Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE ( K.n.y MHE. JOHN P. KADUTU) aliuliza:- Kumekuwa na maombi ya kupata Wilaya na Halmashauri ya Ulyankulu kwa muda mrefu sasa. Pia zimetolewa ahadi za kuunda Wilaya na Halmashauri tangu mwaka 2010. (a) Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi Wilaya na Halmashauri kwani vigezo vya kuwa Wilaya/Halmashauri ni kama vile vya Jimbo ambavyo tayari vimetimia? (b) Je, ni kikwazo gani kimesababisha kutopata Wilaya/Halmashauri mpaka sasa?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la Mheshimiwa Kadutu la Ulyankulu linafanana kabisa na Tarafa ya Mima ambayo imeshatangazwa kwamba imeanzishwa kuwa Tarafa ya Mima, lakini mpaka sasa hakuna majengo, hakuna watumishi. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini mtajenga majengo, mtaleta watumishi ili kweli ile Tarafa ya Mima ianze kufanya kazi mara moja maana sasa inatamkwa tu Tarafa ya Mima?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Kata za Matomondo pamoja na Mlembule ni kata kubwa sana na zina vigezo vyote kuwa tarafa, je, Mheshimiwa Naibu Waziri, unasemaje kuhusu hili? Ni lini mtaanzisha Tarafa hizi Kata mbili, Mlembule na Matomonda?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Senior MP Mheshimiwa Lubeleje ambaye mimi namuita grader la zamani makali yale yale kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika Tarafa ya Mima ambayo kwa mujibu wa utaratibu Mheshimiwa amesema kwamba imeshaanzishwa lakini majengo ni bado. Basi mimi naomba nielekeze katika Halmashauri husika kwa sababu nadhani wakati tunafanya mchakato wa kuanzisha tarafa hizi ni lazima tutakuwa tumejipanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nafahamu kwamba unafanya juhudi kubwa, lakini niwasihi wenzetu kule, kwa sasa hivi iangalie namna ya kufanya katika mipango ile ikiwezekana ya Kihalmashauri na Kiwilaya. Katika maana hiyo tuanze michakato ya kuanzisha majengo kwa kuangalia suala zima la ki-bajeti. Jambo hili linaanzia kule kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo wakati wa mchakato wa bajeti na sisi tutaunga mkono suala la watumishi; ambayo ndiyo mamlaka yetu kupeleka watumishi kama Serikali. Nikuhakikishie Mheshimiwa Lubeleje kwamba jambo hili tutalifanya kwa kadiri taratibu za Serikali zinavyokwenda sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuanzishwa tarafa mpya katika Kata ya Matomondo na. Najua kwamba michakato hii iko vile vile kwa mujibu wa Sheria za uanzishwaji wake. Kwa sababu hiyo basi nishauri Baraza la Madiwani kwamba jambo hili likionekana linakidhi sasa katika Halmashauri yetu ya Mpwapwa basi liweze kufanyika katika ile michakato ya kimsingi ambayo inaanzia katika vijiji inakuja katika vikao vya Ward C, na Halmashauri ya Wilaya then DCC ya wilaya na Mkoa, baadaye inakuja Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kwa maamuzi zaidi.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Lubeleje naomba nikuhakikishie kwamba mkianza mchakato huo Ofisi ya Rais TAMISEMI itasikiliza kilio chenu na kuweza kukifanyia kazi kwa kadri inavyoona inafaa.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE ( K.n.y MHE. JOHN P. KADUTU) aliuliza:- Kumekuwa na maombi ya kupata Wilaya na Halmashauri ya Ulyankulu kwa muda mrefu sasa. Pia zimetolewa ahadi za kuunda Wilaya na Halmashauri tangu mwaka 2010. (a) Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi Wilaya na Halmashauri kwani vigezo vya kuwa Wilaya/Halmashauri ni kama vile vya Jimbo ambavyo tayari vimetimia? (b) Je, ni kikwazo gani kimesababisha kutopata Wilaya/Halmashauri mpaka sasa?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mchakato wa uanzishwaji wilaya ni wa muda mrefu na hili swali sasa ni la mara nyingi tunauliza; kwa kuwa Ulyankulu ilikuwa na makazi ya wakimbizi, na ambao wapo mpaka sasa, na kwamba vile vile wapo wakimbizi ambao wamepewa uraia na kusababisha kuongezeka kwa idadi ya watu na kuwa na watu wengi.
Je, Serikali haioni hilo? je, ni lini sasa inaweza ikaamua kwa maksudi kuhakikisha kwamba wilaya ile sasa inakuwepo baada ya kukamilisha vigezo vyote tulivyovileta. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema pale awali, mapendekezo ya kwanza yalivyokuja ikaonekana kuna mapungufu ya idadi ya watu, hii ndiyo iliyokuwa miongoni mwa vigezo ambavyo vilifanya isi-qualify kipindi kile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge amekiri hapa kwamba kuna baadhi ya makazi ya wakimbizi, nadhani takriban kata tatu, zimesababisha kuwepo kwa sasa idadi kubwa sana ya watu katika maeneo hayo ambayo sasa wamesajiliwa kuwa kama raia wa Tanzania. Hata hivyo utaratibu ni ule ule kwa sababu lile jambo la mwanzo lilidondoka haliku--qualify. Kwamba kama tunaona idadi sasa hivi inatosha twende na michakato ile ile kama nilivyosema awali, kwamba ipitishwe katika vikao vya kisheria ambavyo katika Ward C, DCC pamoja na RCC.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vikifika kwetu sisi, tutawatuma wataalam kuja kufanya verification, iki-qualify biashara imekwisha. Kwa hiyo mama Mwanne Mchemba naomba nikutoe shaka katika hilo, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) itasikiliza jambo hili na kwa kupitia document zote zilizotumwa kutoka kwenu tutalifanyia kazi jambo hili. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE ( K.n.y MHE. JOHN P. KADUTU) aliuliza:- Kumekuwa na maombi ya kupata Wilaya na Halmashauri ya Ulyankulu kwa muda mrefu sasa. Pia zimetolewa ahadi za kuunda Wilaya na Halmashauri tangu mwaka 2010. (a) Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi Wilaya na Halmashauri kwani vigezo vya kuwa Wilaya/Halmashauri ni kama vile vya Jimbo ambavyo tayari vimetimia? (b) Je, ni kikwazo gani kimesababisha kutopata Wilaya/Halmashauri mpaka sasa?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yaliyopo huko Wilaya ya Ulyankulu yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko katika Jimbo langu la Manyoni Magharibi. Jimbo la Manyoni Magharibi ni Tarafa ya Itigi ambayo ina upana mkubwa, eneo moja mpaka eneo lingine ni kilometa 219, ni jimbo kubwa kuliko majimbo mengi. Tumeshapeleka na kupitia taratibu zote hadi RCC kuiombea Itigi kuwa Wilaya lakini hadi leo Serikali imekuwa kimya. Je, Serikali inasema nini kuhusu jambo hili la Wilaya ya Itigi? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli. Kwanza awali hata hili eneo la Itigi tulikuwa hatujapata Halmashauri kamili na ndiyo maana mchakato wa kwanza ulikuwa ni kupata Halmashauri. Suala hili najua Mheshimiwa Massare umelizungumza mara nyingi tangu uchaguliwe kuwa Mbunge. Naomba nikuhakikishie kwamba tutafanya verification katika ofisi yetu kuona hizi document ziko katika process gani. Kama hali haijawa sawa sawa tutatoa maelekezo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kwamba ikamilishe zile taratibu ningine zote ambazo zitakuwa zimepungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nakumbuka kwamba Mheshimiwa Mbunge tulifika pale Itigi na kweli ukiangalia jiografia hata aliyekuwa Mkuu wa Wilaya wa kule ambaye sasa hivi ndiye Mkurugenzi wetu Mkuu wa TIC alikuwa anapata changamoto kubwa sana kui-manage ile Wilaya ya Manyoni. Kwa hiyo, Mheshimiwa Massare naomba nikuhakikishie kwamba mambo haya yote yakikamilika, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) itakapojiridhisha, haitasita kufanya maamuzi kwa maslahi mapana ya eneo lako husika.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE ( K.n.y MHE. JOHN P. KADUTU) aliuliza:- Kumekuwa na maombi ya kupata Wilaya na Halmashauri ya Ulyankulu kwa muda mrefu sasa. Pia zimetolewa ahadi za kuunda Wilaya na Halmashauri tangu mwaka 2010. (a) Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi Wilaya na Halmashauri kwani vigezo vya kuwa Wilaya/Halmashauri ni kama vile vya Jimbo ambavyo tayari vimetimia? (b) Je, ni kikwazo gani kimesababisha kutopata Wilaya/Halmashauri mpaka sasa?

Supplementary Question 4

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa nia kubwa ya kugawa maeneo ni kusogeza huduma kwa wananchi na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri baada ya sisi wananchi wa Kilolo kupige kelele kutokana na ukubwa wa Wilaya yetu, uliridhia na kutupa Halmashauri ya Mji Mdogo sasa ni muda mrefu na ulifika na kuona kwamba sasa tunastahili kupata Halmashauri kamili. Je, ni lini sasa Mheshimiwa? Hebu tupe jibu ili wananchi wakusikie.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli. Mwaka jana tulikwenda na Mbunge tukafika mpaka jimbo lake, tukatembea. Kijiografia jimbo lile ni kubwa sana, linapakana na ndugu yangu Profesa Jay, linapakana na Waziri wangu Simbachawene huku Kibwakwe, ni jimbo ambalo liko tata kweli kweli. Hata hivyo tulivyofika pale Ilula tumekutana na wananchi wa Ilula ambao mapendekezo yao yametufikia, na bahati nzuri baada ya ile ziara nikatuma timu kwenda kufanya verification.
Mheshimiwa Mwenyekiti, verification imeshafanyika na hivi sasa tuko katika mchakato wa kufanya maamuzi ambapo kwa jambo hili mwenye kufanya maamuzi ni Mheshimiwa Rais mwenyewe mwenye dhamana katika eneo hilo, atakaporidhia basi Mheshimiwa Mwamoto naomba usiwe na hofu, ni kweli Serikali imefanya process zote na sasa tuko katika final stage katika kufanya maamuzi. (Makofi)

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE ( K.n.y MHE. JOHN P. KADUTU) aliuliza:- Kumekuwa na maombi ya kupata Wilaya na Halmashauri ya Ulyankulu kwa muda mrefu sasa. Pia zimetolewa ahadi za kuunda Wilaya na Halmashauri tangu mwaka 2010. (a) Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi Wilaya na Halmashauri kwani vigezo vya kuwa Wilaya/Halmashauri ni kama vile vya Jimbo ambavyo tayari vimetimia? (b) Je, ni kikwazo gani kimesababisha kutopata Wilaya/Halmashauri mpaka sasa?

Supplementary Question 5

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Arumeru ina Halmashauri mbili kwa maana kwamba Halmashauri ya Meru na Arusha DC. Wilaya hii eneo lake ni kubwa kiasi kwamba hata wakati mwingine huduma kuzifikia jamii inakuwa ni vigumu. Je, ni lini sasa Serikali (kwa sababu tayari ilikwishaanza mchakato siku za nyuma) itaendelea na mchakato huo kuhakikisha kwamba inagawanya wilaya hii inakuwa wilaya mbili ili huduma za kijamii ziweze kuwafikia wananchi kwa haraka? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la dada yangu Amina Mollel Mbunge ambaye anawakilisha hasa kundi la walemavu kwa umakini zaidi humu Bungeni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Wilaya ya Meru ni kubwa sana, ina Arusha DC na Meru. Ukiangalia, bahati mbaya Halmashauri ile iko kama mbalamwezi fulani hivi, kwamba Jiji la Arusha liko katikati halafu ile wilaya imezunguka hivi. Kwa hiyo hata management yake inakuwa ni ngumu zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili kama nilivyosema katika maeneo mbalimbali, kwanza naamini michakato mbalimbali imeanza huko lakini wakati mwingine inawezekana taarifa zikawa zimekuja lakini vigezo havikukidhi. Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge Amina Mollel kwamba tutakapopata taarifa za vikao vya RCC kutoka Mkoa wa Arusha na Mkuu wetu wa Arusha akishajipima kule akiona kwamba jambo hilo limeridhia, na likishafika kwetu na sisi tutalifanyia kazi kufanya taratibu zote za kisheria zinazohitajika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikionekana kwamba inafaa sasa kuigawanya zile wilaya mbili, Serikali itaona jinsi gani ya kufanya katika hilo. Kwa hiyo naomba nikuhakikishie, ni kwamba utaratibu ni ule ule wa kisheria tu, kama unavyosema ugawanyaji wote wa maeneo unasemaje. Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana wa eneo hilo akiridhia, basi mchakato utakamilika hatimaye mtapata wilaya mpya.