Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:- Wilaya ya Muheza imetenga eneo sehemu ya Chatur kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za NHC za bei nafuu na baadae kuuziwa wananchi na NHC walishalipia eneo hilo. Je, ni lini ujenzi huo utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nilikuwa na mambo mawili. Kwanza ni swali na pili ni ushauri.
Mheshimiwa Mwenyekii, ni kweli kabisa watalaam walikuja Muheza na walikwenda wakaangalia hiyo sehemu na Wana Muheza waliahamasika sana baada ya kuwaona watalaam hao. Hata hivyo tangu watalaam hao wamendoka nafikiri mwezi mmoja au miwli iliyopita bado hawajarudi. Sasa nilitaka kujua, ni lini watalaam hao watarudi tena na ujenzi wa hizi nyumba utaanza?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ambalo naona kama ni ushauri; ni kwamba eneo ambalo linajengwa ni eneo la Chatur sehemu ya Kibanda, Kata ya Kilulu na lina ekari 83. Sasa nyumba ambazo zimeshawekeana saini ni nyumba 20, kwa hiyo ina maana kwamba kuna eneo kubwa ambalo litabaki. Ni ushauri tu kwamba ni kwa nini sasa hivi Shirika la Nyumba lisianze marketing kushawishi wana Muheza waanze kulipia kwenye hizo nyumba ambazo zitajengwa ili eneo lote la ekari 83 liweze kutumika ipasavyo? Pamoja na hayo, ni vizuri wakati marketing hiyo inafanyika basi na watu wa benki wanakuwepo ili kuweza kutoa mikopo kwa wananchi wa Muheza. Nakushukuru sana.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anauliza ni lini watalaam hawa watarudi tena na ujenzi uanze kuanza. Naomba nimwambie tu kwamba tatizo ambalo limefanya wasianze mapema ni kwa sababu mpango wa matumizi ya eneo lile awali watu wa Muheza walipanga kama eneo la matumizi ya umma, kwa maana walikuwa wamekusudia kuweka stand pale. Sasa unapobadilisha kupeleka kwenye kujenga makazi inabidi mchakato wa kubadili matumizi ya eneo lile ufanyike. Kinachofanyika sasa ni kubatilisha ili litoke kwenye matumizi ya umma na liende kwenye eneo la makazi, wakikamilisha wataanza kazi hiyo.
Swali la pili, anasema marketing ianze kufanyika kwa ajili ya zile nyumba 10 ziweze kununuliwa. Napenda nimhakikishie tu Mheshimiwa Balozi Adadi kwamba tayari wanunuzi wameshaanza kujitokeza, wanachosubiri ni kuona nini kinafanyika pale. Kwa wazo lake la kusema mabenki wasogee nadhani hilo tunalichukua na ni kawaida ya National Housing wanafanyakazi sambamba na mabenki katika zoezi zima la uendelezaji miliki.