Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa mipaka katika Pori la Hifadhi ya North Ugala, Wilayani Urambo, Kata ya Nsenda, Kijiji cha Kangome, Kitongoji cha Lunyeta. Mgogoro huo umesababishwa na mipaka mipya iliyowekwa na hivyo kusababisha upungufu wa eneo la shughuli za kilimo na ufugaji. (a) Je, Serikali inafahamu kuwepo wa mipaka ya zamani ambayo haikuzingatiwa wakati wa kuweka mipaka mipya? (b) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mipaka ili wananchi wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba amejibu swali ambalo yeye mwenyewe alifika Urambo na kujionea kwamba mpaka uliowekwa na Serikali upo, beacon zilizowekwa na Serikali zipo, lakini cha kushangaza ni kwamba wananchi waliondolewa kwenye eneo ambalo lina mpaka halali wa Serikali. Kwa hiyo, kuwaondoa wananchi kwangu mimi naona ni kwamba hawakutendewa haki kwa sababu waliidhinishwa na mpaka wa Serikali uliokuwepo. Kwa hiyo, kuwaondoa ni kwamba kumewapunguzia eneo lao la kilimo na la ufugaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri ulijionea wewe mwenyewe, je, upo tayari kurudi tena na mimi tukakae na wale wananchi tuondoe huu mgogoro ili wananchi waendelee kutumia maeneo yao waliyoyazoea ambayo sasa hivi tunawapa umaskini kutokana na kuwapunguzia eneo la kulima? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Pori la Hifadhi ya North Ugala lina maeneo mengi ya migogoro ya aina hiyo hiyo kutokana na kubadilishiwa mpaka wa awali na kuwawekea wa pili ambao umesababisha upungufu. Sasa swali langu, je, upo tayari kutenga muda wa kutosha tukakae mimi na wewe muda mrefu hasa Urambo umalize migogoro yote katika mpaka huo wa msitu? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana mheshimiwa Mbunge Margaret Simwanza Sitta kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akifanya katika kuwatetea wananchi wake wa Urambo. Kwa kweli anafanya kazi nzuri sana na ni mwanamke wa Jimbo ambaye kwa kweli anaonyesha mfano wa kuigwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilishawahi kutembelea katika hili eneo na nilijionea hali yenyewe na tulikaa na wananchi tukatoa elimu tukaelimishana vizuri kabisa na niombe kusema kwamba nipo tayari kurudi tena kwenye eneo lile ili twende pamoja, tuambatane na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na ambao ndio wenye dhamana ya kuthibitisha mipaka. Tukakae na Wizara ya Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii na wananchi ili tupitie hatua kwa hatua kuweza kumaliza migogoro ambayo ipo katika eneo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili, nipo tayari pia kutenga muda wa kutosha kabisa kuhakikisha tunapitia miogoro yote ambayo ipo katika Jimbo hilo. (Makofi)

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa mipaka katika Pori la Hifadhi ya North Ugala, Wilayani Urambo, Kata ya Nsenda, Kijiji cha Kangome, Kitongoji cha Lunyeta. Mgogoro huo umesababishwa na mipaka mipya iliyowekwa na hivyo kusababisha upungufu wa eneo la shughuli za kilimo na ufugaji. (a) Je, Serikali inafahamu kuwepo wa mipaka ya zamani ambayo haikuzingatiwa wakati wa kuweka mipaka mipya? (b) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mipaka ili wananchi wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwanza nianze kuwapa pole wananchi wa Kilolo ambao wameunguliwa na shule ya wazazi kule Ukumbi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niulize swali langu moja, kwa kuwa wananchi wa Kilolo moja ya zao kubwa wanalolitegemea ni misitu, tumehamasisha na inasaidia kutunza mazingira. Pia kwa njia ya misitu wanapata mbao ambazo zimesaidia kwa kiwango kikubwa sana kujenga majengo ambayo yamesababisha ofisi nyingi kuhamia Dodoma haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa ambalo lipo sasa ni kwamba wale wananchi wameanza kunyanyasika kusafirisha mbao, watu wa TFS (Wakala wa Misitu) wanawasumbua, TRA wanawasumbua kiasi kwamba wananchi sasa wako tayari kuacha kupasua mbao. Je, Mheshimiwa Waziri utakuwa tayari kwenda kukaa na watu wa TRA kule ili tatizo hili liishe na wananchi wa Kilolo waendelee kufanya biashara zao?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa zao la misitu ni la muhimu sana na limekuwa likitoa mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi yetu, na wananchi wa Kilolo ni mojawapo ambao wmaekuwa wakijishughulisha sana na hili zao, kwa kweli hongera sana kwa kuhamasisha jinsi wanavyojishughulisha na hili suala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumeweka utaratibu kwamba mwananchi yeyote mwenye misitu ambaye anataka kujishughulisha na hili zao lazima apate kibali kutoka kwa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) pamoja na TRA ili ahakikishe kwamba anasafirisha kwa kufuata utaratibu. Na niombe tu kusema kwamba niko tayari kwenda kukaa na TRA pamoja na TFS kuhakikisha kwamba utaratibu mzima unafuatwa pale ambapo wananchi wa Kilolo wanataka kusafirisha mbazo zao.

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa mipaka katika Pori la Hifadhi ya North Ugala, Wilayani Urambo, Kata ya Nsenda, Kijiji cha Kangome, Kitongoji cha Lunyeta. Mgogoro huo umesababishwa na mipaka mipya iliyowekwa na hivyo kusababisha upungufu wa eneo la shughuli za kilimo na ufugaji. (a) Je, Serikali inafahamu kuwepo wa mipaka ya zamani ambayo haikuzingatiwa wakati wa kuweka mipaka mipya? (b) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mipaka ili wananchi wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 3

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la kukosekana kwa mipaka limeendelea kuleta migogoro na kuwaumiza wananchi wengi hapa nchini. Tatizo hilo limeendelea kuwaumiza wananchi wa Mtaa wa CCT Mkundi pale Manispaa ya Morogoro ambao wamevunjiwa nyumba zao, takribani miaka miwili imepita baada ya kuambiwa kwamba wamejenga kwenye Hifadhi ya Msitu wa Kundi. Hata hivyo wananchi wale walikuwa na vibali halali na walipewa ramani zote na mji kujenga nyumba zao. Je, Serikali ipo tayari kuwalipa fidia wananchi hawa wa Mtaa wa CCT Mkundi?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kulikuwa na matatizo katika msitu wetu ule wa Mkundi ambapo wananchi wengi walikuwa wameondolewa kwa sababu walikuwa wamevamia katika maeneo haya. Kama nilivyokuwa nimesema, hata jana ambapo tumekuwa tukitoa maelezo kwa muda mrefu, kwamba yapo maeneo ambayo yalikuwa yamepimwa katika hifadhi za Taifa, maeneo ni mengi, na jana nilisema kwamba vijiji takribani 366 vimepimwa kwenye hifadhi za misitu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili eneo pia wananchi hawa kweli walikuwa wamepewa katika hayo maeneo lakini tulipogundua kwamba wamepewa kimakosa ndiyo maana jitihada zikafanyika katika kuwaondoa.
Kuhusu fidia, kwa sababu taratibu zilikuwa zimekiukwa, kwa kweli Wizara tutaangalia kama kweli wanaweza waka-qualify kupata fidia, lakini tunaamini kabisa kwamba kama walivamia na kama Serikali hawakupewa kihalali kwa kupitia, kwa sababu ule ni msitu, basi fidia inaweza isitolewe, lakini kama tutakuta kwamba waliondolewa kimakosa basi tutalitafakari na kuona namna bora ambavyo tunaweza tukalitatua hilo tatizo la wananchi wake.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa mipaka katika Pori la Hifadhi ya North Ugala, Wilayani Urambo, Kata ya Nsenda, Kijiji cha Kangome, Kitongoji cha Lunyeta. Mgogoro huo umesababishwa na mipaka mipya iliyowekwa na hivyo kusababisha upungufu wa eneo la shughuli za kilimo na ufugaji. (a) Je, Serikali inafahamu kuwepo wa mipaka ya zamani ambayo haikuzingatiwa wakati wa kuweka mipaka mipya? (b) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mipaka ili wananchi wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 4

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nipate kuuliza swali dogo tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi ndani ya Bunge kwamba ingeweza kumaliza migogoro ya wananchi na mapori ya hifadhi mwezi Desemba mwaka jana. Moja kati ya maeneo ambayo yanakabiliwa na mgogoro mkubwa sana ni pamoja na eneo la Swagaswaga katika Wilaya ya Chemba ambako wananchi wamekuwa wakifukuzana na askari wanyamapori kila siku.
Ningeomba kauli ya Serikali, pamoja na kwamba Mheshimiwa Waziri anajiandaa kwenda Urambo, hapa Chemba ni karibu sana, yuko tayari kwenda Chemba pale kabla ya kwenda Urambo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu katika Pori letu la Swagaswaga na ninaomba nimjibu tu kwamba hivi sasa ninavyoongea, Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii leo hii ameenda kutembelea hilo pori pamoja na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango kwa ajili ya kuangalia huo mgogoro ili waweze kulitatua hili tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa mipaka katika Pori la Hifadhi ya North Ugala, Wilayani Urambo, Kata ya Nsenda, Kijiji cha Kangome, Kitongoji cha Lunyeta. Mgogoro huo umesababishwa na mipaka mipya iliyowekwa na hivyo kusababisha upungufu wa eneo la shughuli za kilimo na ufugaji. (a) Je, Serikali inafahamu kuwepo wa mipaka ya zamani ambayo haikuzingatiwa wakati wa kuweka mipaka mipya? (b) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mipaka ili wananchi wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 5

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mgogoro wa misitu na wananchi wa Jimbo la Ukonga Kata ya Vingiziwa, Chanika, Buyuni na Pugu tangu mwaka 1998, mgogoro huu Mheshimiwa Waziri Mkuu anaufahamu, wameshaunda timu huko nyuma.
Ninaomba nipate kauli ya Serikali leo; mgogoro huu unafikia lini mwisho ili wananchi wale wajue kwamba wanaendelea kuishi kwa kufanya maendeleo au wanaondoka na wanakwenda wapi? Naomba nipate majibu hayo.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwepo na mgogoro wa muda mrefu katika msitu ule na mimi mwenyewe katika kipindi cha hivi karibuni nimetoka kule nimetembelea mipaka ile na kuangalia, lakini naomba nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba hatua zilichukuliwa na Serikali katika kuwaondoa wananchi wote waliokuwa wamevamia katika yale maeneo na mipaka rasmi imechorwa pamoja na kuweka barabara pembezoni ya mpaka. Kwa hiyo, wananchi wale wote ambao wako ndani wameshaondolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini yapo maeneo machache ambayo yamebaki ambayo sasa Mheshimiwa Waitara alisema kwamba bado inabidi tukae nao chini na mimi nakubali kwamba baada ya Bunge hili leo hii ntaomba tukutane ili tukae pamoja ili tuweze kutoa tamko la mwisho juu ya wale watu ambao wako katika haya maeneo yaliyobaki.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa mipaka katika Pori la Hifadhi ya North Ugala, Wilayani Urambo, Kata ya Nsenda, Kijiji cha Kangome, Kitongoji cha Lunyeta. Mgogoro huo umesababishwa na mipaka mipya iliyowekwa na hivyo kusababisha upungufu wa eneo la shughuli za kilimo na ufugaji. (a) Je, Serikali inafahamu kuwepo wa mipaka ya zamani ambayo haikuzingatiwa wakati wa kuweka mipaka mipya? (b) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mipaka ili wananchi wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 6

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chanzo cha migogoro hii pia kinatokana na hifadhi ambazo zinatolewa bila utaratibu, tunajua mpaka eneo litangazwe kuwa hifadhi kuna utaratibu ambao unatakiwa kufuatwa. Hivi karibuni kumekuwa na utaratibu wa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kushirikiana na halmashauri kuwaondoa wananchi na kusema maeneo fulani ni hifadhi na wakijua kabisa maeneo hayo hayajatangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
Nini tamko la Serikali juu ya Halmashauri ambazo zinaondoa wananchi hao na ikiangalia kabisa hawajafuata taratibu na sheria za nchi yetu? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hifadhi za misitu kuna misitu ambayo inasimamiwa na Serikali Kuu, kuna misitu inayosimamiwa na TAMISEMI na kuna misitu inayosimamiwa na Serikali za Vijiji. Kwa hiyo, kama vijiji vimetenga kwamba maeneo hayo ni ya hifadhi basi mamlaka zinazohusika zina wajibu wa kuhakikisha kwamba wananchi hawavamii katika hayo maeneo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo basi, mimi naamini kabisa Wakuu wa Wilaya wamechukua hatua kutokana na maamuzi yaliyokuwa yamefanywa na Halmashauri zinazohusika. Kama kuna maeneo ambayo wananchi wameondolewa bila kufuata taratibu basi ntaomba Mheshimiwa Mbunge anipe hayo maeneo ili tuone na tutafakari ni hatua zipi zilistahili kuchukuliwa. (Makofi)

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa mipaka katika Pori la Hifadhi ya North Ugala, Wilayani Urambo, Kata ya Nsenda, Kijiji cha Kangome, Kitongoji cha Lunyeta. Mgogoro huo umesababishwa na mipaka mipya iliyowekwa na hivyo kusababisha upungufu wa eneo la shughuli za kilimo na ufugaji. (a) Je, Serikali inafahamu kuwepo wa mipaka ya zamani ambayo haikuzingatiwa wakati wa kuweka mipaka mipya? (b) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mipaka ili wananchi wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 7

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa la ardhi katika Wilaya ya Sikonge, Mkoa wa Tabora, eneo kubwa ni eneo la hifadhi kuliko eneo ambalo wanaishi binadamu na inabidi wale wanadamu wafanye kazi kwenye eneo la hifadhi.
Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza eneo la hifadhi na kuwapa wananchi ili waweze kufanya shughuli zao za kibinadamu kuliko ilivyo hivi sasa ambapo wananyanyasika, wanadhalilika na kuteseka? Nakushukuru.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli na mimi naomba niungane naye kusema kwamba Mkoa wa Tabora ni mojawapo ya mikoa ambayo ina sehemu kubwa sana ya Hifadhi ya Taifa, kwa kweli hilo Serikali tunakubali na tumeona kabisa juhudi mbalimbali ambazo zimefanywa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli nchi yetu kama tulivyokuwa tunasema kila siku na tumekuwa tukisema, ardhi haiongezeki, idadi ya watu inazidi kuongezeka, shughuli za kibinadamu zimezidi kuongezeka, mambo mengi yamezidi kuongezeka. Kwa kweli mpango wa kupunguza maeneo ya hifadhi hautatusaidia kutatua matatizo, tatizo linaweza kutatuliwa kwa kuwa na mipango bora ya matumizi ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwa na mipango mizuri ya kutumia ardhi iliyopo hiyo itatusaidia kuliko kupunguza hifadhi. Leo hii tutapunguza kesho idadi ya watu itaongezeka zaidi, je tutazidi kupunguza? Mwisho hifadhi zote zitaisha.
Kwa hiyo hatuna mpango wa kuweza kupunguza bali ni kuwashauri wananchi watumie muda wao vizuri wapangilie vizuri ardhi yao ili ile ambayo ipo kwa ajili ya shughuli za kilimo na makazi itumike kama ambavyo imekusudiwa. (Makofi)