Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Primary Question

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED aliuliza:- Kwa kipindi kirefu sasa Bandari za Tanga na Mkokotoni zimekuwa zikitumika na kusababisha maafa makubwa kwa watumiaji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha usalama wa wasafiri hao?

Supplementary Question 1

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ambayo hayako makini, majibu ambayo hayaendi sambamba na swali langu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mantiki ya swali langu lililenga usalama wa wasafiri pale na mali zao. Kwa kipindi kirefu sasa wananchi wanaotumia bandari mbili hizi, kila bahari inapopata michafuko kidogo wamekuwa wakifa kwa wingi sana pale.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inathibiti vifo vya watanzania katika bandari mbili hizi ambao mara kwa mara wanapotea wao na mali zao?
Swali langu la pili la nyongeza, inaoneka Serikali haikufanya utafiti wa kutosha. Swali langu halilengi ubora wa bandari, linalenga usalama wa raia wetu pale kati ya bandari mbili hizi.
Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kufuatana na mimi kuona mazingira halisi ya usafiri pale katika bandari ya Mkokotoni kwa sababu TRA wako pale wanakusanya kodi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama amenisikiliza vizuri katika jibu langu la msingi hatua ambazo tunazichukua ya kwanza ilikuwa inajibu swali lake kikamilifu. Hatua zilizofuata tumeongeza mipango mingine tunayoifanya, kwamba SUMATRA hufanya ukaguzi kila mwaka, vilevile hufanya kaguzi za kushtukiza kuhakikisha kwamba vyombo hivi vinavyoelea majini vinakuwa na usalama wa abiria na mizigo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili niko tayari, tutapanga tukubaliane siku ya kwenda na tukaelee majini kati ya Bandari ya Tanga na Mkokotoni ili tukubaliane haya ambayo Serikali inayasema na Mheshimiwa Mbunge anadhani kwamba hatuyajibu kikamilifu. (Makofi)

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED aliuliza:- Kwa kipindi kirefu sasa Bandari za Tanga na Mkokotoni zimekuwa zikitumika na kusababisha maafa makubwa kwa watumiaji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha usalama wa wasafiri hao?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nakubaliana na Waziri kwamba suala la kwanza ni ukaguzi, lakini kwa kweli suala la ujuzi na utaalam ndio muhimu sana katika uokozi.
Je, Serikali imejiandaa vipi katika suala hili la kutayarisha umma na wataalam wa kuweza kufanya uokozi kuliko kungojea kutibu badala ya kuzuia?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tumeongelea umuhimu wa shughuli za SUMATRA na hapa tuliongelea masuala ya ukaguzi, lakini unafahamu kwamba SUMATRA wana kituo kikubwa Dar es Salaam ambacho kinashughulika na masuala ya uokozi katika bahari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo hiki vilevile kina vituo vidogo Mwanza na wanawasiliana na vituo vingine vya sehemu mbalimbali katika Bahari ya Hindi ili kuhakikisha kwamba kama kunatokea tatizo lolote vyombo hivi ambavyo vinashirikiana hata na wenzetu wa Marine Service kuhakikisha kwamba usalama wa baharini unakamilika. Mheshimiwa Ally Saleh unafahamu kuna tower kubwa sana kwenye Bandari ya Dar es Salaam kazi yake kubwa ni kuhakikisha kwamba ina-coordinate shughuli zote za uokozi na wataalam tunao.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED aliuliza:- Kwa kipindi kirefu sasa Bandari za Tanga na Mkokotoni zimekuwa zikitumika na kusababisha maafa makubwa kwa watumiaji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha usalama wa wasafiri hao?

Supplementary Question 3

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo ya usafiri wa baharini ya Bumbwini yanafanana sana na matatizo ya usafiri baina ya Bandari ya Kilindoni, Mafia na Bandari ya Nyamisati, Kibiti. Wananchi wa Mafia wamekuwa wakisafiri katika maboti ya mbao ambayo si salama na hayana bima.
Je, ni lini Serikali itainunulia Wilaya ya Mafia boti ya kisasa kuondokana na tatizo la usafiri baina ya Bandari ya Nyamisati na Kilindoni ili kuepusha maafa? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbaraka Dau anafahamu kwamba Serikali ina mikakati maalum ya kuhakikisha inatatua tatizo la usafiri Mafia. Tukianzia kuhakikisha kwamba magati yanayotumika ni ya kisasa na yako salama. Kwa vyovyote vile magati haya yakishakaa salama tutavutia wawekezaji wa kuleta meli na kama ikitokea kwamba hakutakuwa na meli zitakazofika, pamoja na kuimarisha gati kwa maana ya gati iliyoko tayari pale Mafia, lakini vilevile hili linalopokea upande wa Bara, tukishakamilisha hizo kama hatutakuwa na wawekezaji binafsi watakaovutika kutoa huduma za usafiri nikuhakikishie Mheshimiwa Dau tutakaa pamoja tuangalie tufanyeje pamoja na Serikali tuone namna ya kutatua usafiri wa eneo hili la Mafia. (Makofi

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED aliuliza:- Kwa kipindi kirefu sasa Bandari za Tanga na Mkokotoni zimekuwa zikitumika na kusababisha maafa makubwa kwa watumiaji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha usalama wa wasafiri hao?

Supplementary Question 4

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hoja ya msingi ambayo inaonekana ni usalama wa raia wakati wakivuka. Mbunge wa Mafia alisema kutoka Nyamisati na Kilindoni, maboti yaliyoko pale ni maboti ya mbao, Serikali ina mikakati ya mrefu ufumbuzi haupatikani.
Swali la msingi sasa, Serikali ina mkakati gani wa ziada sasa kuhakikisha maboti haya yanayochukua abiria yamepewa uwezekano wa kuwa makoti ya kuokolea maisha (life jacket) ili kunusu maisha ya abiria?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tukianzia na lile swali la Mheshimiwa Dau, Serikali ina mpango wa kupeleka kivuko eneo lile, kwanza kazi inayofuata ni kufanya feasibility study, baada ya kufanya feasibility study na kujua bei ya hicho kivuko then tutapanga pesa kwa ajili kununua kivuko hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la Mheshimiwa Masoud ni kweli kwamba kuna tatizo hilo na tutahakikisha kwamba sasa hivi tunapeleka vyombo vyote kuhakikisha kwamba vinakuwa na life jacket ili ikitokea matatizo wananchi wale waweze kujisaidia. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED aliuliza:- Kwa kipindi kirefu sasa Bandari za Tanga na Mkokotoni zimekuwa zikitumika na kusababisha maafa makubwa kwa watumiaji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha usalama wa wasafiri hao?

Supplementary Question 5

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa swali la msingi linahusiana na usalama wa wasafiri, na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri aliahidi kuja maeneo ya Mbulu na kwa kuwa ile barabara ya lami ya kilometa tano ya Hydom na Dongobesh bado. Je, Mheshimiwa Waziri lini sasa atakuja Hydom kuangalia barabara ile ambayo haina usalama kwa wasafiri? Ahsante.

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli anavyosema Mheshimiwa Mbunge na niko tayari wakati wowote kwenda kutembelea eneo hilo. (Makofi)