Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHOZA aliuliza:- Mkoa wa Songwe ni mpya na unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Vyuo Vikuu hata vile vya Ufundi. Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kujenga hata kampasi ya Chuo Kikuu kimojawapo pamoja na vile Vyuo vya Ufundi?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Kampasi ya DIT iliyoko Myunga anayoizungumzia Mheshimiwa Naibu Waziri yalikuwa ni majengo ya TANROADS ambayo kwa sasa ni takribani mwaka mmoja umepita tangu Serikali ipeleke Walimu wanne, lakini hakuna maandalizi mengine yoyote yanayoendelea pale kuonyesha kwamba hicho chuo kitafunguliwa hivi karibuni. Kwenye jibu la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba hicho chuo kitafunguliwa hivi karibuni.
Mheshimiwa Naibu Waziri anatuhakikishia vipi wananchi wa Wilaya ya Momba pamoja na Mkoa wa Songwe kwa ujumla kwamba hicho chuo kitakuwa bora kwa sababu mpaka sasa maandalizi yake ya ufunguzi ni hafifu sana?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika Wilaya ya Ileje kuna chuo cha VETA ambacho kimejengwa kwa jitihada kubwa za Halmashauri pamoja na JICA, mpaka sasa chuo hicho hakijafunguliwa kwa sababu ya ukosefu wa vifaa. Je, Serikali sasa haioni kwamba kuna umuhimu wa kukiongezea nguvu chuo hicho ili kiweze kufunguliwa na hatimaye kiweze kutumika kama chuo cha VETA kwa Mkoa wa Songwe ukizingatia kwamba mpaka sasa Mkoa wa Songwe hakuna chuo cha VETA? Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Chuo cha Myunga, kwanza nichukue nafasi hii kuwashukuru sana wenzetu TANRODS kwa kukubali kambi hiyo itumike kwa ajili ya kutoa mafunzo kupitia Chuo cha DIT. Kimsingi ni kweli kwamba ile kambi haikuandaliwa kama Chuo cha Ufundi, kwa hali hiyo ilibidi kuanza kufanya taratibu zinazostahili ikiwa ni pamoja na kuangalia ni course zipi zinaweza zikafanyika kwa kuanzia katika eneo lile. Vvilevile kupata mahitaji muhimu kama umeme, pamoja na miundombinu ambayo itakuwa sahihi katika ufundishaji na ujifunzaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shughuli hiyo imekamilika lakini tumekwama hasa katika suala la umeme na tumeona tutaanza na umeme wa Solar mna generator lakini baadaye tunategemea kupitia umeme vijiji mahali hapa patakuwa pameshapata umeme na kuweza sasa kutoa mafunzo makubwa zaidi kwa mujibu wa fursa zinazotolewa katika kampasi za vyuo vyenye uwezo wa kutoa mafunzo kuanzia ya ufundi wa sanifu mpaka degree.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika swali la pili kuhusiana na Chuo cha Ileje. Suala hili limekuwa pia likifuatiliwa na Mheshimiwa Janeth Mbene na tulikuwa tumetoa maelekezo baada ya Mkuu wa Wilaya kuja ofisini kwetu. Tulilokuwa tunaliomba kwao ni wao kuongeza eneo lile ukubwa kidogo lakini wakati huo kutupa sisi hati baada ya kupitia mikutano yao ya Halmashauri za Wilaya na RCC ili sasa kuhamisha ile ardhi kuwa katika mikono ya VETA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo sisi tutaendelea na hayo tumeshayafanya maeneo mengi ikiwemo Busekelo. Kwa hiyo, ninachoomba tu kwamba wao wenyewe wajitahidi katika kuongeza jitihada katika hilo. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHOZA aliuliza:- Mkoa wa Songwe ni mpya na unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Vyuo Vikuu hata vile vya Ufundi. Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kujenga hata kampasi ya Chuo Kikuu kimojawapo pamoja na vile Vyuo vya Ufundi?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa, swali lilivyoulizwa na majibu ni kwamba Chuo hicho ambacho kinataka kuanzishwa kipo katika Jimbo la Momba ambalo mimi naongoza. Sasa nataka tu nimuulize pamoja na ahadi hii ambayo imetolewa na tunaamini kwamba kitaanza hivi karibuni na nina uhakika ni mwaka huu wa fedha. Je, endapo hicho anachokizungumza kisipotekelezwa ni hatua gani tumchukulie yeye kama Waziri kuwadanganya wananchi wa Momba? (Makofi/Kicheko)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi ninavyojibu lengo langu sio kusherehesha, ni lengo la kueleza Serikali ni mikakati gani inachukua. Kwa hiyo huu ni mkakati ambao hatujalazimishwa bali tunaona ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma inayostahili. Ndiyo maana tunataka kuanza na mafunzo hayo ya kawaida wakati mikakati mingine inaendelea. (Makofi)

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHOZA aliuliza:- Mkoa wa Songwe ni mpya na unakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Vyuo Vikuu hata vile vya Ufundi. Je, ni lini Serikali itakuja na mpango wa kujenga hata kampasi ya Chuo Kikuu kimojawapo pamoja na vile Vyuo vya Ufundi?

Supplementary Question 3

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja la nyongeza kuhusiana na VETA ya Ileje. VETA ya Ileje mimi ndiyo nilienda kuomba fedha kwa wafadhili zikapelekwa pale na VETA imejengwa kwa kiasi kikubwa. Hata hivyo, hayo masharti kuwa lazima tuwe na hati ndiyo yametukwamisha mpaka sasa hivi. Kupima na kupata hati pia ni suala la Serikali vilevile. Sasa kwa nini hicho Chuo kisianze wakati suala la upimaji linaendelea? Kwa sababu ni miaka miwili sasa Chuo kimesimama na kile Chuo kingekuwa tayari kinasaidia vijana wetu wengi sana wakati suala la hati likiendelea maana nalo ni sehemu ya Serikali vilevile.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sioni kama kuna ugumu kama watu wameamua, kwa sababu kimsingi utoaji wa hati au hatua za kuweza kuchukua eneo na kupeleka eneo lingine linaanzia huko kwenye Halmashauri. Hata hivyo, toka kipindi hicho tulichoongea mpaka leo sijaona kama kuna jitihada yoyote iliyofanyika, kwa sababu maeneo mengine wameshafanya hivyo na wakafanikiwa na wao hawajafanya chochote kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani tukikubaliana si lazima ipatikane hati kabisa, lakini basi hata yale makubaliano ya kwamba Chuo hiki sasa wanakikabidhi kwa VETA basi itakuwa ni jambo jema lakini hatuwezi kwenda tu kuvamia mali ambayo sio mali ya VETA. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru kwa swali na kwa niaba ya Waziri wa Elimu naomba nijibu swali la nyongeza kama ambavyo limeulizwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokupatikana kwa hati inaweza kuwa ni kigezo kweli cha wafadhili kushindwa kuwasaidia. Hata hivyo, ningeomba pengine baadaye tuonane na Mheshimiwa Mbene tujue wamekwama wapi, kwa sababu kama ni suala la taasisi ambayo ni ya Kiserikali na imepitia katika process zote sasa kuna mahali watakuwa wamekwama wao wenyewe katika kufuatilia hati ama kwenye malipo au kitu kingine. Kwa hiyo, nitawasiliana nae ili nijue wamekwama wapi na tuone tunawasaidiaje ili waweze kupata huo ufadhili.