Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leonidas Tutubert Gama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 1

MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi wa Songea kwanza naomba nichukue nafasi hii nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri na Wizara kwa ujumla pamoja na Serikali kwa kuanza ukarabati katika vituo 89, hivyo, katika vituo 187 tunabakiwa na vituo 98 vya maji ya mtiririko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maeneo mengi ambayo yana matatizo ya maji, maeneo hayo ni pamoja na Mlete, Lilambo, Chandarua, Mahilo, Ndilima Litembo, Lizaboni, Tanga na Mletele, Subira na Mwenge Mshindo na Making’inda. Nataka nipate uhakika wa Serikali. Je, Serikali inaweza kuwahakikishia wananchi wa Songea ni lini tatizo la maji litakuwa limekwisha kabisa katika Mji wa Songea?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili naomba nimuulize Waziri liko tatizo kubwa sana la mamlaka za maji hasa SOWASA, kuwabambikizia wananchi bili za maji za uwongo. Mtu anaweza asitumie maji mwezi mzima lakini akakuta anabambikiziwa bili isiyo na sababu. Je, ni lini Serikali itahakikisha inasimamia kidete kuhakikisha bili zinazokwenda kwa wananchi ni zile zinazotokana na matumizi ya maji? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Gama kwa jinsi ambavyo anawahangaikia wananchi wake. Wakati tuko Dar es Salaam amekuja zaidi ya mara saba ofisini na ndiye aliyefanya tukafanikisha ukarabati wa hivi visima vifupi 89, nampongeza sana. Hata hivyo, hata wakati anaondoka kwenda kutibiwa aliniachia maagizo kwa ajili ya kushughulikia Mji wake wa Songea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumemaliza awamu ya kwanza ya maendeleo ya sekta ya maji sasa tumeingia awamu ya pili. Tutahakikisha kwamba maeneo yote aliyoyataja vijiji vinavyozunguka Mji wa Songea katika awamu ya pili na katika hii miaka miwili inayofuata ya bajeti tutahakikisha kwamba maeneo yote tumeyapatia maji. Hilo ndiyo lengo la Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwamba tutakapofika mwaka 2020 basi tuwe tumefikia asilimia kubwa ya wananchi wa vijiji kuwapatia maji safi na salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la bili, nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge na nilizungumze kwa niaba ya Wabunge wote sasa. Ni kweli Mamlaka zetu za Maji Mijini kuna hiyo hali ya kwamba unaletewa bili hata kama maji yalikuwa hayatoki hata Mheshimiwa Rais juzi ameizungumzia hii, lakini hili tumeshaliona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mambo mawili ambayo tumeyagundua; moja kuna kitu wanaita service charge inakuwa kwamba wewe umekodi ile mita, kwa hiyo kwa maana ya kuikodi walikuwa wameweka utaratibu kwamba hata kama maji hayajatoka kwa sababu umekodi wanakuchaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji juzi baada ya bajeti Wakurugenzi wote walikuwa hapa amewaagiza wakaiangalie hii kwa maana ya kuitoa. Kwa sababu siwezi nikakodi kifaa sipati huduma lakini naendelea kukilipia kwa kuwa nyumbani kwangu. Kwa hiyo, suala hili Mheshimiwa Mbunge ni kwamba tayari tumeanza kulifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini liko tatizo la pili ambalo nimelifanyia study kupitia Mamlaka ya Maji DAWASCO. Hawa wahudumu wetu system yetu ya kusoma mita unasoma halafu unakwenda kupachi kwenye computer. Unaweza ukakuta unit 15 ukapanchi ukaona 15 baadaye ukarudia tena ile inaji-double ndio maana bili zinakuwa kubwa. Kwa hiyo, hilo nalo tunaliangalia kitaalam ili hiyo double isitokeze, kwa hiyo Waheshimiwa Wabunge niwahakikishieni kwamba hili suala tumeshaliona, tunalishughulikia na tutalimaliza.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, mradi wa maji wa visima Gairo umekamilika lakini kwa bahati mbaya maji haya ni ya chumvi kiasi wananchi wanapata shida kuyatumia. Je, mradi wa maji ambayo hayana chumvi kutoka milima ya Nongwe utakamilika lini? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulichimba visima saba pale Gairo vina maji mengi lakini yale maji hayafai kwa matumizi ya binadamu. Ndani ya ule mkataba tulikuwa tumepanga kununua mashine kwa ajili ya kitu wanaita desalination tumeiondoa hiyo badala yake tumeenda kutafuta sasa visima kwenye milima iliyoko na Gairo na ripoti yake inakamilika leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuwasiliane na Mheshimiwa Mbunge wiki ijayo tutapata majibu tunataka sasa tuchukue maji kutoka kule milimani ambayo hayana chemicals tuyalete pale Gairo ili wananchi wapate maji yaliyo safi na salama, tutatumia miundombinu ile ambayo imeshajengwa iko pale Gairo.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza linalohusiana na masuala ya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la maji lililopo Songea linafanana kabisa na tatizo lililopo Wilayani Masasi hasa katika Vijiji vya Lukuledi, Chikunja, Maparagwe, Liputu, Mlingura pamoja na Namajani. Maeneo haya yote yanahudumiwa na mradi wa maji wa MANAWASA kutokea mradi wa Mbwinji ambao unapeleka maji mpaka Nachingwea. Tunataka kufahamu sasa kwa sababu tatizo kubwa ni miundombinu ya kusambaza maji haya kwa watumiaji. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka pesa kwa ajili ya kununua vitendanifu kwa ajili ya kuunganisha maji katika maeneo niliyoyataja? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wiki mbili zilizopita nilienda Masasi mpaka mradi wa Mbwinji, Mamlaka ya Maji MANAWASA Mkurugenzi wake ameomba milioni 500 na tunampatia ili akamilishe kuunganisha vijiji vilivyobaki ambavyo viko pembezoni mwa bomba linalotoa maji Mbwinji kupeleka Masasi Mjini, lakini pia kwenda Nachingwea pamoja na vijiji kadhaa vya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, kwa hiyo kote tunapeleka maji.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 4

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la maji la Songea linashabihiana na kwa kiasi kikubwa na tatizo la maji katika Wilaya ya Mkinga. Hivi karibuni tumewasilisha taarifa ya Maafa kwa kuharibika mabwawa takribani saba katika Wilaya ya Mkinga na kwamba watu wanashida kubwa ya maji. Je, ni nini kauli ya Serikali kwa tatizo hili? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uharibifu mkubwa ulioharibu miundombinu ya maji Mkoa wa Tanga kutokana na mvua, Mheshimiwa Mbunge nimuahidi kwamba, ni kweli taarifa niliipokea ambayo imeandikwa kwenda upande wa maafa na mimi ninayo, lakini kabla hatujachukua hatua, basi baada ya Bunge tu naomba mimi na yeye mguu kwa mguu, twende nikajionee kule na nitakuwa na wataalam ili tuweze kuona sasa tutafanya nini. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 5

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mji wa Mkuranga ni miongoni mwa miji inayokua kwa kasi sana; na kwa kuwa visima vya maji vilivyoko katika Mlima Kurungu vilishachimbwa na maji yanamwagika kuelekea mashambani; na kwa kuwa tumeshaomba shilingi milioni 800 Serikalini ya kuhakikisha tunayatoa maji yale ya Mto Kurungu kuyaleta Mkuranga Mjini na Vijiji vya jirani vya Kiguza, Dundani, Kiparang’anda, Magoza, Tengelea na kwingineko. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kunihakikisha kwamba milioni 800 zile tutazipata kwa ajili ya kuwahudumia watu wa Mkuranga na vijiji hivyo vingine nilivyovitaja?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Ulega, ni kweli ameniletea andiko kuhusiana na maji ya Mlima Kurungu. Maji ni mengi, yanamwagika, yanapotea na sasa hivi Wizara yangu tayari nimeshawakabidhi wataalam lile andiko wanalifanyia kazi. Nimhakikishie kwamba milioni 800 itatolewa na Wizara ya Maji na Umwagiliaji pamoja na wataalam washirikiane na Halmashauri ili yale maji yasipotee wananchi wayatumie. (Makofi)

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 6

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa mazingira ya Mitaa ya Matogolo, Ndilimalitembo, Lizaboni na Bombambili kwa upande wa Songea Mjini, yanafanana kabisa na matatizo ya Mitaa ya Luwiko, Lusaka, Bethlehemu, Misheni, Mbinga A, Mbinga B, na Lusonga kwa upande wa Mbinga Mjini ni lini Serikali italeta neema ile ile inayotaka kuipeleka Songea Mjini kwa upande wa Mbinga Mjini?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, neema inakuja tunamsubiri Mheshimiwa Waziri wa Fedha, akamilishe finance agreement ya milioni 500 kutoka India ambayo sehemu ya fedha hiyo pia na Jimbo la Mheshimiwa Mbunge litafaidika na huo msaada. Tayari sasa hivi tupo katika hatua ya kuwapata Consultants ambao watafanya study kwa muda mfupi sana tutangaze tenda. Mheshimiwa Mbunge nimhakikishie kwamba Jimbo lake na Mji wake wa Mbinga utapata maji safi na salama baada ya muda mfupi. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 7

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa swali la nyongeza. Halmashauri ya Mji wa Liwale ulikuwa na miradi ya maji wa vijiji 10, lakini mpaka sasa hivi vijiji vyote 10 vimeshatobolewa lakini vijiji vilivyofungwa miundombinu ya maji ni vijiji vitatu tu. Vijiji ambavyo sasa hivi vina maji ni Kijiji cha Mpigamiti, Barikiwa, pamoja na Namiu. Je, vile vijiji saba vilivyobaki lini watatoa pesa kwa ajili ya kujenga miundombinu kumalizia vile visima ambavyo tayari vimeshatobolewa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwamba chanzo cha maji cha Mji wa Liwale kinatokana na Mto Liwale na ni kweli kwamba chanzo kile kidogo kimeleta shida. Katika bajeti ya fedha ya mwaka unaokuja tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya study ili tuweze kuimarisha chanzo au kutafuta chanzo kingine kuhakikisha vijiji vilivyobaki sasa vinapata maji bila wasiwasi wowote na hii itatekelezwa kwenye mwaka wa fedha unaokuja ambapo bajeti yake Mheshimiwa na yeye mwenyewe nafikiri aliikubali siyo kwamba aliikataa.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Mji wa Songea ni kati ya Miji yenye matatizo makubwa ya maji katika nchi yetu na katika utoaji wa maji, Halmashauri ya Mji wa Songea inategemea visima virefu na vifupi na maji ya mtiririko. Mji huo una jumla ya vituo 187 ambavyo havitoi maji ambapo kila kituo kinagharimu wastani wa shilingi milioni tatu (3) kwa ajili ya ukarabati, gharama zote ni jumla ya shilingi milioni 561. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kumaliza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni kuwa ikondoa tatizo hilo itakuwa imemaliza kero kubwa kwa wananchi zaidi ya 30,000 ambapo kila kituo kitakuwa kinahudumia watu 250?

Supplementary Question 8

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Jimbo la Babati Mjini pamoja na kwamba ni Halmashauri ya Mji kuna baadhi ya maeneo bado hayana maji. Tulipeleka maombi katika ofisi ya Mheshimiwa Waziri kwa ajili ya kuchimbiwa visima katika Mtaa wa Wa’wambwa, Kijiji cha Singu na cha Hala, maombi hayo yameishafika kwa Wakala wa Uchimbaji Visima. Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya maombi yetu haya?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa wakala wetu wa kuchimba visima unapeleka maombi kwao moja kwa moja hatuwaingilii, wanakujibu, mkiingia mikataba sisi kazi yetu ni kuchukua sehemu ya hela yako uliyotengewa na Wizara ya Maji na Umwagiliaji, wakishachimba tunawalipa ili shughuli ziendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uzuri wa taasisi yetu hii, ina- survey yenyewe, inachimba yenyewe, haikupata maji haidai ndiyo uzuri wake. Nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge kwamba tujaribu kutumia taasisi yetu na sisi tunaendelea kuiimarisha kwa kuiongezea mitambo ili iweze kutusaidia katika hili suala la matatizo ya maji vijijini. (Makofi)