Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tafsiri hii ni nzuri sana, lakini ni ya kitaalam zaidi. Je, sasa Serikali ina mpango gani kuwaelimisha wananchi juu ya tafsiri hii? (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nimhakikishie tu Mheshimiwa Hija kwamba toka maambukizi ya virusi vya UKIMWI yalipotokea miaka ya mwanzo ya 1980 Serikali pamoja na wadau mbalimbali tumekuwa tukishirikiana kuelimisha wananchi juu ya virusi vya UKIMWI, UKIMWI, magonjwa nyemelezi, lakini pia madhara yanayotokana na UKIMWI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi hiyo imeendelea na imefanyika kwa ufanisi mkubwa na kwa mafanikio makubwa sana. Ndiyo maana leo hii ninavyozungumza hapa, kiwango cha maambukizi ya UKIMWI kimepungua sana mpaka kufikia sasa hivi tuna kiwango kama cha asilimia 4.6 tu (prevalence rate).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huo tuna mafanikio makubwa sana kwenye eneo hili kuliko anavyofikiria. Vile vile tutaendelea kutumia mbinu ambazo tumekuwa tukitumia, lakini pia ubunifu wa taasisi mbalimbali tunazoshirikiana nazo kuweza kuzidisha uelewa wa wananchi juu ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda tu kwa ufupi nitoe elimu tu kidogo hapa kwamba virusi vya UKIMWI, yaani VVU ama HIV ama kitaalam Human Immunal Deficiency Virus, ni kirusi ambacho kipo katika familia ya retroviridae na viko virusi vingi vinavyosababisha magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na virusi hiki nacho kimo katika kundi hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kinayofanya ni kuingia kwenye chembe chembe ya mwanadamu ya aina ya white blood cell ambayo inahusika na kinga mwilini na kitakaa mle kwa miaka kati ya hiyo mitano mpaka 10 hadi 12 bila kujulikana na baada ya hapo sasa kama mtu alipima atajulikana, lakini kama hakupima, haitajulikana kwamba ana maambukizi. Kuanzia hapo zile cells za kinga zitapungua mwilini na mtu sasa ataanza kuonesha dalili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale mtu anapoanza kuonesha dalili kwamba amepungua kinga mwilini, ndiyo tunasema amepata UKIMWI. Hiyo ndiyo tofauti. Isipokuwa unaweza ukaishi na hicho kirusi kwa muda huo niliousema bila kuonesha dalili; na kwa maana hiyo, utakuwa na kirusi tu, lakini hauna UKIMWI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa UKIMWI maana yake ni ugonjwa unaokuja baada ya kuwa umeambukizwa virusi vya UKIMWI labda miaka mitano ama kumi huko nyuma, kinga ikashuka, sasa ndiyo unaanza kupata UKIMWI na kwa sababu kinga imeshuka, magonjwa ambayo kwa kawaida hayatokei kwenye watu wenye afya, yanaanza kutokea kwako kama magonjwa mbalimbali ya cancer mbalimbali, kama Kaposi’s sarcoma, magonjwa ya kukohoa kama Kifua Kikuu, magonjwa ya kifua kisichopona mara kwa mara; magonjwa ya ngozi kama herpes zoster na vitu vingine. Kwa hiyo, hapo tunasema sasa una UKIMWI.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wote tunajua kwamba maambukizi ya virusi vya UKIMWI au UKIMWI yanatokana na sababu kubwa ya kuwa na sexual partners wengi; lakini kwa hapa Tanzania na duniani kote inaonekana wanawake ndio wanakuwa wengi kuliko wanaume. Je, Mheshimiwa Waziri anatuambia sababu hasa ni nini? Kwa nini wanawake wanakuwa na maambukizi kuliko wanaume? Je, tatizo ni kwamba wanaume ndio wanawaambukiza zaidi au wanawake wanakosa maadili? Tusaidie kwa hilo.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nitazingatia muda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwamba wanawake wanaambukizwa zaidi kuliko wanaume; uwiano hauko mbali sana, tofauti ni ndogo, lakini ni kweli kwamba maumbile ya kibaiolojia ya wanawake ni tofauti sana na maumbile ya wanaume. Pia tabia za wanawake kuhusiana na ngono ni tofauti sana na tabia za wanaume kuhusiana na ngono.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanaume wengi wana tabia ya kuchepuka sana na mara nyingi wanaweza wakavitoa virusi nje wakavileta kwenye ndoa zao kwa wanawake ambao wametulia; hilo halibishaniwi. Kwa hiyo, nitoe rai kwa wanaume wenzangu kujipanga sana kwenye eneo hili la kuchepuka, kuachana na michepuko, lakini pia kupima afya zetu, kupima hali zetu lakini pia kupima hali za wenza wetu. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wale Waislamu wenzangu, tunapewa fursa ya kuoa wake hadi wanne; kuliko kuchepuka na watu usiowajua, unawakuta mtaani huko, ni bora ukapima na ukajiridhisha kwamba unayekwenda kumuoa yuko salama, ukatulia na wake zako wanne. (Makofi)

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, Serikali ina mikakati gani ya kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI katika Jamii? Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali lake ni refu kidogo; tuna mikakati gani ya kupunguza maambukizi mapya? Mikakati tuliyonayo ni mingi sana. Mkakati mkubwa wa kwanza ni kinga, kuzuia watu wasipate maambukizi ya UKIMWI kwa kutoa Elimu ya Afya kwa Umma.
Mkakati wa pili, ni tiba ambapo tunatumia zaidi ya kliniki zaidi ya 2000 za CTC (Care and Treatment Clinics) ambazo zimetapakaa nchi nzima mpaka kwenye ngazi za Vituo vya Afya kwa ajili ya kutoa dawa za ART (antiretroviral therapy) dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI, tukiamini kwamba watu ambao wanatumia dawa, wanapungua virulence, wanapungua kiwango ambacho wanaweza wakaambukiza. Kwa hiyo, hata ikitokea bahati mbaya akafanya ngono ambayo siyo protected anaweza asimwambukize partner wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, tuna mkakati wa kuongeza sasa idadi ya watu ambao tunawatibu, kwamba kila atakayepimwa na kubainika na Virusi vya UKIMWI kuanzia Oktoba, 2016 atatibiwa hapo hapo, ataanza kupata dawa za kupunguza makali ya Virusi vya UKIMWI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni mkakati mpya wa kisasa ambapo tumehama sana kwenye mikakati ambayo ipo preventive based tunahamia kwenye treatment based, kwamba badala ya kutoa tu kinga sasa tunatoa tiba zaidi. Kwa kufanya hivi, taratibu tutapunguza maambukizi mapya kwa kiasi kikubwa.

Name

Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 4

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali ilitoa elimu na tamko kuwa wanaume ambao hawajafanyiwa tohara wana maambukizo zaidi. Je, ni Mkoa upi ulioelimika na wanaume wengi kufanya tohara kwa hiari zao ili kuzuia kuambukiza maradhi ya UKIMWI?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni kweli nakubaliana na yeye kwamba kumekuwa kuna makabila mengi nchini ambayo traditionally hawapendi kufanya tohara ya kukata, wana tohara nyingine ambazo wanafanya za elimu na vitu kama hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua hilo na ndiyo maana tumeweka msisitizo sana katika suala hili. Kwenye Country Operational Plan ya mwaka huu tumepewa takribani milioni 526 za Kimarekani na Mfuko wa UKIMWI wa Rais wa Marekani (PEPFAR). Hizo pesa ndani yake pamoja na kuongeza watu 360,000 kwa ajili ya kuwapa dawa za ART lakini pia tutahamasisha na kuimarisha mkakati wetu wa kuwafanyia tohara wanaume katika mikoa ambayo predominantly hawapendi kufanya tohara ya kukata.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 5

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa niulize swali moja la nyongeza. Ugonjwa wa UKIMWI siyo tishio kwa maana ya kuua, tishio kubwa ni magonjwa nyemelezi. Kwa bahati mbaya Serikali imekuwa ikinunua dawa hasa hasa kwa ajili ya kufumbaza Virusi vya UKIMWI aina ya TLA (Tenofovir, Lamivudine na Efavirenz). Je, ni lini Serikali itaanza kununua dawa kwa ajili ya magonjwa nyemelezi (Opportunistic Infections -OI drugs) hasa hasa Azithromycin, Fluconazole na Co- trimoxazole?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inanunua dawa za Opportunistic Infections lakini siyo kwa kiwango ambacho tunanunua dawa hizi za UKIMWI za moja kwa moja kama hizo anazosema Mheshimiwa Mbunge za Tenofovir, Lamivudine, Zidovudine, Efavirenz na nyinginezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na upungufu tulionao sasa hivi tunaboresha kwa ujumla wake mfumo wa kutoa dawa nchini. Kwa hivyo, kadri mfumo wa dawa utakavyoboreka, dawa za kutibu magonjwa nyemelezi pia na zenyewe zitaongezeka kuwepo katika vituo vyetu. Kwa hivyo, ni lini, ni kadri tunavyoendelea kuboresha ndivyo ambavyo tutaendelea kuwa na dawa hizi kwenye vituo vyetu.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 6

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, Mwenyezi Mungu akupe wepesi katika siku hii ya leo kwa sababu Wabunge umewafurahisha sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Mheshimiwa Waziri, kuna watu wanafanya makusudi kabisa kuambukiza wenzao ugonjwa huu. Mtu anajua kama ni muathirika wa UKIMWI lakini anambukiza watu kwa makusudi hata watoto wadogo ambao ni wanafunzi wa vyuo. Je, Serikali ina mikakati gani kwa hawa ambao wanafanya maambukizi ya makusudi kwa wanafunzi wa vyuo na hata kwa ambao hawajaambukizwa maradhi haya? Naomba tamko la Serikali. (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Bunge lako Tukufu palitungwa sheria ambayo inatoa adhabu kwa watu ambao wataambukiza wengine Virusi vya UKIMWI kwa makusudi huku wakijua kwamba wana Virusi vya UKIMWI. Kwa hivyo, ili sheria hii iweze kufanya kazi ni watu kuripoti kwamba wameambukizwa Virusi vya UKIMWI kwa makusudi. Watakaporipoti, mkondo wa sheria utafuata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kwanza watu wenyewe wapime, kwa mfano wewe unazungumzia mabinti, maana yake mabinti wapime wajue hali zao. Wakishajua hali zao hata ikitokea ameambukizwa na mtu ambaye hakupima naye anaweza akasema wewe ndiyo umeniambukiza kwa sababu mimi nilikuwa sina maambukizi. Kwa hivyo, wapime wajue hali zao na waweze kutumia kinga kama hawawezi kuacha kufanya ngono, lakini kama wanaenda kuoana basi wapime kila mtu ajue hali wakate wanaoana ili wasiambukizane bila kujua.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 7

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Nina swali dogo la nyongeza. Kwa nini Serikali isiwezeshe lishe kwa kaya duni ambazo zinatumia dawa za kupunguza makali ya UKIMWI?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hatuna mpango wa kuwezesha chakula kwenye kaya duni au kaya yoyote ile. Tunaamini wagonjwa na watu wengine wanapaswa kuhudumiwa na familia zao. Hata hivyo, tunatoa dawa ama kemikali ambazo zina nutritive effect, zina effect ya kuongeza lishe kwenye miili ya wagonjwa wanaotumia dawa hizi. Kwa hiyo, tunawapo multivitamins na dawa nyingine inatosheleza kwa kweli kuhimili mikikimikiki ya ART.

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 8

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa ugonjwa wa TB unaenea kwa hewa na sanasana naona Wizara inahamasisha sana watu kujikinga na UKIMWI lakini sijaona wanaweka nguvu sana kwenye ugonjwa wa TB na umeenea kwa kasi sana. Ni lini Serikali itatoa hamasa na kuwajulisha watu ugonjwa wa TB kuwa ni mbaya sana kwa vile huenea kwa hewa? (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ugonjwa wa Kifua Kikuu ama Tuberculosis unaibuka tu kwenye mwili wa mwanadamu, pale ambapo kinga yake imeshuka. Ndiyo maana sasa unauona upacha wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI, UKIMWI pamoja na Kifua Kikuu, sio kwamba ugonjwa haupo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana hata sisi wazima na tuna afya tuna vimelea vya Mycobacterium tuberculosis kwenye miili yetu lakini havitajionyesha mpaka tutakufa navyo kama hatutoshusha kinga za mwili wetu. Kwa hiyo, kwanza tuepuke maambukizi ya Virusi vya UKIMWI, lakini pili tuwe na tabia ya kupima afya zetu kwa kweli ili tuweze kudhibiti magonjwa kama haya kabla hayajatokea.

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Wataalam wa Afya wanaeleza kuwa mtu anaweza kuwa na virusi vya UKIMWI lakini hana ugonjwa wa UKIMWI:- Je, nini maana ya maelezo haya?

Supplementary Question 9

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mheshimiwa Waziri amesisitiza mara kadhaa kwamba tuwe na desturi ya kupima, ni kitu kizuri kwa sababu UKIMWI bado upo na sometime unaona kama umezoeleka hivi. Ni kwa nini sasa vile vipimo (disposable) haviko kwenye maduka ya dawa ya kawaida ili hayo maelekezo ya Waziri anayoyasema kwamba tuwe na desturi ya kupima iwe rahisi? Kwa sababu yale mambo ya kusema kwamba mtu atazimia ni ya kizamani. Ni vizuri vipimo vya UKIMWI viwe available madukani kama ilivyo kwa vipimo vya sukari, pressure na kadhalika ambavyo viko available madukani. (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni swali zuri na nieleze tu kwamba, katika hizi USD milioni 526 tulizopewa na Serikali ya Marekani kwenye mwaka huu wa fedha unaokuja, tumeweka mkakati wa kufanya majaribio ya self-test hiyo unayoisema. Kwa hivyo, tutaanza majaribio hayo, tunakwenda kisayansi, hii siyo blaa-blaa ya siasa mzee, tunakwenda kisayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunafanya majaribio tuone hasara na faida zake, tukijiridhisha kwamba ni kitu ambacho tunaweza tukakifanya ndiyo tuna launch sasa scale up project kwa nchi zima. Kwa hivyo, kwa mwaka huu tunafanya majaribio na ni hatua nzuri kwa sababu zamani tulikuwa hata tunaogopa kuruhusu watu kupimwa bila kuwa na ushauri nasaha kutoka kwa wataalam kwa kuepuka mambo mengine ambayo yangeweza kuibuka.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Nataka kutoa ufafanuzi kwenye swali la nyongeza la Mheshimiwa Khadija Nassir kwamba tuna mikakati gani ya kuzuia maambukizi mapya. Kati ya mkakati mkubwa ambao tumeutekeleza na tunaendelea kutekeleza katika kupunguza maambukizi mapya ya VVU ni kupunguza maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo hili tumefanikiwa sana, asilimia 92 ya vituo vyetu vya huduma takribani 5,200 vinatoa huduma ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Takribani wanawake zaidi ya asilimia 90 wote wanaohudhuria katika kliniki ambao ni wajawazito wameweza kupata huduma wale ambao wamekutwa na maambukizi. Tumefanikiwa sana Tanzania, kwa sababu ya mkakati huu, tumepunguza maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kutoka watoto 14,000 hadi watoto 6,500. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, huo ndiyo mkakati mkubwa na niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge katika maeneo yetu, katika majimbo yetu, tuwahimize wanawake wajawazito mara tu wanapojigundua kwamba ni wajawazito waende kliniki lakini pia wapime UKIMWI kwa sababu wataweza kuzaa watoto ambao hawatakuwa na maambukizi ya UKIMWI. Niliona nilisisitize hili. Ahsante sana. (Makofi)