Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y MHE. ALLY S. UNGANDO) aliuliza:- Asilimia 90 ya wakazi wa Delta ya Mto Rufiji katika Kata ya Salale, Maparoni, Mbuchi na Kiangoroni ni wavuvi ambao hutumia mitumbwi isiyo na mashine na ndilo eneo pekee katika mwambao wa Bahari ya Hindi kunapatikana samaki aina ya kamba (prawns) kwa wingi; na kwa kuwa Ilani ya Uchaguzi wa CCM ya mwaka 2015 imeazimu kuwapatia wavuvi wadogo wataalam, vifaa vya kisasa vya uvuvi ili wajiendeleze na kuongeza Pato la Taifa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo semina kuhusu uvuvi bora wa kisasa? (b) Kwa kuwa mikopo hutolewa kwa vikund mbalimbali; je, Serikali itatoa mikopo kwa vikundi vya uvuvi vilivyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu haya ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Waziri katika majibu katika majibu ya msingi ameeleza kwamba Wilaya za Kibiti, Rufiji na Wilaya yangu ya Mkuranga ni miongoni mwa Wilaya ambazo wavuvi wake hajaomba mikopo. Inawezekana kabisa kutokuombwa kwa mikopo hii ni kutokana na ukosefu wa elimu ya kuweza kuwafahamisha na kuwawezesha waweze kuwa na uelewa wa kuomba hii mikopo.
Sasa swali langu, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri aniambie moja kwa moja ni lini tunaweza tukashirikiana sisi na wao ili kwa haraka zaidi Watanzania hawa wa Kisiju, Kibiti Delta na Rufiji mpaka Bagamoyo waweze kutumia fursa hii ya mikopo inayotolewa? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ulega siyo mgeni sana kwenye Ofisi ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, kwa hiyo, naendelea kumkaribisha amekuja mara nyingi sana kufuatilia changamoto za wananchi wake, aje ofisini hata akitaka leo mchana tuongee na tuangalie namna ya kufikisha elimu hii kwa ukubwa zaidi kwa sababu tayari Halmashauri zinatakiwa zitoe elimu kwa wavuvi na kuwafahamisha kwamba kuna fursa hiyo. Kama nilivyosema niko tayari kukaa naye tuweke mkakati wa kupeleka elimu zaidi.

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y MHE. ALLY S. UNGANDO) aliuliza:- Asilimia 90 ya wakazi wa Delta ya Mto Rufiji katika Kata ya Salale, Maparoni, Mbuchi na Kiangoroni ni wavuvi ambao hutumia mitumbwi isiyo na mashine na ndilo eneo pekee katika mwambao wa Bahari ya Hindi kunapatikana samaki aina ya kamba (prawns) kwa wingi; na kwa kuwa Ilani ya Uchaguzi wa CCM ya mwaka 2015 imeazimu kuwapatia wavuvi wadogo wataalam, vifaa vya kisasa vya uvuvi ili wajiendeleze na kuongeza Pato la Taifa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo semina kuhusu uvuvi bora wa kisasa? (b) Kwa kuwa mikopo hutolewa kwa vikund mbalimbali; je, Serikali itatoa mikopo kwa vikundi vya uvuvi vilivyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wavuvi hata ho wa maeneo ya Rufiji na maeneo mengine wanaojishughulisha kwa mambo ya uvuvi wametengeneza Beach Management Units na hizi BMUs zina uongozi. Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa Wizara ya Kilimo pamoja na Halmshauri husika wakawa wanaviongezea nguvu hizi Beach Managementi Units kwa kuwasaidia kielimu hata na masuala ya kifedha?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema vikundi vya usimamizi wa rasilimali za uvuvi katika mwambao au tunaziita Beach Management Units ni kweli imekuwa ni fursa ambayo inaweza ikatumika katika kutoa elimu, lakini vilevile kutoa misaada mbalimbali ambayo inaweza ikawasaidia wavuvi kufanya shughuli za uvuvi katika utaratibu ambao ni endelevu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wowote ambao Serikali imetoa elimu tumetumia sana Beach Management Unit, Serikali ndiyo imesaidia kuzianzisha lakini niendelee kumsihi Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote kujaribu kuhimiza Halmashauri zao ambao kimsingi wao wanakaa kwenye Baraza la Madiwani kuendelea kutoa elimu kwa kupitia Beach Management Units lakini vilevile kuhakikisha kwamba tunatenga raslimali kwenye halmashauri zetu ili hiyo elimu iweze kutolewa kwa urahisi zaidi.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y MHE. ALLY S. UNGANDO) aliuliza:- Asilimia 90 ya wakazi wa Delta ya Mto Rufiji katika Kata ya Salale, Maparoni, Mbuchi na Kiangoroni ni wavuvi ambao hutumia mitumbwi isiyo na mashine na ndilo eneo pekee katika mwambao wa Bahari ya Hindi kunapatikana samaki aina ya kamba (prawns) kwa wingi; na kwa kuwa Ilani ya Uchaguzi wa CCM ya mwaka 2015 imeazimu kuwapatia wavuvi wadogo wataalam, vifaa vya kisasa vya uvuvi ili wajiendeleze na kuongeza Pato la Taifa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo semina kuhusu uvuvi bora wa kisasa? (b) Kwa kuwa mikopo hutolewa kwa vikund mbalimbali; je, Serikali itatoa mikopo kwa vikundi vya uvuvi vilivyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 3

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi niweze kusema kuuliza swali moja la nyongeza.
Tunatambua kwamba katika kupambana na uvuvi haramu hawa Beach Management Units wamekuwa wakisaidia sana, lakini kwa bahati mbaya sana walikuwa hapati kipato cha moja kwa moja, kwa hiyo wakati mwingine wanageuka wao nao kushiriki katika uvuvi haramu.
Je, ni lini Serikali itaanzisha huu ufugaji wa samaki kwa njia ya cage ambao utakuwa unawapatia vile vikundi wa Beach Management Units kipato cha ziada ili waendelee kutunza maeneo yetu haya ya Uvuvi?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue kwanza nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mathayo kwa sababu amekuwa mmoja kati ya Wabunge ambao wamejitahidi sana kuhakikisha kwamba wavuvi wao wanaingia katika ufugaji wa samaki vilevile uvuvi ambao ni endelevu, tunatambua jithata hizo zimezaa matokeo mazuri sana kwani katika eneo analotoka uvuvi haramu umepungua sana. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ufugaji wa samaki kwenye vizimba (cage culture) ni moja kati ya aina ufugaji wa sasa ambao Serikali imeamua kuhimiza wananchi wajihusishe nao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inachofanya ni kutoa elimu pamoja na kuweka mazigira wezeshi ambayo wavuvi mbalimbali wanaweza wakajihusisha katika cage culture kwa hiyo katika BMUs lakini vilevile kwa wavuvi mmoja mmoja kama kuna ambao wanataka kuingia katika ufugaji wa samaki katika vizimba Wizara yangu iko tayari kushirikiana na Halmashauri wanazotoka ili kutoa elimu ya njia sahihi ya kuweza kufanya ufugaji wa samaki kwenye vizimba.

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y MHE. ALLY S. UNGANDO) aliuliza:- Asilimia 90 ya wakazi wa Delta ya Mto Rufiji katika Kata ya Salale, Maparoni, Mbuchi na Kiangoroni ni wavuvi ambao hutumia mitumbwi isiyo na mashine na ndilo eneo pekee katika mwambao wa Bahari ya Hindi kunapatikana samaki aina ya kamba (prawns) kwa wingi; na kwa kuwa Ilani ya Uchaguzi wa CCM ya mwaka 2015 imeazimu kuwapatia wavuvi wadogo wataalam, vifaa vya kisasa vya uvuvi ili wajiendeleze na kuongeza Pato la Taifa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo semina kuhusu uvuvi bora wa kisasa? (b) Kwa kuwa mikopo hutolewa kwa vikund mbalimbali; je, Serikali itatoa mikopo kwa vikundi vya uvuvi vilivyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 4

MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja la nyongeza. Katika jibu la msingi la Mheshimiwa Waziri ametaja Wilaya ambazo zitapata fursa wavuvi hao Wilaya ya Pangani hakuitaja. Sasa ningependa kufahamu wana mpango gani na wavuvi wa Pangani hasa ukizingatia nao pia kuna uvuvi wa prawns, lakini pia wamesahaulika sana katika elimu, kitu ambacho wangeweza kupata elimu wangeweza kupata hiyo mikopo ambayo ingewasaidia katika suala zima la uvuvi. Ahsante (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, orodha ya Halmashauri au Wilaya ambazo nimetaja ni zile ambazo tayari zimeshanufaika na mpango huo wa wavuvi kupatiwa asilimia 40 ya fedha kwa ajili ya kununua vifaa vya uvuvi hasa injini za boti. Kwa hiyo, ninachosema mpango huu upo na unapatikana kwa Halmashauri zote ili mradi wenyewe wajipange na wakidhi vigezo halafu tutaoa asilimia 40.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Pangani, mimi nimefika Pangani na watu wa Pangani nawapenda sana, Mheshimiwa Aweso nilikutana naye kule. Kimsingi niliwaahidi kwamba wakijipanga kwenye vikundi, nipo tayari kuwasaidia waweze kupata asilimia hiyo 40. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namwambia vilevile mheshimiwa Mbunge wapangeni wavuvi wenu katika vikundi, watafute fedha asilimia 60 halafu baada ya hapo tutawasaidia kupata hiyo asilimia 40 waweze kununua injini na waweze kufanya uvuvi kwa njia ambayo ni rahisi zaidi. (Makofi)