Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Kituo cha Afya cha Mji Mwema katika Manispaa ya Songea kinahudumia watu zaidi ya laki mbili lakini kinapata mgao wa dawa sawa na vituo vingine vya afya:- (a) Je, Serikali ina mpango wa kukiongezea dawa kituo hiki ili kipate mgao wa dawa na vifaa tiba kama Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha vifaa vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Manispaa ya Songea haina Hospitali ya Wilaya lakini pia katika Manispaa ya Songea, wakazi wengi wanategemea Kituo cha Afya cha Mji Mwema na kituo hicho hakina gari la wagonjwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta gari kwa ajili ya wagonjwa ili kurahisisha kutoa huduma pamoja na kurekebisha jengo la upasuaji ili kuweza kwenda sawasawa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali ina mkakati gani wa kuweka Kituo cha Damu Salama katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali la kwanza kuhusu ambulance, kama ambavyo tumekuwa tukisema hapa Bungeni kila siku siyo jukumu la Wizara ya Afya. Kimsingi ni jukumu la Halmashauri husika kwamba katika vituo wanavyovimiliki na wanavyoviendesha, kama kuna mahitaji ya ambulance basi Halmashauri husika iweke katika vipaumbele vyake iweze kununua ambulance hizo na kuzipeleka kwenye vituo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachokifanya sisi Wizara ya Afya na naona sasa kinatuletea shida, tunaomba kwa wahisani watupe ambulance katika maeneo ya kipaumbele kama eneo la kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto, tukipata ndiyo tunatawanya kwenye Majimbo na kwenye Halmashauri kadri ambavyo tutaweza kufanya hivyo, lakini sio jukumu letu. Kwa hiyo, natoa rai kwake na kwa Halmashauri zote nchini kuweka kipaumbele cha kununua ambulace katika Halmashauri zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili linahusu damu salama. Mpaka sasa tuna upungufu wa kuwa na vituo vikubwa vya kanda vya damu salama katika mikoa saba nchini, Mikoa ya Geita pamoja na Arusha wameonesha uwezekano wa kujenga vituo vyao wenyewe. Mikoa ambayo imebaki tumeweka kwenye bajeti, mwaka jana tuliweka shilingi bilioni mbili bahati mbaya hatukufanikiwa kukamilisha, mwaka huu pia kwenye bajeti hii tumeweka tena shilingi bilioni mbili. Malengo yetu kwa kweli ni kuhakikisha mikoa hii ukiwemo Mkoa wa Ruvuma pale Songea tunajenga kituo kikubwa cha Damu Salama ili kuokoa Maisha ya Watanzania wenzetu.

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Kituo cha Afya cha Mji Mwema katika Manispaa ya Songea kinahudumia watu zaidi ya laki mbili lakini kinapata mgao wa dawa sawa na vituo vingine vya afya:- (a) Je, Serikali ina mpango wa kukiongezea dawa kituo hiki ili kipate mgao wa dawa na vifaa tiba kama Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha vifaa vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Hospitali ya Rangi Tatu, Mbagala ina upungufu mkubwa wa dawa na huwa zinachelewa kuletwa katika hospitali ile. Vilevile tunawadai MSD dawa zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 300. Je, Wizara itatusimamia dawa zile zipatikane ili tuweze kutoa huduma hasa ikizingatiwa tunatoa huduma mpaka maeneo ya Mkoa wa Pwani maeneo ya Mkuranga?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kituo hiki cha Rangi Tatu nakifahamu vizuri kwa sababu mdogo wangu pale ndiyo in charge wa kituo kile, sidhani kama Mheshimiwa Issa anajua, kwa hiyo nafahamu changamoto hiyo na kwamba kina wateja wengi sana, maana yake analalamika halali kwa kufanya kazi kwa bidii kuwahudumia Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakachokifanya, nitafanya kazi kwa ukaribu na Mheshimiwa Mangungu kufuatilia tuone kama kweli wanadai shilingi milioni 300 na kama wanadai basi waweze kupata huduma hiyo ya dawa.

Name

Raisa Abdalla Mussa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Kituo cha Afya cha Mji Mwema katika Manispaa ya Songea kinahudumia watu zaidi ya laki mbili lakini kinapata mgao wa dawa sawa na vituo vingine vya afya:- (a) Je, Serikali ina mpango wa kukiongezea dawa kituo hiki ili kipate mgao wa dawa na vifaa tiba kama Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha vifaa vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema?

Supplementary Question 3

MHE. RAISA ABDALLA MUSSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri wanayotoa Wizara ya Afya mara nyingi wanapoulizwa maswali hapa Bungeni nina swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la msingi ni kwamba kunahitajika vifaa tiba katika hospitali za Serikali. Sasa pamoja na vifaa tiba, kuna kitu muhimu ambacho kinatakiwa na Watanzania katika Hospitali hasa za Serikali nacho ni kauli nzuri ya wahudumu na wafanyakazi katika hospitali za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie Waziri na Naibu Waziri kwamba suala hili halipatikani katika katika Hospitali zetu za Serikali. Ama ukienda hospitali za binafsi jinsi wanavyofanya biashara zao wanawanyenyekea watu, lakini hospitali hizi za wanyonge hilo halipatikani. Je, Mheshimiwa Waziri anatuambia vipi kuhusu wafanyakazi ambao wanatoa kauli ambazo haziridhishi kwa Watanzania? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza natambua kazi nzuri na kubwa inayofanywa na wataalam wanaotoa huduma kwa watu wetu hapa nchini. Napenda sisi kama viongozi tutambue kazi kubwa wanayoifanya kwa kujitoa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia natambua kuwa kuna baadhi ya wafanyakazi ambao wana changamoto hizo anazozisema Mheshimiwa Raisa kwamba wana lugha mbaya, wanashindwa kuhudumia watu vizuri na customer care ni mbovu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwamba wataalam wote kwenye sekta ya afya wale wachache ambao bado hawajabadilika, huu ni wakati wa kubadilika. Kwa sababu kwa kweli tukipata taarifa za mtaalam ambaye amem-treat vibaya mteja wetu huwa tunachukua hatua bila kulaza damu. Kwa hiyo, nitoe rai wasiombe nikawakuta na tuhuma hizi kwa sababu nitawapeleka kwenye Baraza lao la Kitaalam waweze kuchukuliwa hatua za kitaaluma. Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Kituo cha Afya cha Mji Mwema katika Manispaa ya Songea kinahudumia watu zaidi ya laki mbili lakini kinapata mgao wa dawa sawa na vituo vingine vya afya:- (a) Je, Serikali ina mpango wa kukiongezea dawa kituo hiki ili kipate mgao wa dawa na vifaa tiba kama Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha vifaa vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mimi Mbunge wa Jimbo la Nyang’wale niliweza kujitolea na kujenga zahanati na kuikamilisha katika Kijiji cha Mwamakiliga na kwa kuwa niliweza kujitolea na kujenga wodi mbili na chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya ambayo ni Hospitali ya Wilaya ya Nyang’wale, nimeweza kuyafikisha majengo hayo kiwango cha asilimia 75 na nimekwama. Je, Serikali inasaidia vipi sasa kuweza kuifungua ile zahanati ya Mwamakiliga ili iweze kufanya kazi na kukamilisha majengo hayo yaliyo katika Kituo cha Afya Kalumwa ili yaweze kufanya kazi? (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Hussein Nassoro Amar kwa kujitoa kiasi hicho kwa ajili ya wananchi wa Nyangh’wale. Nimwombee dua Mungu apokee swaumu yake katika Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa sadaka hiyo kubwa aliyoitoa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimhakikishie kwamba sisi tutakuwa pamoja naye, bahati mbaya sikufika pale Kalumwa wala Mwamakiliga nilipokuja kwenye ziara ya Mkoa wa Geita, lakini baada ya Bunge hili nina ziara tena ya kuzunguka mikoani na nitapita Mkoa wa Geita na mahsusi nitafika kwako na kwa Mheshimiwa Musukuma nina ahadi yangu naikumbuka. Nitakapofika pale, nitaongea na wataalam wale tujue ni nini cha kufanya kwa kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ili kuweza kuunga mkono jitihada nzuri alizozionyesha. (Makofi)

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Kituo cha Afya cha Mji Mwema katika Manispaa ya Songea kinahudumia watu zaidi ya laki mbili lakini kinapata mgao wa dawa sawa na vituo vingine vya afya:- (a) Je, Serikali ina mpango wa kukiongezea dawa kituo hiki ili kipate mgao wa dawa na vifaa tiba kama Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini Serikali itakamilisha vifaa vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema?

Supplementary Question 5

MHE. DEVOTA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Matatizo ya afya katika Mkoa wa Songea yanafanana kabisa na matatizo ya afya katika Hospitali ya Mkoa Morogoro ambapo licha ya kazi nzuri inayofanywa na Madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro lakini hospitali ile inaelemewa na wagonjwa wengi. Kwa mwezi mmoja Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro inatibu zaidi ya wagonjwa 15,000. Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kupeleka vifaa muhimu kama MRI, CT- Scan na X-ray machines za kisasa ili kuwapunguzia mzigo wagonjwa ambao wanalazimika hivi sasa kwenda Muhimbili kwa matibabu?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mheshimiwa Mohamed Abood kwa kazi nzuri anayoifanya kwenye hospitali ile lakini pia kwa kutumia pesa zake za mfukoni kuweza kununua baadhi ya vifaa tiba ambavyo vinatumika katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kumwaga sifa hizo kwa Mheshimiwa Abood, naomba nijibu sasa swali la Mheshimiwa Devota Minja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango mkubwa kupitia mradi wake wa ORIO wa kupeleka vifaa tiba kwenye Hospitali za Mikoa nchini, Hospitali za Wilaya na baadhi ya vituo vingine maalum vya kutolea huduma za afya nchini. Mradi huo ulisuasua mwaka jana kwa sababu tulikuwa hatujalipa counterpart funds kwa Serikali ya Netherlands ambao ndiyo wafadhili wa mradi ule. Sasa tumeshaanza kukamilisha sehemu yetu ya fedha ambazo tunapaswa kulipa ili mradi uanze kutekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina hakika baada ya miezi mitatu mradi huu utaanza kutekelezwa. Mradi huu ukitekelezwa, tutaweza kupata CT-Scan, MRI, Ultra-sound, digital X-rays na vifaa vingine vingi vya kufanyia uchunguzi wa magonjwa kwa ajili ya hospitali zetu hapa nchini. Sina hakika mgao umekaaje mahsusi na Hospitali ya Rufaa ya Morogoro, lakini naamini kwa vile ni kati ya hospitali kubwa hapa nchini inawezekana ikapata badhi ya vifaa hivi vikubwa ambavyo vinatarajiwa kuja lakini nitaangalia na akipenda nimpe taarifa nitampa baadaye.