Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ya Serikali na Taasisi zake. Je, Serikali inategemea kuchukua hatua gani ili kutekeleza azma hiyo ya kudhibiti matumizi ya fedha za umma katika taasisi zake?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali na hatua ambazo zimechukua katika kudhibiti matumizi ya fedha za umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya eneo ambalo limekuwa na matatizo makubwa katika taasisi za umma ni eneo linalohusu ununuzi wa vipuri na matengenezo ya magari pamoja na mafuta.
Swali la kwanza, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wafanyakazi wote walioko katika Menejimenti za Mashirika hayo wanakopeshwa magari badala ya kutumia magari ya Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ndiye mwenye wajibu wa kukagua hesabu zote za Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na Taasisi za Umma, lakini kwa muda mrefu tumeona kwamba hesabu za taasisi za umma, Mkaguzi Mkuu amekuwa akizipatia sekta binafsi zimekuwa zikikagua kwa niaba yake, lakini sekta hizo binafsi zimekuwa ziki-charge fedha kubwa sana ya ukaguzi. Je, ili kupunguza matumizi Serikali ina mpango gani wa kuimarisha ofisi ya CAG ili iweze kufanya kazi hiyo sawa sawa badala ya kutumia sekta binafsi?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ununuzi wa vipuri na matengenezo na watumishi kukopeshwa magari, tunapokea wazo lake zuri na tutalifanyia kazi kuona ni jinsi gani utekelezaji wake ili kuona tunapunguza matumizi haya kama alivyosema kwenye magari. Tusisahau pia ni taratibu na kanuni za utumishi ndizo ambazo zinaelekeza haya yote ambayo yanatendwa na Serikali yetu, pale ambapo itaonekana inafaa tofauti na uamuzi uliopo sasa, basi Serikali yetu haitasita kufanya hivyo ili kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kama ambavyo Serikali imekusudia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuimarisha ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, napenda kuliambia Bunge lako Tukufu Serikali yetu inatambua umuhimu wa ofisi hii ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na imekuwa ikiimarisha kila mwaka hatua kwa hatua kuhusu wafanyakazi kupewa ujuzi lakini pia kuhusu na bajeti yake. Sote ni mashahidi tumeona juzi tumepitisha bajeti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na imeongezeka kama Bunge lako Tukufu ambavyo ilipendekeza, ni imani yangu ofisi hii itakagua ofisi zetu na taasisi zote za umma pale ambapo inaonekana inafaa.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ya Serikali na Taasisi zake. Je, Serikali inategemea kuchukua hatua gani ili kutekeleza azma hiyo ya kudhibiti matumizi ya fedha za umma katika taasisi zake?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NGUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na mimi kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika dhana ya kupunguza matumizi ya fedha na kubana matumizi katika Serikali, Serikali imekuwa inanunua magari kutoka kwa ma-dealers, magari haya huwa yanakuja na warrants ya kilometa laki moja au miaka mitatu matengenezo yanakuwa bure, lakini warrant hii Serikali imekuwa haitumii na badala yake imepeleka magari kwenye garage za watu binafsi na kutumia gharama kubwa sana.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwanza inasimamia hizi warrant, ikiwa ni pamoja na kuwa na mpango wa kununua magari kutoka kwa manufactures?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepokea ushauri wake tutaenda kuufanyia kazi na baadae tutamletea majibu stahiki.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:- Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ya Serikali na Taasisi zake. Je, Serikali inategemea kuchukua hatua gani ili kutekeleza azma hiyo ya kudhibiti matumizi ya fedha za umma katika taasisi zake?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri kujaribu kueleza sheria mbalimbali za kudhibiti fedha za umma, lakini kuna changamoto moja kubwa. Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali ndio mtu pekee ambaye amekuwa akisimamia na kudhibiti hili suala la umma na kutuonesha wapi kwenye mapungufu na matumizi sahihi. Lakini Serikali imekuwa haipeleki fedha za kutosha kwa CAG ili aweze kudhibiti hizi fedha.
Je, Serikali haioni kwamba yenyewe ndio yenye jukumu la kuzorotesha Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kushindwa kufanya kazi yake ili tuweze kujua hayo mapungufu, kwa kushindwa kupeleka hizo fedha?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu swali la pili la Mheshimiwa Hasunga kwamba Bunge hili hata wiki haijapita tangu tumepitisha Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango, ndani yake ikiwepo bajeti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na sote tumeona commitment ya Serikali yetu katika kuiongezea ofisi hii bajeti ya kutosha. Katika taasisi zote za Serikali ni taasisi hii tu ambayo imepata bajeti yake kwa mwaka huu kwa zaidi ya asilimia mia moja. Hii ni commitment ya kutosha kabisa na tunahakikisha kwamba itaendelea kuimarishwa kama nilivyosema. (Makofi)