Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA (K.n.y. MHE. CATHERINE MAGIGE) aliuliza:- Serikali ilishatoa ahadi ya kujenga barabara ya Mto wa Mbu hadi Loliondo kwa kiwango cha lami. Je, mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani na ujenzi wake utaanza lini?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Mheshimiwa Waziri Mkuu katika ziara yake Wilayani Ngorongoro mwaka jana aliahidi nyongeza ya kilometa 50 kwenye ujenzi wa barabara unaoendelea. Je, ahadi hii itatekelezwa lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Ilani ya CCM ya mwaka 2015 – 2020 imeainisha ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 65 kutoka Sanya Juu hadi Longido; ni lini ujenzi wa barabara hii utaanza?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwapongeze sana Wabunge wa Chama cha Mapinduzi waliopo Mkoa wa Arusha, ninatambua juhudi nyingi wanazozifanya ili kuhakikisha miundombinu ya barabara katika mkoa inaimarika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nampongeza sana Mheshimiwa Olenasha kwa sababu amefuatilia barabara hii ya Loliondo – Mto wa Mbu, na mimi niseme tu kwamba tutaendelea kuhakikisha kwamba barabara zinajengwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Mheshimiwa Waziri Mkuu alitembelea Loliondo na aliahidi ujenzi wa barabara ya nyongeza kwa kilometa 50, kwa hiyo nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili tunalishughulikia na tunaangalia kadri itakavyowezekana katika bajeti hii inayokuja nyongeza ya hii barabara tutaendelea kujenga. Kwa sababu barabara hii inayo urefu wa kilometa 218 kwa hiyo karibu asilimia 25 sasa barabara hii inajengwa, sasa tukiendelea kuongeza tutapata asilimia 50 na hatimaye barabara hii itakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, barabara hii ya Sanya Juu hadi Longido imetamkwa katika Ilai ya Uchaguzi, na niwahakikishie tu Waheshimiwa Wabunge na Bunge lako Tukufu kwamba tunaendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi na tuna kipindi cha miaka mitano nah ii barabara tutaitazama katika bajeti zinzaokuja ili tuhakikishe ahadi za Chama cha Mapinduzi na tuna kipindi cha miaka mitano nah ii barabara tutaitazama katika bajeti zinazokuja ili tuhakikishe ahadi za Chama cha Mapinduzi zinatekelezwa kikamilifu. Ahsante. (Makofi)

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA (K.n.y. MHE. CATHERINE MAGIGE) aliuliza:- Serikali ilishatoa ahadi ya kujenga barabara ya Mto wa Mbu hadi Loliondo kwa kiwango cha lami. Je, mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani na ujenzi wake utaanza lini?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nchi yetu ya Tanzania kuna baadhi ya barabara za lami zimejengwa chini ya kiwango, kwa mfano barabara ya Chalinze hadi Mlandizi.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweza kuzikarabati barabara hizi?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J.KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu barabara hii imekuwa ni barabara ya siku nyingi, barabara hii ilijengwa kwa kiwango kizuri, lakini kwa sababu haikudumu kwa muda mrefu na matumizi ya barabara yameongezeka kwa maana ya kupitisha magari mengi na mizigo, kwa hiyo barabara imechakaa. Serikali inao mpango wa kuifanyia matengenezo makubwa barabara hii ili iweze kuwa imara zaidi.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA (K.n.y. MHE. CATHERINE MAGIGE) aliuliza:- Serikali ilishatoa ahadi ya kujenga barabara ya Mto wa Mbu hadi Loliondo kwa kiwango cha lami. Je, mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani na ujenzi wake utaanza lini?

Supplementary Question 3

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kibena – Lupembe – Madeke, kilometa 126 ni barabara pekee ambayo inaunganisha Mkoa wa Njombe na Mkoa wa Morogoro kupitia Mlimba. Barabara hii mwaka wa fedha 2016/2017 ilitengewa fedha, mwaka 2017/2018 ilitengewa fedha lakini mpaka leo hii haijaanza kujengwa kwa kiwango cha lami.
Nataka kupata kauli ya Serikali, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuweza kuokoa uchumi unaopotea kule Lupembe na Mkoa mzima wa Njombe kwa ujumla?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J.KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Hongoli kwa sababu amekuwa akiifuatilia sana hii barabara, na hii barabara ni muhimu sana inapita sehemu ambazo zina uzalishaji mkubwa lakini pia ni kiungo kikubwa cha wananchi wa Njombe na wananchi wa Morogoro, na tumezungumza juu ya ujenzi wa hiyo barabara, barabara hii imeshasanifiwa. Kwa hiyo niseme ujenzi wa kiwango cha lami umeshaanza kwa sababu baada ya usanifu wa barabara hizo ndiyo harakati za kuanza ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge, kwa vile barabara hii ilikuwa imetengewa fedha na Serikali ilikuwa inaendelea kupata fedha mara tu fedha zikipatikana ujenzi wa barabara hii utaanza mara moja. Naomba tu Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa Njombe wawe na matumaini, wawe na imani na Serikali, inatafuta fedha na itaendelea kujenga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na niliambie tu Bunge lako Tukufu kwamba kila mwezi tunatumia fedah nyingi sana kulipa certificates zinazotoka, takribani bilioni 80 zinalipwa kila mwezi, kwa hiyo hii ni ushuhuda kwamba Serikali inafanya kazi kubwa kuhakikisha kila wakati, kila siku barabara tunaendelea kuziboresha na kuzijenga. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA (K.n.y. MHE. CATHERINE MAGIGE) aliuliza:- Serikali ilishatoa ahadi ya kujenga barabara ya Mto wa Mbu hadi Loliondo kwa kiwango cha lami. Je, mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani na ujenzi wake utaanza lini?

Supplementary Question 4

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Lushoto kwenda Mlalo, lakini pia kutoka Mlalo kwenda Bombo Mtoni hadi Maramba ni ya muda mrefu sana na inakuwa inajengwa kwa kiwango cha kilometa mbili mbili kila mwaka. Je, ni lini sasa Serikali itaweka nguvu ili barabara hii ya kutoka Lushoto - Mlalo na kutoka Mlalo kwenda mpaka Maramba ijengwe kwa kiwango cha lami?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J.KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Shangazi amekuwa akifuatilia sana barabara pamoja na maendeleo mbalimbali katika Jimbo la Lushoto. Ninatambua mahitaji ya barabara katika maeneo haya ambayo ameyataja maeneo ya kiunganishi cha Lushoto - Mlalo na ile barabara ya Mlalo kupita Maramba kwenda Mkinga na Mheshimiwa Kitandula amekuwa akifuatilia hii.
Kwa hiyo, kama nilivyojibu pale awali kwamba tunaendelea kutafuta fedha kama Serikali inavyokusanya fedha vizuri tutaendelea kujenga barabara mbalimbali. Kwa hiyo, niwaombe tu wananchi wa Mlalo, Maramba Mkinga na wananchi wa Lushoto kwa ujumla na watanzania wote kwamba waendelee kuvuta subira tu kadri fedha zinavyopatikana tutaendelea kuboresha barabara zote nchini ili ziweze kutoa mchango mkubwa katika ujenzi wa uchumi wa nchi yetu.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA (K.n.y. MHE. CATHERINE MAGIGE) aliuliza:- Serikali ilishatoa ahadi ya kujenga barabara ya Mto wa Mbu hadi Loliondo kwa kiwango cha lami. Je, mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani na ujenzi wake utaanza lini?

Supplementary Question 5

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wilaya ya Mbozi ambayo ni Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe inapakana na Wilaya ya Songwe lakini Wilaya hizi mbili hazijaunganishwa kwa barabara na hivyo wananchi wa Wilaya ya Songwe hulazimika kupita Mkoa mwingine wa Mbeya kupitia njia ya Mbalizi kwenda Makao Makuu ya Mkoa ambayo yako Mbozi.
Naomba sasa kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini Wilaya ya bozi na Wilaya ya Songwe zitaunganishwa kwa barabara ili kuwasaidia wananchi wa maeneo haya yote mawili kuweza kurahisisha mawasiliano?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J.KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge nikupongeze tu kwa kufuatilia na unajua umuhimu wa barabara ina mchango mkubwa sana kwenye maendeleo. Kwa vile sijapata fursa ya kutembelea wa Mbeya mimi napenda tu nilichukue hili ni jambo la kufanyia kazi na mimi nitatembelea Mbeya ili niweze kufika maeneo haya ili tuweze kushauriana vizuri na Mheshimiwa Mbunge wakati Serikali inafanya harakati za kufanya makusanyo na kuboresha barabara nchini. (Makofi)

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA (K.n.y. MHE. CATHERINE MAGIGE) aliuliza:- Serikali ilishatoa ahadi ya kujenga barabara ya Mto wa Mbu hadi Loliondo kwa kiwango cha lami. Je, mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani na ujenzi wake utaanza lini?

Supplementary Question 6

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza niipongeze Serikali kwa majibu yake mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la Mto wa Mbu lina linalingana kabisa na tatizo la Mji wa Mombo. Mji wa Mombo toka Awamu ya Nne ulihaidiwa na Serikali kwamba utajengwa kiwango cha lami kilometa moja na nusu, na wataalam walienda pale wakapima na wakachukua sample ya udongo, lakini cha kushangaza mpaka leo hii barabara hile ya Mji Mdogo wa Mombo haijafanyiwa utafiti wala haijafanyiwa chochote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini tamko la Serikali kuhusiana na Mji Mdogo wa Mombo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J.KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi kwamba amekuwa akilifuatilia suala hili na tumezungumza naye. Nitumie tu nafasi hii nimuelekeze Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tanga ili aweze kuharakisha zoezi la kusanifu eneo hili ili sasa tuweze kujenga na kuboresha kama ilivyo kwenye ahadi, ahsante sana. (Makofi)