Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Mkandarasi anayejenga Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino anaidai Serikali shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kukamilisha jengo la Halmashauri. Je, ni lini Serikali itamlipa mkandarasi huyo kiasi hicho cha fedha ili ujenzi huo uweze kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ilianzishwa zaidi ya miaka Kumi iliyopita na Halmashauri hii Makao yake Makuu yako karibu sana na Chamwino Ikulu. Kwa hiyo, nilitegemea Serikali ingeliangalia hili suala kwa jicho la kipekee kabisa. Idara za Halmashauri hii zimetawanyika, ukitoka Ofisi ya Mkurugenzi hadi Ofisi ya Ardhi ni kilometa tano.

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitoka Ofisi ya Mkurugenzi hadi Idara nyingine ambazo nyingine ziko kwenye shule za msingi, nyingine ziko kwenye nyumba za watu binafsi kwa hiyo, ufanyaji kazi na huduma kwa wananchi uko katika hali ngumu kabisa kutokana na jengo lile kutokamilika. Halmashauri waliwafuata TBA wakafanya tathmini wakaona kwamba, zinahitajika shilingi…

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa shilingi bilioni 2.3 na Serikali imetenga shilingi milioni 600 tu kukamilisha lile jengo.
Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha za kutosha kwa ajili ya lile jengo la Halmashauri na likamilike kwa wakati, japo floor ya chini, ili watumishi wahamie wakafanye kazi pale?
Swali la pili, Halmashauri ya Chemba iliomba shilingi milioni 950 kwa mwaka huu wa fedha na wamepata shilingi milioni 450 tu. Je, shilingi milioni 500 zilizobaki watapata lini ili waendelee na ujenzi wa jengo la Halmashauri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, watumishi wa Halmashauri ya Chamwino wanapata shida kubwa sana na hili tunalijua wazi. Ninajua kwamba mkataba wa kwanza wa mkandarasi wa kwanza umevunjwa lakini commitment ya Serikali iko pale pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali mpaka hivi asubuhi na-cross check pale tumeshapeleka shilingi milioni 750 hivi sasa. Kama ulivyosema tathmini iliyofanywa na TBA imeonekana kumaliza lile eneo la ground floor peke yake karibu ni shilingi bilioni mbili. Hata hivyo, nimeongea nimeongea na Kaimu Mkurugenzi pamoja na Engineer leo wafike ofisini kwangu kuangalia way forward tunafanyaje kwa sababu tathmini iliyofanywa gharama yake ni kubwa, lakini Engineer na timu yake wanasema kwa kutumia wao utaalamu wao pale ile shilingi milioni 750 wataweza kumaliza ile ground floor na hivi sasa tunajielekeza kuangalia jinsi gani fedha zitumike vizuri.
Kwa hiyo, nimemuagiza Kaimu Mkurugenzi na Engineer leo hii wanakuja kukutana na wataalam katika ofisi yetu tuangalie tufanye nini ili tumalize ile ground floor.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la ujenzi pale Chemba, ni kweli tumepeleka shilingi milioni 500 mpaka hivi sasa, tunachotaka kufanya ni kuhakikisha kwamba, fedha tunazipeleka maeneo haya na maeneo mengine tofauti, lengo kubwa ofisi hizi ziweze kukamilika na watumishi wetu wapate maeneo mazuri ya kufanya kazi. (Makofi)

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Mkandarasi anayejenga Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino anaidai Serikali shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kukamilisha jengo la Halmashauri. Je, ni lini Serikali itamlipa mkandarasi huyo kiasi hicho cha fedha ili ujenzi huo uweze kukamilika?

Supplementary Question 2


MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo Chamwino ndiyo tatizo lililopo Manispaa ya Tabora. Ofisi mpya ya Halmashauri imekwama kwa muda mrefu sasa kukamilika kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Kwa kuwa ombi maalum kupitia Hazina Serikali iliahidi kutoa shilingi bilioni mbili ili kuweza kukamilisha ujenzi huo pamoja na kumlipa mkandarasi anayedai karibu shilingi bilioni moja Masasi Construction.
Je, Serikali ni lini italeta pesa hiyo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ili jengo hili liweze kukamilika? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli lilikuwa ombi maalum, lakini tutaenda kulifanyia kazi. Siwezi kutoa commitment hapa lakini tutaenda kulifanyia kazi tuangalie kwamba lile ombi la awali limefikia wapi halafu tutapeana mrejesho nzuri na Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu najua ni kweli Manispaa ya Tabora wanapata shida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tutakwenda kuangalia jinsi gani tutafanya.

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Mkandarasi anayejenga Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino anaidai Serikali shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kukamilisha jengo la Halmashauri. Je, ni lini Serikali itamlipa mkandarasi huyo kiasi hicho cha fedha ili ujenzi huo uweze kukamilika?

Supplementary Question 3

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la Halmashauri ya Chamwino linafafana na tatizo la Halmashauri ya Tabora Uyui. Tuna zaidi ya miaka kumi tumeamia Isikizya, lakini jengo la Halmashauri yetu lina zaidi ya miaka mitano halijakamilika kutokana na kutoletewa pesa.
Je, ni lini Serikali itatusaidia ili kumalizia ujenzi wa jengo hilo. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema mwanzo ni kwamba maombi haya ya Halmashauri yako katika maeneo mbalimbali na ni kweli Mheshimiwa Mbunge nimefika kwako Uyui tulikuwa pamoja siku ile, kikubwa zaidi tutaangalia kipindi hiki kutokana na bajeti zilizotengwa katika mahali ambapo pesa ambazo hazijapelekwa basi tutafanya harakati ziwezekanazo mradi tuweze kupeleka fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niweze kusema kwamba commitment ya Serikali ni kuhakikisha kwamba kama tulivyofanya mwaka huu hivi sasa tumepeleka takriban bilioni 30 kwa Halmashauri mpya na Halmshauri mbalimbali kwa hiyo tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kuwezesha mpango huu wa Serikali ambao tumeupanga katika bajeti zetu. (Makofi)