Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Mji wa Liwale unakuwa kwa kasi lakini una chanzo kimoja cha maji ambacho kwa sasa hakiwezi kukidhi mahitaji hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa maji. • Je, ni lini Serikali itachukua hatua ya kuwaondolea wananchi adha ya upatikanaji wa maji? • Je, mradi wa kumwagilia wa Ngongowele utakamilika lini?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa ninasikitika tu kwamba hili swali halijajibiwa; kwa sababu hapa nilizopewa ni story tu, nimeona hapa zimepatikana story tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tatizo letu Liwale ni kwamba Mji wa Liwale unategemea maji kutoka Mto Liwale na Mto Liwale sasa umekauka, kwa hiyo, shida yetu ni kutafuta chanzo cha pili mbadala cha maji. Sasa hapa Mheshimiwa Waziri anasema kwamba hatua ya awali yaani kwa muda mfupi wanakarabati matenki, wanakarabati chanzo cha maji na wananunua dira. Sasa unakarabati chanzo cha maji, unakarabati vipi? Mto umekauka unaukarabati vipi? Matenki unayokarabati unataka uweke nini na mita unazokwenda kufunga unataka zitoe nini? Hapo naona swali bado halijajibiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, katika muda mrefu wanasema wametenga shilingi bilioni 3.5 lakini hizi shilingi bilioni 3.5 kuna Halmashauri 14 zimewekwa hapa. Kwa nini sasa Mheshimiwa Waziri hajatenganisha kujua kwamba Halmashauri fulani ina kiasi gani maana kuzifumba hapa ni nini?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ninalouliza mo wamba, scheme ya Umwagiliaji ya Ngongowele itakamilika nini? Nimepewa story tu. Sasa nataka nijue hatua gani imefikiwa ili tuweze kupata chanzo cha maji mbadala kwa Mji wa Liwale, hilo ndio swali ambalo naomba niulize. Vilvile naomba nirudie, tunaomba mradi wa Ngongowele ukamilike. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kwenda na mimi kuangalia huo mradi?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, utangulizi umesema majibu yote ni story, sio story ndiyo ukweli ulivyo. Mto Liwale ambao ndiyo chanzo cha maji cha Mji wa Liwale unakauka kiangazi na ndio maana tunaweka sasa upembuzi yakinifu. Lakini nikwambie maana ya ukarabati, ukarabati ni kuongeza uwezo ndani ya huo ukarabati basi tutabaini ni eneo gani sasa baada ya mto kukauka tunaweza tukapata maji ambayo yatahakikisha yanahudumia Mji wa Liwale bila matatizo yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije kwenye swali namba moja; hatua tunayoichukua ni kufanya upembuzi yakinifu, upembuzi yakinifu utabaini chanzo cha maji cha kudumu pamoja na huo Mto Liwale. Ikiwa siwezi kuanza kuzungumza utafiti utakaofanyika lakini baada ya kufanyika itabainisha ni wapi tutakuwa na maji ambayo yatakuwepo kwa miezi 12 ama kwa visima ama kwa kujenga bwawa ili yale maji yanapokuwa ni mengi kipindi cha kiangazi tuyapeleke kwenye bwawa tuyahifadhi ili tuweze kuhakikisha kwamba sasa Mji wa Liwale unakuwa na maji mwaka mzima. Ndio hatua tunayoichukua sasa hivi tunachukua hatua ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umeuliza swali kuhusu mradi wa umwagiliaji utakamilika lini. Mradi ule ulikamilika, umepata madhara ya mafuriko. Sasa hivi tumepata fedha kutoka Serikali ya Japan, tunapitia miradi yote ambayo ilikuwa imekamilika lakini imepata matatizo mbalimbali yakiwemo ya kukosa maji, unakuta kwamba kilimo kinafanyika mara moja badala ya mara mbili. Kwa hiyo, tunafanya mapitio ya hiyo miradi ikiwemo mradi wako wa Ngongowele ili tuweze sasa kuhakikisha kwamba tunauimarisha ili wananchi waweze kunufaika na kile walichokitarajia. (Makofi)

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Mji wa Liwale unakuwa kwa kasi lakini una chanzo kimoja cha maji ambacho kwa sasa hakiwezi kukidhi mahitaji hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa maji. • Je, ni lini Serikali itachukua hatua ya kuwaondolea wananchi adha ya upatikanaji wa maji? • Je, mradi wa kumwagilia wa Ngongowele utakamilika lini?

Supplementary Question 2

MHE. KANGI A. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na kilio cha muda mrefu cha kutokukamilika mradi wa maji wa Kibara, mradi wa maji wa Bulamba na mradi wa maji wa Nyabehu na hata Mheshimiwa Waziri Mkuu Pinda alifika maeneo yale na Mheshimiwa Maghembe. Sasa nataka kujua miradi hiyo mitatu kwasababu ni zaidi ya miaka nane itakamilika lini kwa sababu Mbunge wao amepiga kelele sasa mpaka hata mate yamenikauka? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, umesema kwamba mradi umechukua miaka nane ni ukweli. Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji tumeianza kwenye bajeti ya mwaka 2006/2007; kwa hiyo, umakta ijumlisha mpaka leo unakuta inakwenda kwenye hiyo miaka saba mpaka miaka nane. Ndani ya hiyo programu tulikuwa na miradi 1810, hadi leo tumeshakamilisha miradi 1333, bado 477. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ndani ya hiyo ambayo imebaki ni pamoja na miradi yako Mheshimiwa Mbunge na tumeendelea kutenga fedha na mwaka wa fedha huu tulionao 2016/2017 tuliamua sasa kila Halmashauri kuiwekea bajeti, tukaweka maelekezo kwamba wakamilishe kwanza miradi inayoendelea kabla ya kuingia kwenye miradi mipya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe Mheshimiwa Mbunge, kama kuna changamoto yoyote ile ambayo kama Wizara tunaweza kuingilia kitaalam basi naomba tuwasiliane ili tuweze kushughulikia hilo kuhakikisha kwamba miradi hiyo imekamilika.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Mji wa Liwale unakuwa kwa kasi lakini una chanzo kimoja cha maji ambacho kwa sasa hakiwezi kukidhi mahitaji hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa maji. • Je, ni lini Serikali itachukua hatua ya kuwaondolea wananchi adha ya upatikanaji wa maji? • Je, mradi wa kumwagilia wa Ngongowele utakamilika lini?

Supplementary Question 3

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wanawake wa Mkoa wa Singida wametaabika sana na kero kubwa ya ukosefu wa maji safi na salama kwa muda mrefu sasa. Je, Serikali haioni imefika wakati muafaka wa kuvuta maji kutoka Ziwa Victoria kupitia Igunga hadi Mkoa wa Singida ili kuwaondolea wananchi wa Mkoa wa Singida kero hiyo? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikupongeze wewe ni mama na unawapenda akina mama na unajua jinsi wanavyopata shida ya maji. Mkoa wa Singida ni miongoni mwa Mikoa ambayo haina vyanzo vya uhakika vya maji na mabwawa yaliyopo kama Kindai, Lake Singidani yote yana maji ya chumvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa mawazo mazuri na sisi tunawaza hilo. Kupitia mradi wa maji wa Ziwa Victoria sasa tunafikisha maji Igunga tunafikiria kwamba tufanyeje kuyatoa pale Igunga tupandishe Mlima Sekenke ili yaje mpaka Singida. Hayo ni mawazo namba moja ambayo na sisi tunayapokea, Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba tutayafanyia kazi. (Makofi)

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Mji wa Liwale unakuwa kwa kasi lakini una chanzo kimoja cha maji ambacho kwa sasa hakiwezi kukidhi mahitaji hivyo kusababisha uhaba mkubwa wa maji. • Je, ni lini Serikali itachukua hatua ya kuwaondolea wananchi adha ya upatikanaji wa maji? • Je, mradi wa kumwagilia wa Ngongowele utakamilika lini?

Supplementary Question 4

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona.
Kwa kuwa katika Mkoa wa Njombe na hasa katika Halmashauri ya Mji wa Njombe kumekuwa na tatizo kubwa sana la maji kwa muda mrefu, kuna mradi wa Hagafilo ambao wananchi wale waliahidiwa kwamba wataletewa mradi huo na kwamba fedha zingetoka huko India lakini hadi sasa hakuna chochote kinachoendelea. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ni kweli Mji wa Njombe unapata huduma ya maji kutoka kwenye Mto unaopita pale Njombe na hiyo huduma haitoshelezi, lakini ni kweli kwamba Mji wa Njombe ni kati ya Miji 16 ambayo itafaidika na mkopo kutoka Serikali ya India.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ni kwamba kinachoendelea ni kwamba Kamati ya Madeni Hazina imeshakaa na kuridhia mkopo huo wa dola milioni 500. Kwa sasa Serikali kupitia Hazina wanakamilisha taratibu za kusaini ile financial agreement, pia Serikali kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji sasa hivi inaandaa makandarasi watakaofanya usanifu wa haraka ili tuweze kuwaza tenda kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya huo mradi kukamilika nikuhakikishie Mheshimiwa Mlowe kwamba Mji wa Njombe sasa utakuwa na maji ya uhakika ambayo wananchi watapata maji safi na salama kwa wakati wote.