Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA) aliuliza:- Baadhi ya vituo vya Polisi na Magereza nchini vina majengo chakavu sana vikiwemo Kituo cha Polisi Bagamoyo na Gereza la Kigongoni Bagamoyo:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kujenga nyumba za Polisi na Askari Magereza Bagamoyo?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri yenye kuleta matumaini ya ujenzi wa Vituo vya Polisi na Magereza, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Gereza hili la Kigongoni lina changamoto kubwa ya tatizo la mgogoro wa mpaka wa ardhi kati yake na wananchi wa Sanzare na Matibwa, mgogoro huu umepelekea uvunjifu wa amani mara kadhaa. Je, ni lini Serikali itashirikiana na uongozi wa Wilaya ya Bagamoyo katika utatuzi wa mgogoro huu?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Mkoa wa Pwani ukiachia Wilaya ya Mafia una tatizo kubwa la kutokuwepo kwa Vituo vya Polisi na kwa kuwa kuna hali tete ya usalama katika maeneo hayo ya Wilaya za Mkoa wa Pwani ukiacha Mkuranga, Kibiti na Rufiji. Pia kwa kuwa Wilaya ya Mkuranga imeanza ujenzi wa Kituo cha Polisi kwa ushirikiano wa Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo na wananchi wa Wilaya ile ya Mkuranga. Je, ni lini Serikali itakubali kuisaidia Wilaya hii ya Mkuranga kukamilisha kituo hicho cha Polisi ili kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Mbunge na wananchi wake? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa maswali yake mazuri. Nikianza na la kwanza la mgogoro uliopo kati ya Gereza pamoja na wananchi wa kule Bagamoyo, nikiri ni kweli mgogoro huo upo na Mheshimiwa Mbunge Dkt. Shukuru Kawambwa amekuja mara kadhaa Ofisini na mara nyingine aliongozana na baadhi ya viongozi.
Mheshimiwa Spika, kitu tulichomuahidi ni kwamba baada ya Bunge, ama tukipata fursa baada ya kupigia kura bajeti, tutatembelea eneo husika tukiwa na Timu ya Mkoa ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ili tuweze kujionea wapi na nini chanzo cha mgogoro huo na njia nzuri ya kulimaliza tatizo hilo ili wananchi wake wasipate shida na uwepo wa Gereza hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusu kuunga mkono jitihada za Mbunge wa Mkuranga, ni kweli na Mbunge anafanya kazi nzuri sana na sisi kama Serikali ukanda ule tumeupa Mkoa Maalum wa Kipolisi, kwa hiyo Wilaya zote ambazo zinakaa ukanda ule ikiwemo Mkuranga tutazipa umuhimu na upendeleo unaostahili ili tuweze kupata makazi ya Askari, Ofisi za Polisi pamoja na Ofisi za Kanda na kwa pamoja na wingi wa Askari ili kuweza kusaidia shughuli za usalama katika eneo hilo ili wananchi waweze kufanya kazi bila kuwa na hofu yoyote. (Makofi)

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA) aliuliza:- Baadhi ya vituo vya Polisi na Magereza nchini vina majengo chakavu sana vikiwemo Kituo cha Polisi Bagamoyo na Gereza la Kigongoni Bagamoyo:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kujenga nyumba za Polisi na Askari Magereza Bagamoyo?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa watu wanaokwenda kwenye Magereza ni wahalifu na huwa wamehukumiwa, naomba Wizara ya Mambo ya Ndani iniambie na itoe kauli hapa, ni lini Gereza la Muleba litaenda kuzungushiwa fensi, maana yake leo Gereza la Muleba lina uzio kwa maana wafungwa wakiamua kuondoka leo, kesho wanaondoka, mtawakamata wale viongozi bure, sasa nataka commitment ya Serikali ni lini itafanya emergence ya kwenda Muleba kuweka uzio wa Magereza?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, ni kweli Gereza la Muleba linahitaji kuwekewa uzio, tunatambua na tumejipanga kwamba wakati wowote ambapo tutakamilisha kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa uzio huo tutafanya hiyo kazi. Jambo hilo tunalitambua na lipo katika vipaumbele vyetu.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA) aliuliza:- Baadhi ya vituo vya Polisi na Magereza nchini vina majengo chakavu sana vikiwemo Kituo cha Polisi Bagamoyo na Gereza la Kigongoni Bagamoyo:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kujenga nyumba za Polisi na Askari Magereza Bagamoyo?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kituo cha Polisi cha Himo ambacho kinatoa huduma kwa wakazi takribani 400,000 na kiko mpakani, Serikali iliahidi hapa kwamba itafanya ukarabati wa miundombinu ya kituo hicho hasa Ofisi. Sasa ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya tangu mwaka jana na hali ya kituo inazidi kuwa hoi bin taabani? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, jibu la suala hili, halitofautiani sana na jibu langu nililojibu mwanzo, kwamba kituo hiki cha Himo ni moja kati ya vituo ambavyo vina changamoto na hasa ukitia maanani kipo karibu na mpakani kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amezungumza. Kitu ambacho kimekwamisha kama ambavyo nimezungumza mwanzo ni suala la bajeti. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira tuna mpango wa kujenga vituo na kukarabati vituo vingi nchini kama nilivyozungumza katika jibu langu la msingi kwamba tuna upungufu wa vituo katika Wilaya 25 na vituo vingi vipo katika hali mbaya nchini, lakini tutafanya kazi ya kuvirekebisha na kujenga hatua kwa hatua.

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA) aliuliza:- Baadhi ya vituo vya Polisi na Magereza nchini vina majengo chakavu sana vikiwemo Kituo cha Polisi Bagamoyo na Gereza la Kigongoni Bagamoyo:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kujenga nyumba za Polisi na Askari Magereza Bagamoyo?

Supplementary Question 4

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Gereza la Bukoba Mjini linakuwa na msongamano mkubwa sana wa wafungwa na tuna Magereza ambazo zimechakaa sana kwa mfano kama Kitengule, Rwamlumba ni lini Serikali itapanua hiyo Rwamlumba ili kuweza kuwapunguza wafungwa walioko Bukoba Mjini? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, tumekuwa tukitenga pesa za bajeti kuongeza mabweni mwaka hadi mwaka na hii ni kwa sababu ya kutambua changamoto za msongamano wa Magereza yetu nchini. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo tumelipokea, tutajitahidi katika mwaka wa fedha ujao tuweze kuweka Gereza Bukoba Mjini miongoni mwa Magereza ya vipaumbele vya kuongeza mabweni ili kupunguza idadi ya msongamano katika Magereza yetu nchini.