Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Kampuni ya Group Sogesca Lanari Estero (GSLE) iliyokuwa inajenga barabara ya Nyanguge – Musoma kati ya mwaka 1979 – 1990 iliacha majengo katika Kijiji cha Yimtwila “A” ambapo Serikali kwa kushirikiana na wananchi wakaanzisha shule ya sekondari ya kutwa. Je, ni kwa nini Serikali isitumie fursa ya uwepo wa majengo haya kupandisha hadhi shule hiyo kuwa ya kidato cha tano na sita kwa kuwa nyumba za walimu na mabweni yanaweza kupatikana?

Supplementary Question 1

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, amekiri wazi kwamba Serikali ina mpango wa kuanzisha shule ya kidato cha tano na cha sita katika maeneo ya Mkula tofauti na maeneo yanayotumika kwenye majengo yaliyoachwa na Kampuni ya Group Sogesca.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza; itambulike kuwa shule hii ambayo ameizungumzia kwamba ni ya kutwa iko kwenye mgogoro baina ya wananchi pamoja na Kampuni ya SK iliyoko mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro huu Mheshimiwa Waziri Mkuu anaujua. Alipokuja kwenye ziara tarehe 2 mwezi wa tatu mwaka wa jana aliukuta mgogoro huu wa wananchi, kwamba shule hii iko kwenye majengo ambayo yana mgogoro. Nataka kusikia kauli ya Serikali, Waziri Mkuu aliagiza kuwa majengo yale yarudi kwenye mikono ya wananchi ili shule ile iweze kuendelea vizuri. Sasa nataka kuuliza, nini kauli ya Serikali kuhusu shuke iliyoko kwenye majengo yenye mgogoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa kipaumbele cha Serikali ni masomo ya sanyansi. Mkoa wa Simiyu walimu wa masomo ya sayansi ni changamoto kubwa sana hususan shule iliyoko Wilayani Itirima, shule ya Mwarushu ina mwalimu mmoja tu wa masomo ya sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kusikia sauti ya Serikali ni nini mkakati wa Serikali kupeleka walimu wa sayansi katika maeneo hayo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Dada yangu Gimbi Dotto, kumbe alikuwa anataka aniingize katika choo kisichokuwa na jinsia maalum, kwamba shule kumbe ina mgogoro halafu tuanzishe kidato cha tano na cha sita. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna mgogoro lakini nadhani Naibu Waziri wa Ardhi atazungumzia hasa katika suala hili la mgogoro jinsi gani Serikali imejipanga mara baada ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kutoa maagizo; Serikali inayafanyia kazi hayo yote kwa pamoja na nikuhakikishie Mheshimiwa Gimbi kwa sababu najua wewe ni mpiganaji mpaka umeniletea walimu ambao walikuwa na matatizo katika eneo lako kule. Siku zote unaniletea taarifa ofisini kwangu pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba tutashughulikia matatizo katika Mkoa huu wa Simiyu kwa kadri iwezekanavyo ili mambo ya elimu yaende vizuri. Kuhusu shule ambayo haina walimu wa sayansi, naomba tuseme kwamba katikati tulipeleka walimu wa sayansi lakini si kwamba tumeziba gap zote za walimu wa sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa tunaendelea kupeleka walimu wa sayansi. Tutaichukulia hii shule ambayo unaisemea kuwa ni kipaumbele, tutafanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kwamba tunapeleka walimu wa sayansi wa kutosha. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba watoto wanapata elimu vizuri. Kwa hiyo naomba uendelee na hizo juhudi zako nzuri za kuwawakilisha vizuri wananchi wako wa kule.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali dogo la nyongeza ambalo limeulizwa. Ninamshukuru pia Mheshimiwa Naibu Waziri ambaye amejibu swali lake vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimfahamishe Mbunge pengine wakati mwingine ni muhimu pale ambapo Serikali inachukua hatua tuwe tunaweza kuweka kumbukumbu zetu vizuri. Mgogoro huu anaouzungumzia tayari Serikali ilishaumaliza, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa Lukuvi alishakwenda kule na yule Bwana alinyang’anywa title yake na Mheshimiwa Rais alishaifuta, kwa hiyo hakuna mgogoro pale na SK Investment si mmiliki tena wa eneo lile kwa sababu Serikali imeshafuta umiliki wake na ilitangazwa kwenye vyombo vya habari, naomba tuwe tunafuatilia vizuri ili tusiwe tunachanganya haya mambo. (Makofi)

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Kampuni ya Group Sogesca Lanari Estero (GSLE) iliyokuwa inajenga barabara ya Nyanguge – Musoma kati ya mwaka 1979 – 1990 iliacha majengo katika Kijiji cha Yimtwila “A” ambapo Serikali kwa kushirikiana na wananchi wakaanzisha shule ya sekondari ya kutwa. Je, ni kwa nini Serikali isitumie fursa ya uwepo wa majengo haya kupandisha hadhi shule hiyo kuwa ya kidato cha tano na sita kwa kuwa nyumba za walimu na mabweni yanaweza kupatikana?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Shule hii iliyotajwa na Mheshimiwa Gimbi na ninapenda nimshukuru kwa swali lake, lengo lake ni kwamba kuipandisha kuwa high school, lakini kwa mpangilio wa Wilaya ya Busega tumeipanga kuwa ni Chuo cha VETA. Je, ni lini Serikali kupitia Wizara ya Elimu itatusaidia kuwa na shule ya VETA katika majengo haya Sogesca?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi ipo tayari kwa kila fursa inayojitokeza, kwa hiyo tutaenda kuangalia kuona kama inafaa, basi tutafanya hivyo.