Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ni ya zamani sana, ni chakavu sana na wakati mwingine huduma hazitolewi kabisa. • Je, ni kwa nini Serikali imeitelekeza Wilaya ya Kasulu? • Je, mahakama hiyo itajengwa lini?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri mafupi ya Mheshimiwa Waziri Profesa Kabudi. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Swali la kwanza, Mheshimiwa Waziri kwa kuwa Mahakama hiyo tumeisubiri kwa muda mrefu na umekiri kwamba mkandarasi amepatikana, je mkandarasi huyo anaitwa nani? Na mkandarasi huyo atajenga kwa gharama gani, kwa maana kama amepatikana atakuwa anajulikana na gharama ya ujenzi inajulikana?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali dogo la pili; pale pale Kasulu kilomita kama 10 hivi kuna Mahakama ya mwanzo ya Heru Juu, na bahati nzuri mimi kule Heru Juu ndiko ninakozaliwa, Mahakama ile iliangukiwa na mti mwaka 2010 na bahati nzuri Mtendaji Mkuu wa Mahakama alifika pale akaiona. Je, hiyo Mahakama ya mwanzo ya Helujuu ni lini itakarabatiwa, maana haijengwi, inakarabatiwa, ili wananchi waendelee kupata huduma za Mahakama ya Mwanzo katika Mahakama ile? Ahsante.

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mkandarasi ambaye atajenga Mahakama ya Wilaya ya Kasulu anaitwa Morad Tanzania Ltd. ambaye pia ndiye amejenga Mahakama ya Kibaha. Gharama ya ujenzi wa mahakama hiyo nitamuomba Mheshimwa Mbunge baadaye nimpe ili ajue ni kiasi gani. Hata hivyo haitazidi gharama ambayo imetumika kwa ile Mahakama ya Kibaha na kama umeona kitabu cha bajeti ya mwaka huu kule nyuma Mahakama ile ya Kibaha umeiona na ndivyo itakavyokuwa Mahakama ya Kasulu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mahakama ya Mwanzo ya Heru Juu, kijiji ambacho na mimi nimewahi kufika na nimekipenda sana, napenda nikuarifu kwamba Mahakama ya Mwanzo ya Heru Juu itaanza kujengwa katika mwaka wa 2017/2018.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ni ya zamani sana, ni chakavu sana na wakati mwingine huduma hazitolewi kabisa. • Je, ni kwa nini Serikali imeitelekeza Wilaya ya Kasulu? • Je, mahakama hiyo itajengwa lini?

Supplementary Question 2

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Uchakavu katika Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ni sawa na hali ilivyo katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda. Jengo ni la kizamani, dogo na halikidhi mahitaji ya sasa ya Wilaya na Mkoa kwa ujumla. Ni lini Serikali itajenga jengo jipya la Mahakama ya Wilaya ya Mpanda?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu la mjumbe, niwe na hakika, Mbunge ni Kapufi!

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama ya Wilaya ya Mpanda imepangiwa kujengwa katika mwaka wa fedha 2019/2020. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ni ya zamani sana, ni chakavu sana na wakati mwingine huduma hazitolewi kabisa. • Je, ni kwa nini Serikali imeitelekeza Wilaya ya Kasulu? • Je, mahakama hiyo itajengwa lini?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kama ilivyo Mahakama ya Kasulu ni chakavu, lakini Wilaya ya Liwale ni Wilaya ambayo ina umri wa miaka 42 mpaka leo haina jengo la Mahakama. Jengo linalotumiwa ni lile jengo ambalo lilikuwa Mahakama ya Mwanzo ambalo sasa hivi limechakaa limefika mahali ambapo mafaili yanafunikwa na maturubai. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuijengea Liwale Mahakama ya Wilaya?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama ya Wilaya ya Liwale itajengwa mwaka 2017/2018.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO aliuliza:- Mahakama ya Wilaya ya Kasulu ni ya zamani sana, ni chakavu sana na wakati mwingine huduma hazitolewi kabisa. • Je, ni kwa nini Serikali imeitelekeza Wilaya ya Kasulu? • Je, mahakama hiyo itajengwa lini?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa Jimbo la Kavuu na Mkoa mzima wa Katavi, kutokana na jiografia yake imekaa kama umbo la pweza. Je, Serikali inafikiria nini katika Jimbo la Kavuu, Halmashauri ya Mpingwe kuanzisha Mahakama yenye hadhi ya Wilaya kutoka kwenye hadhi ya Mahakama ya Mwanzo ili kuwanusuru wananchi kwenda katika makao makuu ya Nyonga ambayo wanapita katikati ya mbuga na kuhatarisha maisha yao?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi yake nimeyasikia tutayafanyia kazi, na baada ya hapa namuomba tuonane katika ukumbi wa Bunge ili tuweze kuongea na nielewe hasa nini kifanyike kwa ajili ya eneo hilo. (Makofi)