Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE (K.n.y MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko ya kupokea dawa za ARV zilizokwisha muda wa matumizi (expired) kwenye vituo vya afya katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Mkoa wa Kigoma kwa ujumla:- Je, ni lini Serikali itafanya ukaguzi katika Manispaa ya Ujiji na Mkoa wa Kigoma ili kubaini ukweli wa malalamiko hayo?

Supplementary Question 1

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Naibu Waziri bado kuna malalamiko makubwa juu ya dawa hizo zilizopitwa na wakati na bado watu wanapata dawa zilizopitwa na wakati. Hapa katika jibu lake amesema kuna watu wanaofuatilia, je, ni nani anaeyefanya monitoring ya Kamati hiyo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuna wagonjwa ambao mpaka sasa hivi wanapata matatizo kwa sababu vituo vyao ni mbali, wanatembea umbali mrefu na wengine wanakata tamaa wanaamua kuacha dawa. Je, Serikali ina mkakati gani kuongeza vituo? Ahsante.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza nani anayefanya monitoring ya Kamati hiyo. Kwanza hii Kamati ya Dawa ni Kamati ambayo ipo kwenye kila kituo na Kamati hii inahusisha Watumishi kwa maana ya wataalam kwenye kituo husika lakini pia inahusisha wawakilishi wa wananchi ambao wanaingia kwenye Kamati hiyo ili kulinda maslahi ya watumiaji wa huduma za afya kwenye kituo.
Mheshimiwa Spika, kwa msingi huo, hii ni Kamati shirikishi na ushirikishi wake unaifanya Kamati hii ipate uhalali wa macho ya wananchi kwa sababu wananchi moja kwa moja wamewakilishwa na kwa msingi huo wanajua wanachokipokea na wanashiriki aidha, kwa kusaini ama kwa kushuhudia mtu ambaye anasaini nyaraka hizo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama kuna upungufu wowote ule ambao unaweza kuwa umejitokeza, basi ushiriki wa wananchi kwenye eneo hilo utakuwa ni mdogo. Nitoe rai kwa Mheshimiwa Mbunge ashiriki yeye pamoja na Baraza la Madiwani kufanya ufuatiliaji wa kazi inayofanywa na Kamati ya Dawa ya kila Kituo na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetimiza wajibu wetu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, jibu letu ni kwamba, wanaofanya Monitoring ni wenye mali, wenye mali ni wanaomiliki Kituo husika na wanaomiliki kituo husika, maana yake ni wananchi na wananchi wamehusishwa humo ndani na wawakilishi wa wananchi, ni wasimamizi wa vituo vyao vyote ndio maana wanaenda kufanya supportive supervision kila mwezi na kuna bajeti kwenye Halmashauri zote nchini ya kufanya hivyo.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu mkakati ya Serikali kuongeza vituo, kwanza kusema umbali ni mrefu sana hapana, kwa sababu toka Alma-Ata declaration hata kabla ya hapo toka Afya kwa wote miaka hiyo ya 70 Serikali imekuwa ikiongeza idadi ya Vituo siku hata siku na mwishoni tumekuja kuweka hili Azimio kwenye Ilani ya Uchaguzi kwamba tutajenga Kituo cha Afya kwenye kila Kata na Zahanati kwenye kila Kijiji ambalo sasa hivi tuko mbioni kutekeleza kwa kiasi fulani.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, uwezo wetu wa kuwa na vituo ambavyo vipo karibu na wananchi umeongezeka sana toka miaka hiyo ambayo naisema ya Azimio la Afya kwa wote la miaka ya 1971 – 1972 na kwamba kuna umbali mrefu, hapana. Sema tumejiongezea malengo, sisi wenyewe tumeongeza target, targets za zamani zilikwishafikiwa na Serikali zilizopita, kwa hiyo tunachokifanya sasa hivi ni kuboresha huduma na kuongeza tena vituo vingi zaidi, lakini hakuna umbali mrefu.
Mheshimiwa Spika, nilitaka kukanusha hilo ili kuweka sawa. Pia mkakati wetu ni huo ambao nimeusema wa kujenga Kituo cha Afya kwenye kila Kata na Zahanati kwenye kila Kijiji.