Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Hamad Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ole

Primary Question

MHE. JUMA HAMAD OMAR aliuliza:- Kuna wakati mwananchi anapaswa kulipa kodi zaidi ya thamani ya bidhaa au kifaa alichonacho:- (a) Je, Serikali haioni kwamba yanapotokea hayo yanashawishi mlipa kodi husika kulipa kwa njia ya panya au kukwepa kodi? (b) Je, ni kiasi gani cha misamaha ya kodi kimekuwa kikitolewa na Serikali kwa kipindi cha miaka kumi nyuma na ni nini athari zake katika uchumi?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa ufafanuzi wa swali langu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba Serikali inapoteza kiasi cha shilingi za Kitanzania trilioni 1.18 kila mwaka. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Idara ya Afrika ya IMF kuhusu effect ya hizi exemptions kwa uchumi wa nchi ambazo ziko Kusini mwa Jangwa la Sahara, imebainika katika ripoti hii kwamba Tanzania ikiwa ni moja ya nchi hizo inapoteza kiasi cha Dola bilioni 1.2 hadi Dola bilioni 2.2 kwa wastani kwa mwaka ambapo hiyo ni sawasawa na kiasi cha shilingi za Tanzania trilioni 2.2 mpaka kwenda kwenye shilingi trilioni 4.6. Nataka kujua ni takwimu zipi sahihi za Waziri au za utafiti huu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ripoti hii ya uchunguzi imebainisha kwamba kivutio cha misamaha ya kodi sio tena kivutio kikubwa kwa maana ya kuwa-attract wawekezaji kuingia katika nchi. Yako mambo matatu ambayo sasa hivi wawekezaji wanaangalia sana yakiwa ni kipaumbele. Kwanza, ubora wa miundombinu. Pili, sera sahihi za fedha zinazotabirika (predictable financial and monetary policies). Tatu, utawala bora na utulivu wa kisiasa (good governance and political stability). (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, kwa sababu tax incentive siyo tena kipaumbele au vigezo wanavyoviangalia wawekezaji, haoni kwamba time imefika sasa ya kubadilisha ile Sheria ya Uwekezaji hasa Kifungu cha 38 na kubadilisha sheria zinazoanzisha Maeneo Tengefu (Economic Processing Zone, Sspecial Economic Zone and Export Processing Zones) ili misamaha hiyo itolewe kidogo sana kuliko ilivyo sasa ambapo inachukua karibu asilimia 8.3 ya bajeti yote ya Serikali? (Makofi)

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza, naomba nisema takwimu nilizozisema mimi ni halali kabisa kwa sababu zimetoka katika takwimu za Serikali na naomba aziamini. Hatuna sababu ya kudanganya takwimu hizo kwa sababu tunajua madhara ya mishamaha hii ya kodi kwa uchumi wa Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, nakiri kwamba ni sahihi kivutio cha kodi sio kivutio tena lakini nimwambie tu Tanzania yetu ni nchi ya mfano katika Bara letu la Afrika na dunia kwa ujumla kwa sera zake za monitory pamoja na fiscal policies ndiyo maana wawekezaji wanaongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nilikumbushe Bunge lako, ni juzi tu wakati tunapitisha bajeti ya Wizara ya Viwanda pamoja na bajeti ya Wizara ya Fedha, Waheshimiwa Wabunge hawa hawa walikuwa wakilalamika kwamba zipo tax incentive ambazo tunashindwa kuzitoa na wawekezaji wanashindwa kuja nchini kwetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii napata shaka kidogo na swali hili la Mheshimiwa Omar, lakini kama Serikali tunajua na tunafahamu misamaha hii ya kodi tunaitoa kisheria na tunaangalia mazingira ya kiuchumi ya Taifa letu, nani anakuja na kufanya nini katika uchumi wetu, lakini pia kijamii ana impact gani mtu huyu tunayempa msamaha huu na sheria zetu pia tunaziangalia kwa uhakika kabisa.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. JUMA HAMAD OMAR aliuliza:- Kuna wakati mwananchi anapaswa kulipa kodi zaidi ya thamani ya bidhaa au kifaa alichonacho:- (a) Je, Serikali haioni kwamba yanapotokea hayo yanashawishi mlipa kodi husika kulipa kwa njia ya panya au kukwepa kodi? (b) Je, ni kiasi gani cha misamaha ya kodi kimekuwa kikitolewa na Serikali kwa kipindi cha miaka kumi nyuma na ni nini athari zake katika uchumi?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Nina swali dogo tu la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri. Ulipaji wa kodi unategemea uwepo wa ofisi za TRA katika maeneo mbalimbali. Nimekuwa nikiuliza zaidi ya mara mbili, sisi Halmashauri ya Mji wa Kasulu tumeshatoa kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za TRA na tumewapa bure. Swali langu, kwa sababu bajeti imepita kwa kishindo, ni lini ofisi ya TRA itajengwa katika Mji wa Kasulu ili kuhudumia Wilaya nne zilizopo katika Mkoa wa Kigoma za Kakonko, Kibondo, Buhigwe na Uvinza? Nashukuru.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza yeye pamoja na Halmashauri yake kwa kutoa kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za TRA katika Wilaya ya Kasulu, hongereni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, niseme Mheshimiwa Waziri wa Fedha alitoa commitment kwamba ofisi hizi zitajengwa na nirudie kusema na niagize ofisi yetu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania wahakikishe ndani ya mwaka huu wa fedha 2017/2018, ofisi hizi zinajengwa katika Wilaya ya Kasulu ili kusogeza karibu huduma hizi kwa wananchi wetu.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA HAMAD OMAR aliuliza:- Kuna wakati mwananchi anapaswa kulipa kodi zaidi ya thamani ya bidhaa au kifaa alichonacho:- (a) Je, Serikali haioni kwamba yanapotokea hayo yanashawishi mlipa kodi husika kulipa kwa njia ya panya au kukwepa kodi? (b) Je, ni kiasi gani cha misamaha ya kodi kimekuwa kikitolewa na Serikali kwa kipindi cha miaka kumi nyuma na ni nini athari zake katika uchumi?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo tu la nyongeza japokuwa kidogo linafanana na muuliza swali aliyepita. Ili kurahisisha ukusanyaji na ulipaji kodi ni kwa nini TRA isiweke vituo katika kila Halmashauri ya Wilaya ili kupunguza usumbufu mkubwa wanaopata walipa kodi? Kwa mfano, ukichukulia Mkoa wetu wa Iringa, jiografia yake ni mbaya sana inawasabisha hata watu wengine kukwepa kodi kwa sababu tu vituo vya TRA viko mbali sana. (Makofi)

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni sahihi na hakuna Taifa lolote linaweza kuendelea bila kukusanya mapato, tunafahamu kabisa hilo kama Wizara yenye mamlaka ya ukusanyaji wa mapato Tanzania. Hili la kuanzisha ofisi kila Halmashauri, nilishawahi kujibu ndani ya Bunge lako Tukufu kwamba kuanzishwa kwa ofisi huwa kuna tathmini ambayo huwa inafanyika kuangalia cost and benefit analysis ya kuanzisha ofisi hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia Mheshimiwa Mbunge, tutafanya uhakiki na tathmini hiyo kujua kama kuna uhitaji mkubwa wa kuweka ofisi hizi katika kila Halmashauri ndani ya Mkoa wa Iringa.

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA HAMAD OMAR aliuliza:- Kuna wakati mwananchi anapaswa kulipa kodi zaidi ya thamani ya bidhaa au kifaa alichonacho:- (a) Je, Serikali haioni kwamba yanapotokea hayo yanashawishi mlipa kodi husika kulipa kwa njia ya panya au kukwepa kodi? (b) Je, ni kiasi gani cha misamaha ya kodi kimekuwa kikitolewa na Serikali kwa kipindi cha miaka kumi nyuma na ni nini athari zake katika uchumi?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Tanzania ndiyo nchi ambayo inaongoza kwa viwango vya juu vya kodi ukilinganisha na nchi ya Kenya, Rwanda na Uganda. Serikali ina mkakati gani wa kupunguza viwango hivi kwa sababu vinaathiri sana wafanyabiashara hasa wadogo wadogo?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi kodi za forodha ambazo zinatozwa huwa tunafuata mfumo wa kodi wa Afrika Mashariki. Kwa hiyo, si sahihi kusema Tanzania tunaongoza kwa viwango vikubwa vya kodi. Jana tu tumepitisha bajeti kuu ya Serikali, tumeona ni kwa kiwango gani tumeweza kupunguza na kuondoa kodi ambazo zimekuwa ni kero kwa wafanyabiashara wetu hasa wafanyabiashara ndogondogo.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. JUMA HAMAD OMAR aliuliza:- Kuna wakati mwananchi anapaswa kulipa kodi zaidi ya thamani ya bidhaa au kifaa alichonacho:- (a) Je, Serikali haioni kwamba yanapotokea hayo yanashawishi mlipa kodi husika kulipa kwa njia ya panya au kukwepa kodi? (b) Je, ni kiasi gani cha misamaha ya kodi kimekuwa kikitolewa na Serikali kwa kipindi cha miaka kumi nyuma na ni nini athari zake katika uchumi?

Supplementary Question 5

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. TRA ni chombo cha Muungano na katika suala linalowakera Wazanzibari kwa ujumla wake ni pale wanapotozwa kodi Zanzibar na wakiingia na mizigo yao Tanzania Bara wakatozwa tena kodi mara ya pili. Suala hili limekuwa ni kero moja kubwa sana na Serikali imekuwa ikilipiga danadana kwa kuliingiza kwenye misamiati kero za Muungano, mchakato lakini halifikii mwisho. Naomba Waziri anijibu suala hili la Wazanzibari kutozwa kodi Zanzibar na wanapoingia Bara na mizigo yao wakatozwa tena kodi ni lini litamalizika na kupatiwa ufumbuzi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimwambie Serikali haina dhamira ya kuwapiga danadana wafanyabishara wa Zanzibar. Nimekuwa nikisema hapa Serikali yetu iko committed katika kuwalea wafanyabiashara wetu hasa sekta binafsi kwa sababu tunajua sekta binafsi ni injini ya uchumi wa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utozaji wa kodi mara mbili na naomba niliweke vizuri sio kodi mara mbili ni kutozwa kodi ambayo iko tofauti kati ya mifumo miwili ambayo inatumika Tanzania Zanzibar na Tanzania Bara. Katika hili, Mamlaka ya Mapato Tanzania pamoja na ZRB wanashughulikia tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nisimwambie ni lini kwa sababu ni suala la kimfumo, kipindi watakapokubaliana kutumia mfumo mmoja, tatizo hili litaondoka. Hili linafanyika ili kulinda tu ile fair competition katika soko letu na hili linafanyika kwa nia njema kabisa.