyabiashara TRA imeendelea kuweka sheria ngumu ikiwepo pamoja na kila duka hata kama ni dogo lazima liwe na ile mashine ya EFD kwa ajili ya kupata zile recept ili waweze kulipa kodi.
Mheshimiwa Spika, lakini Wizara ya Fedha inaendelea kuweka sheria kali na ukaguzi mkubwa sana katika bidhaa. Suala moja ambalo ni zuri kwa sisi Waheshimiwa Wabunge ndugu zangu tuendelee kuwaelimisha wananchi wetu. Sasa kama wewe unapewa hiyo kauli, kwamba ukitaka bidhaa hii itakuwa na shilingi kadhaa lakini hii itakuwa na bei chini zaidi, wewe mwenyewe lazima ujiulize kwamba kwa nini hii ni chini?
Mheshimiwa Spika, kama ningelikuwa ni mimi ningeweza nikasema basi naomba uniuzie hiyo hiyo ya bei ambayo ni kubwa lakini unipe receipt. Kwa sababu hiyo moja kwa moja ameshakwambia hii haina ubora, sasa wewe kwa nini uende ukanunue.
Mheshimiwa Spika, lakini nakiri pia kwamba, si wananchi wote wa Tanzania hasa vijijini wenye elimu ambayo naweza nikawa nayo mimi au unaweza ukawa nayo Mheshimiwa Sakaya. Sasa ni suala letu sisi Waheshimiwa Wabunge na Madiwani na Serikali kwa pamoja tuendelee kuwaelimisha wananchi ili waweze kukwepa haya na ndiyo maana Serikali sasa inaweka viwanda vya ndani.
Mheshimiwa Spika, pamoja na hiyo kama alivyozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba hata viwanda vya ndani nao wanaweza wakafanya vitu vya namna hiyo. Ndugu zangu tunayo kazi kwa hiyo tuendelee kuelimisha jamii na kutunga sheria zilizo kali na tuzisimamie ili haya yaweze kuondoka.