Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:- Shule ya Sekondari ya Lupembe iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ni ya muda mrefu na tulishaomba na kufanya maandalizi ya kuwa na Kidato cha Tano kwa Mchepuo wa CBG. Je, ni lini Serikali itaanzisha Kidato cha Tano katika Shule hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa shule nyingi zimekuwa na matatizo ya kutokuwa na Walimu hasa shule zile za A-level zenye michepuo ya sayansi. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba shule hizi ambazo zina michepuo ya sayansi zinakuwa na Walimu wa kutosha ili wanafunzi hawa waweze kusoma vizuri na kuweza kumudu masomo yao vizuri.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa imekuwa ni kawaida kwa shule za Serikali kuongeza tahasusi kwenye shule hizi za A-level ambavyo huenda sambamba na ongezeko la wanafunzi. Katika shule hizi za A-level utakuta wanafunzi ni wengi na miundombinu haitoshi ukilinganisha na idadi ya wanafunzi. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba ongezeko la wanafunzi linaenda sambamba na ongezeko la miundombinu kwa maana ya madarasa, mabweni na miundombinu mingine? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli tumekuwa na changamoto ya Walimu hasa wa sayansi katika shule zetu na ndiyo maana hapa katikati tuliomba kibali kutoka Ofisi ya Rais, Utumishi na tulipata kibali cha kuajiri Walimu na Walimu wale sasa hivi tumewaajiri kuwapeleka sehemu mbalimbali. Hata hivyo, bado hatujaweza ku-fill hiyo gaps yote iliyonanii na hii ni kutokana na jinsi hali ilivyo huko katika soko.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tutaendelea kufanya kila liwezekanalo, hivi sasa tuko katika mchakato kwa lengo kwamba tukipata wale Walimu wengine ambao maombi yao yalikuwa hayajakamilika vizuri, tuweze kuongeza kupeleka katika shule zetu ili tupate Walimu wa sayansi kwa ajili ya kufundisha vijana wetu wanaojiunga na kidato cha tano na cha sita.
Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili kuhusu suala zima la miundombinu, ni kweli tumeliona hilo ndiyo maana ukiangalia hivi sasa hata wanafunzi waliofaulu na kukidhi vigezo hatukuweza kuwachagua wote kutokana na suala la miundombinu, wengine tutawachagua katika second selection.
Mheshimiwa Spika, Serikali sasa hivi imeweza kufanya harakati na kupata takribani shilingi bilioni 21 ili kuweka miundombinu katika shule zipatazo 85, ambazo tunajua tukifanya hivi itasaidia sana kuhakikisha vijana wetu watafika shuleni na kusoma katika mazingira salama na mwisho wa siku waweze kupata elimu bora kama Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyokusudia.