Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI aliuliza:- Kwa kuwa Serikali kupitia Idara ya Misitu ina jukumu la kutathmini rasilimali zake ikiwemo miti:- • Je, Wizara inatekeleza kwa kiwango gani katika kufanya tathmini za idara zake kuangalia athari za magonjwa ya miti? • Je, nchi inazo ekari ngapi za mioto ya asili na iliyopandwa? • Je, hadi sasa ni ekari ngapi za miti zimekatwa kwa ajili ya mbao na mkaa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nina maswali mawili ya nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa tunajua umuhimu wa misitu na miti na kazi zake katika jamii na katika ekolojia, ni vizuri tukajua kwamba afya ya miti au misitu yetu ikoje. Sasa kwa kuwa kuna changamoto ya kibajeti kwenye Idara hizi za Tafiti za Misitu, napenda kujua Wizara inajipangaje ili kuweza kuweka sawa tathmini ya hali ya misitu nchini in terms za afya?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda kujua kwamba, Wizara inaweka mikakati gani madhubuti ili kuweza kuondokana na changamoto ya upotevu wa misitu kutokana na kukata miti ovyo au uvunaji holela wa miti? Sasa Serikali inajipangaje kujua ni aina gani ya miti na idadi ya miti inapangwa sehemu gani na inashirikishaje jamii ili zoezi hili liwe na manufaa na endelevu? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la kwanza, Wizara imejipangaje katika kuangalia afya ya miti? Kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi, chini ya Taasisi ya TAFORI ambayo ni mahususi kabisa kwa ajili ya kufanya tafiti, Serikali inafuatilia hali ya misitu nchini kwa namna ambayo ni endelevu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wote tunaangalia misitu yetu inaendaje ili kuweza kubaini matatizo yanayoweza kutishia uharibifu wa misitu kutokana na magonjwa na changamoto nyingine zinazohusiana na afya ya miti kwa mfululizo ambao, kwa kuwa ni endelevu, changamoto zinazoonekana zinashughulikiwa mara tu zinapogundulika huko kwenye misitu yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inawezekana kupitia jitihada mbalimbali ambazo ni za Serikali kwa maana ya kupitia bajeti za ndani. Pia kwa sababu suala la uharibifu wa mazingira, masuala ya maendeleo endelevu; haya ni masuala yanayotazamwa na dunia nzima kwa pamoja kwa sababu uharibifu wa mazingira unaathiri dunia yote kwa pamoja. Kwa hiyo, kupitia taasisi mbalimbali ambazo zina maslahi katika kuhakikisha kwamba kuna maendeleo endelevu na utunzaji wa misitu unakuwepo, Taasisi hii ya TAFORI mara kwa mara kwa kupitia maombi mbalimbali inapata support ya kibajeti na kuweza kukamilisha majukumu hayo.
Meshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, napenda kusema kwamba tunao Mkakati wa Taifa wa Kupanda na Kutunza Miti. Hapo awali tumekuwa tukielekeza nguvu kwenye kupanda miti peke yake, lakini sasa baada ya kuona kwamba baada ya kupanda miti bila kufuatilia utunzaji wake na kuhakikisha kwamba inakua, tunapoteza asilimia kubwa sana ya miti ambayo tumetumia rasilimali nyingi sana katika kuipanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika mkakati huu wa Taifa wa sasa hivi unaopita katika kipindi cha miaka mitano ijayo, kuanzia mwaka 2016 mpaka mwaka 2020, Ofisi ya Makamu wa Rais ikiwa ndiyo inayoongoza, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Ofisi ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Asasi za Kiraia, Washirika wa Maendeleo pamoja na Sekta Binafsi, wote katika mkakati huu wamegawana majukumu ya kuhakikisha kwamba tunafanya jitihada za kufikia lengo hili ambalo nimelisema hapo awali la kuweza kufikia upandaji wa miti 1,075,000 kila mwaka katika muda wa miaka 17.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya muda mfupi misitu yetu itakuwa katika hali yake ya afya ya kawaida.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI aliuliza:- Kwa kuwa Serikali kupitia Idara ya Misitu ina jukumu la kutathmini rasilimali zake ikiwemo miti:- • Je, Wizara inatekeleza kwa kiwango gani katika kufanya tathmini za idara zake kuangalia athari za magonjwa ya miti? • Je, nchi inazo ekari ngapi za mioto ya asili na iliyopandwa? • Je, hadi sasa ni ekari ngapi za miti zimekatwa kwa ajili ya mbao na mkaa?

Supplementary Question 2

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa nia ya Serikali ni kupanda miti nchi nzima ili kurudisha uoto wa asili uliopotea na vikundi vya Wilaya ya Lushoto vimeanza kutosha miche ya miti, hasa Kikundi cha Friends of Usambara. Je, Serikali itasaidiaje vikundi hivi, hasa hiki cha Friends of Usambara, maana mpaka sasa kimeshaotesha miche zaidi ya milioni tatu? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Serikali inaunga mkono jitihada zote ambazo zinafanywa na mtu mmoja mmoja, lakini pia hata na vikundi. Hii ni taarifa njema ambayo Serikali inapokea kwa mikono miwili, uwepo wa vikundi katika eneo ambalo amelizungumzia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba awaelekeze wale wanakikundi waweze kuwasiliana na Wizara ili tuweze kuona namna gani Wizara inaweza kuwa-support.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI aliuliza:- Kwa kuwa Serikali kupitia Idara ya Misitu ina jukumu la kutathmini rasilimali zake ikiwemo miti:- • Je, Wizara inatekeleza kwa kiwango gani katika kufanya tathmini za idara zake kuangalia athari za magonjwa ya miti? • Je, nchi inazo ekari ngapi za mioto ya asili na iliyopandwa? • Je, hadi sasa ni ekari ngapi za miti zimekatwa kwa ajili ya mbao na mkaa?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina misitu mikubwa miwili; kuna ule msitu ambao unahifadhiliwa na WMA (Ustawi wa Vijiji) na ule msitu wa Serikali ambao ni Msitu wa Nyera, Kipelele. Msitu huu ni msitu ambao tumeurithi kutoka enzi za Wakoloni, lakini mpaka leo harversting plan ya msitu ule haijatoka. Nini kauli ya Serikali kuharakisha harvesting plan ya msitu huu ili wananchi waweze kupata faida ya kuwepo kwa msitu huu wa Nyera, Kipelele? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika misitu miwili anayoizungumzia, labda niseme tu kwa ujumla, harvesting plan anayoizungumzia maana yake ni mpango wa uvunaji. Tunao mpango wa uvunaji ambao tumeupitisha hivi karibuni unaoeleza namna ambavyo tunaweza tukavuna misitu lakini tukizingatia uvunaji endelevu ili uvunaji usizidi kasi ya kukua kwa misitu na hatimaye tukajikuta kwamba tunamaliza misitu zaidi ya kuitunza na kuifanya iendelee kuwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wakati wowote ule Mheshimiwa Mbunge atakapopata nafasi aje Wizarani, tunaweza tukamwelekeza namna gani au tunaweza tukamwonesha harvesting plan jinsi ilivyo aweze ku-share na wananchi wa maeneo ambayo yanahusika kwa ajili ya matumizi ya wananchi wake.