Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Serikali imeziagiza Halmashauri zote za Wilaya nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya vijana na wanawake:- Je, Serikali imetoa kiasi gani kwa vikundi vya vijana na wanawake tangu zoezi hilo lianze?

Supplementary Question 1

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya wanawake na vijana hususan wa Mkoa wa Mwanza napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, kwa kuwa kumekuwa na tabia ya baadhi ya Halmashauri za Wilaya kutokutoa asilimia kumi kwa wanawake na vijana kikamilifu na nyingine kutokutoa kabisa; je, Serikali inachukua hatua gani juu ya Halmashauri hizi zinazokaidi agizo hili la Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa vikundi vya maendeleo vya wanawake na vijana vimekuwa ni vingi sana na fedha hii imekuwa ikinufaisha vikundi vichache; je, ni lini Serikali itaongeza asilimia hii ili iweze kunufaisha vikundi vingi na ukizingatia kwamba ikifanya hivyo itakuwa imepunguza kwa asilimia kubwa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mbunge kwa harakati zake kama kijana na kama mwanamke kugombea na kupambana kwa haki za wanawake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu suala la asilimia kumi, kwamba Halmashauri nyingine hazitengi; katika bajeti ya mwaka wa 2016/2017, tulipotenga bilioni 56.8 tulitoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote kwamba commitment ya bajeti ya Serikali katika 10 percent, yaani five ya vijana na five ya akinamama lazima itekelezwe. Katika hili tumeona kwamba mpaka mwezi Machi tumetoa bilioni kumi na saba, lakini mpaka juzi wakati tunafuatilia ina maana fedha zinaongezeka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba niwasihi hasa Waheshimiwa Wabunge, sisi ni wajumbe katika Mabaraza yetu, fedha zile zinakusanywa wala haziendi kwa Mpango haziendi Hazina, zinaishia katika Halmashauri zetu. Lazima kila kinachokusanywa kila mwezi tunapoingia katika Kamati ya Fedha tusikubali kupitisha ile bajeti, fedha zimekusanywa pale, lazima tutenge moja kwa moja five percent ya vijana na five percent ya akinamama ili tuwasaidie watu wetu kule site.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili Wakurugenzi wote ambao tumekubaliana lazima walitekeleze na tarehe 30 mwezi wa sita tutafanya assessment ya Wakurugenzi wote ambao wameshindwa ku-meet commitment hii ambayo ilikuwa ni guideline na maelekezo ya Kamati ya TAMISEMI ya Bunge hili wakati tunapitisha bajeti. Kwa hiyo wakurugenzi wote lazima wajiandae, hiyo ni miongoni mwa assessment tutakayoifanya katika performance ya kufanya kazi zao katika maeneo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kuongeza ten percent; naomba nimwambie dada yangu, hii ten percent yenyewe inatosha kwa sababu fedha zile kuna nyingine zinakwenda katika maendeleo, posho za Madiwani na posho ya vijiji. Asilimia kumi kinachotakiwa ni compliance tu, kama kila Halmashauri itaweza kutoa kweli asilimia kumi tutaweza kufanya vizuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwamba asilimia kumi inatosha, isipokuwa sasa lazima wajue tumetoa maelekezo kwamba katika ile asilimia kumi lazima watenge asilimia mbili kwa ajili ya walemavu katika Halmashauri zetu. (Makofi)

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Serikali imeziagiza Halmashauri zote za Wilaya nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya vijana na wanawake:- Je, Serikali imetoa kiasi gani kwa vikundi vya vijana na wanawake tangu zoezi hilo lianze?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa vijana wanaohitimu elimu ya sekondari katika nchi yetu ni kama 400,000 hivi na wanaokwenda kidato cha tano ni kama vijana 90,000, zaidi ya vijana 300,000 wanabaki. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuanzisha kambi maalum ili kusudi sasa vijana hawa waweze kupata misaada ya kutosha ya utaalam wa kilimo na ufugaji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo ni zuri, hata hivyo Serikali imesha-take initiatives za kutosha katika eneo hilo, ndiyo maana Serikali inashirikiana na wadau mbalimbali, na hivi sasa mikoa mbalimbali wameshaanzisha kambi za vijana katika jitihada za kujenga ujasiriamali, ujasiri na uzalendo. Jambo hilo limetokea katika Mkoa wa Tabora pamoja na Pwani na mikoa mingine na zoezi hilo linaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tuwashukuru wenzetu wa taasisi binafsi hasa shirika la Plan International ambalo kupitia mikoa mbalimbali kama vile Mkoa wa Morogoro, Lindi, Mtwara, Dar es Salaam, Pwani na mikoa mingine wameanza kupitisha programu maalum ya vijana kwa ajili ya kuwawezesha katika fani mbalimbali za ufundi. Hili limetoa mafanikio makubwa, zaidi ya vijana 9,500 wamepata skills hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba Serikali itawatumia wadau mbalimbali na nguvu za Serikali lakini na Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya nawashukuru sana, wameshaanza ku- take hiyo initiative kwa kufanya mabadiliko hayo makubwa; naamini tukifanya hivi tutawasaidia sana vijana wetu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Serikali imeziagiza Halmashauri zote za Wilaya nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya vijana na wanawake:- Je, Serikali imetoa kiasi gani kwa vikundi vya vijana na wanawake tangu zoezi hilo lianze?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri zilizo nyingi zinashindwa kutenga hii asilimia kumi kwenye Mfuko wa Vijana na Wanawake na hii inathibitishwa na ripoti mbalimbali za CAG, na ni ukweli kwamba tuna Mifuko karibu 19 ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Je, Serikali haioni sasa iko haja ya kupunguza Mifuko hii angalau kati ya miwili mpaka mitano ikiwemo hii iunganishwe kuwe Mfuko mmoja ili kuwe na ufanisi na iwafikie kweli wananchi? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ku- harmonize hii Mifuko tuwe na Mfuko mmoja nadhani ni suala la kuzungumzika, tutafanya tathmini ya kina. Hata hivyo katika Mfuko wa asilimia kumi kuna maelekezo sasa hivi tunayatoa. Sasa hivi zile fedha katika ten percent zinaingia katika deposit account kama unaingiza katika dust bin mwishowe hata assessment hatuwezi kufanya vizuri; ndiyo maana sasa hivi tunaangalia jinsi gani tutafanya; kama ikiwezekana tuwe na akaunti maalum ya Mfuko katika Halmashauri ili tuweze kui-monitor vizuri; ili zikiingia zinazorudi kutoka kwa watakaokopa tuweze kuisimamia vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni wazo zuri tutaendelea kuchukua yote haya ili hatimaye tuboreshe Mifuko hii iweze kuwasaidia vijana na akinamama na hatimaye tutatengeneza ajira kwa wananchi wetu.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Serikali imeziagiza Halmashauri zote za Wilaya nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya vijana na wanawake:- Je, Serikali imetoa kiasi gani kwa vikundi vya vijana na wanawake tangu zoezi hilo lianze?

Supplementary Question 4

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Kwa kuwa uwezo wa Halmashauri unatofautiana na Halmashauri nyingine ni duni kabisa hazina kipato zikiwepo Halmashauri za Hai, Siha, Rombo na kwingineko; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kufanya top up ili nia yao njema ya kuwezesha wanawake na vijana ifanane Tanzania nzima?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la mama ni zuri, Halmashauri zingine pato lake ni dogo lakini kutokana na wazo hilo zuri ndiyo maana Serikali ina mifuko mingine ya ku-top up. Kuna Mfuko kutoka katika empowerment programu yetu ambayo inasaidia na tuna fedha nyingi sana hapa, takribani kuna Mifuko 17.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo ni wazo zuri lakini Serikali imeshachukua initiative tayari, Mifuko hiyo ipo, isipokuwa jamii yetu wakati mwingine hawana taarifa sahihi kuhusu mifuko hiyo. Ndiyo maana sasa wakati programu hii inaendeshwa hapa Dodoma takribani mwezi mmoja uliopita uwezeshaji huo umeshatolewa na tumewaelekeza sasa Maafisa wetu wa Maendeleo ya Jamii waweze kushuka katika grassroot ili kuweza kuwaelimisha wananchi ni wapi watapata hizi fedha na uwezeshaji ili kujiinua kiuchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni wazo zuri na Serikali hivi sasa inaendelea ku-top up isipokuwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wafanye kazi yao sasa kuhakikisha jamii sasa inapata uelewa wa kutosha juu ya mifuko hii ili waweze kupata uwezeshaji wa kutosha.