Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Khatib Kai

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:- Serikali imeandaa utaratibu wa kuliwezesha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kufanya shughuli zake kwa kuwapatia posho mbalimbali ikiwemo ration allowance. Je, ni lini Serikali itaongeza posho hiyo iendane na maisha yalivyo sasa?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI KHATIB KAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya ufafanuzi wa Mheshimiwa Waziri naomba nimuulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri amekiri katika jibu la msingi kwamba askari wa jeshi sasa hivi wanalipwa posho ya shilingi 10,000 kwa siku hela ambayo kwa maisha ya sasa ni ndogo sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itawaongezea askari hawa posho kutoka shilingi 10,000 angalau hadi 20,000 kwa siku?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Jeshi letu la Tanzania limekuwa likipata sifa kitaifa na kimataifa kutokana na weledi na utendaji wake wa kazi, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba Jeshi hili halitoi malalamiko kwa posho wanazolipwa, hasa ukizingatia kazi wanazozifanya? Ahsante.

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, ni kwamba posho zinaongezwa kadri ya uwezo wa Serikali unavyoruhusu. Katika hili nimetoa mifano, kwamba tulianzia na shilingi 5,000 ikapanda mpaka shilingi 7,500 ikapanda mpaka shilingi 8,500 sasa ni shilingi 10,000; kwa hiyo, tutaendelea kuzipandisha posho hii kwa kadri uwezo wa Serikali utakavyoruhusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na la pili kuhusu malalamiko unayoyazungumzia; nataka nikueleze Mheshimiwa Mbunge ni kwamba kwa kiwango kikubwa posho zinazotolewa sasa kwa askari na maafisa wetu zimeboreshwa kwa kiwango kikubwa. Mimi nataka nikuhakikishie kwamba wengi wanafurahia posho hizi zinazotolewa. Kama nilivyosema hakuna kinachotosha, mara zote kutakuwa kunaupungufu tu. Kwa hiyo, kwa kadri uwezo utavyoruhusu tutaendelea kuwa tunazi-review kila mwaka posho zote kuangalia uwezekano wa kuzipandisha kadri uwezo wa Serikali utakavyoruhusu.

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:- Serikali imeandaa utaratibu wa kuliwezesha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kufanya shughuli zake kwa kuwapatia posho mbalimbali ikiwemo ration allowance. Je, ni lini Serikali itaongeza posho hiyo iendane na maisha yalivyo sasa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na posho za ration allowance kuwa ndogo lakini pia inasemakana kuna mpango wa kuzifuta posho hizi ili askari wasipewe cash wawe wanakula ration makambini. Je, ni kweli?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, posho ya ration tutambue madhumuni yake kwanza, madhumuni ya posho ya ration ni kumlisha askari na maafisa ili waweze kutekeleza majukumu yao. Sasa wako wale ambao wako kwenye makambi, wako wale ambao wanalazimika kula ili waweze kutekeleza majukumu yao, hao kuna wazabuni katika Makambi yote wanaopewa fedha hizo ili waweze kuwalisha, lakini wale ambao majukumu yao hayapo katika Kambi wao wanapewa fedha zao taslimu ili waweze kutumia wanavyoamua wao wenyewe.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:- Serikali imeandaa utaratibu wa kuliwezesha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kufanya shughuli zake kwa kuwapatia posho mbalimbali ikiwemo ration allowance. Je, ni lini Serikali itaongeza posho hiyo iendane na maisha yalivyo sasa?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Mimi nina swali moja tu; kwa kuwa Serikali imerejesha Kambi ya JKT Mpwapwa na kwa kuwa vijana wengi wa Wilaya ya Mpwapwa wanataka kujiunga na JKT Mpwapwa, je, ni taratibu gani watumie ili waweze kujiunga na ile kambi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba JKT ina azma ya kufungua makambi mapya katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Mpwapwa, na utaratibu utakaotumika wa kujiunga ni ule ule ambao unatumia sasa kwamba wakati ukifika JKT itatoa nafasi za vijana wa kujitolea kuomba ili kuingia katika makambi haya mapya. Kwa pale Mpwapwa haitokuwa vijana wa Mpwapwa peke yao, itakuwa kwa nchi nzima, tutazigawa nafasi kama tunavyozigawa sasa kupitia Wilayani na Mikoani na hatimaye vijana watajiunga na Kambi hiyo ya Mpwapwa itakapokuwa tayari kutoa mafunzo. Vile vile kwa siku zijazo tukiwa tayari kambi hiyo pia itatumika kwa vijana kwa mujibu wa sheria.