Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Wilaya ya Malinyi haina kabisa huduma za Kibenki ambapo wananchi hufuata huduma hizi katika Wilaya jirani ya Kilombero au Ulanga. Serikali kupitia taasisi za kibenki zikiwemo CRDB na NMB zimeahidi kuanza kutoa huduma toka mwaka 2015, lakini hadi leo hakuna utekelezaji wowote:- • Je, ni lini huduma hizi zitaanzishwa rasmi katika Wilaya ya Malinyi? • Wakati benki zikisubiri ujenzi wa Matawi yao; Je, kwa nini wasianze kutoa huduma hizo kwa kutumia matawi yanayohamishika (Mobile Service)?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Jibu la Serikali limeeleza kwamba kwa muda huu Wilaya ya Malinyi inapata huduma za Kibenki kupitia mawakala wa fahari ambayo ni Malinyi SACCOS na Zidua Shop. Huduma hizi hazitoshelezi kabisa, kwa sababu mawakala hawa wawili wana changamoto kubwa ya mtaji. Je, Serikali kupitia hiyo benki CRDB wanawawezeshaje kwa mikopo isiyokuwa na masharti magumu kuongeza mitaji kwa mawakala hawa wawili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani yupo na maeneo haya ya Malinyi ndio wazalishaji wakubwa wa Mpunga wa Brand inayojulikana ya Kilombero au Ifakara. Wananchi hawa kwa kukosa huduma za kibenki wanalazimika kwenda Mahenge au Ifakara kupata huduma hizi za kuweka na kutoa fedha. Sasa matokeo yake kutembea na fedha nyingi wanahatarisha maisha yao na usalama wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na matukio kwa muda wa miaka mitatu iliyopita zaidi ya matukio kama kumi hivi, ni kwamba kati ya Lupilo, Ilagua na Itete kuna matukio ya ujambazi yanayotokea mara kwa mara wananchi wanapora fedha na kuhatarisha maisha yao. Je, Wizara ya Mambo ya Ndani wanawasaidiaje Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro hususani Wilaya ya Malinyi kukabiliana na ujambazi huo? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mponda kwa swali lake zuri na anaonekana analielewa vizuri Jimbo lake na ndio maana wananchi wameendelea kumchagua. Niseme tu Wizara ya Mambo ya Ndani kwanza tumejipanga kuwasaidia usafiri watu walioko maeneo yale ambayo yanahitaji doria zinazohitaji kuzunguka mwendo mrefu kama ilivyo kwenye Jimbo lake na Majimbo mengine ya aina hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakapokuwa tumeimarisha usalama, tutakuwa tumeweka ushawishi pia kwa taasisi za kifedha kuweza kuweka benki zao huku wakijua kwamba kutakuwepo na usalama wa kuweka benki hizo na fedha zao zitakuwa salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wilaya hiyo pamoja na Majimbo hayo ni wazalishaji wakubwa, sina mashaka kuhusu upatikanaji wa wateja ambao unaweza ukavutia benki hizo kuweza kuweka matawi yao kwa namna hiyo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutalifanya hilo na mimi binafsi nitatembelea huko ili kuweza kutekeleza haya tunayoyasema. (Makofi)

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Wilaya ya Malinyi haina kabisa huduma za Kibenki ambapo wananchi hufuata huduma hizi katika Wilaya jirani ya Kilombero au Ulanga. Serikali kupitia taasisi za kibenki zikiwemo CRDB na NMB zimeahidi kuanza kutoa huduma toka mwaka 2015, lakini hadi leo hakuna utekelezaji wowote:- • Je, ni lini huduma hizi zitaanzishwa rasmi katika Wilaya ya Malinyi? • Wakati benki zikisubiri ujenzi wa Matawi yao; Je, kwa nini wasianze kutoa huduma hizo kwa kutumia matawi yanayohamishika (Mobile Service)?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mfumo wa ulipaji wa fedha sasa hivi kwa wakulima wa korosho, kuanzia mwaka jana unatumika katika kulipa kwenye akaunti zao. Wakulima wameamrishwa wafungue akaunti benki ili waweze kulipwa kupitia benki. Sambamba na hilo alilouliza Mheshimiwa Mponda, Serikali haioni kwamba sasa kuna umuhimu wa hizi benki wakati wa kulipa wakulima wa korosho, wakawa wanakwenda kufanya huduma kule vijijini kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, badala ya wananchi kuwa wanasafiri kwenda umbali mrefu. Kwa mfano pale Mchinga kwenda Lindi kwenda kuchukua fedha, wakati unajulikana kabisa leo fulani anaenda kuchukua pesa kutoka benki. Hilo ndiyo swali langu.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Bobali ametoa ushauri na sisi kama Serikali tunauchukua kuona unatekelezwa vipi ili kuhakikisha kwamba wananchi wetu wako salama, wanapokwenda kuchukua na kupokea fedha zao kutoka kwenye malipo hayo. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Wilaya ya Malinyi haina kabisa huduma za Kibenki ambapo wananchi hufuata huduma hizi katika Wilaya jirani ya Kilombero au Ulanga. Serikali kupitia taasisi za kibenki zikiwemo CRDB na NMB zimeahidi kuanza kutoa huduma toka mwaka 2015, lakini hadi leo hakuna utekelezaji wowote:- • Je, ni lini huduma hizi zitaanzishwa rasmi katika Wilaya ya Malinyi? • Wakati benki zikisubiri ujenzi wa Matawi yao; Je, kwa nini wasianze kutoa huduma hizo kwa kutumia matawi yanayohamishika (Mobile Service)?

Supplementary Question 3

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Mazingira ya swali hili yanafanana kabisa na hali halisi iliyopo katika Jimbo la Vwawa hasa katika Wilaya ya Mbozi. Kwa kuwa, Wilaya ya Mbozi inajishughulisha sana na kilimo na niwazalishaji wakubwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Tawi la Benki ya Kilimo ili liweze kutoa mikopo kwa wakulima hawa wa Wilaya ya Mbozi?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo tumekuwa tukisema hapa, Benki ya Kilimo sasa inaelekea kufungua Ofisi za Kanda na ofisi mojawapo ya Kanda itakayofunguliwa katika Mkoa wa Mbeya, ambapo najua ni karibu kabisa na Wilaya ya Mbozi. Ni imani yangu wananchi wetu na wakulima wetu wa Wilaya ya Mbozi watapata faida za kupata mikopo nafuu kutoka katika benki hii.