Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Wilaya ya Karagwe ina walimu ambao bado wanadai malimbikizo ya mishahara, walimu hawa hupandishwa madaraja bila ya kurekebishiwa mishahara yao kitu ambacho kimekuwa ni kero kubwa kwa walimu wa Karagwe na maeneo mengine nchini. (a) Je, Serikali inawaambia nini walimu hawa na imefikia wapi kutatua kero zao? (b) Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakikisha Teachers Service Commission (TSC) inapata rasilimali watu na fedha ili iweze kutetea maslahi ya walimu nchini?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza, lakini kabla ya kuuliza maswali haya, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rais na Serikali kwa utaratibu uliowekwa sasa wa kuhakikisha hakuna mwalimu anahama mpaka stahiki zake zinalipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yangu mawili ni kama ifuatavyo; naishukuru Serikali imeongeza annual increment kwa walimu lakini ni lini Serikali itawapandishia mishahara? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa nini walimu wanachukua muda mrefu kupandishwa madaraja? Kuna walimu tangu mwaka 2012 mapaka hivi sasa walitakiwa wawe wamepandishwa zaidi ya mara tatu lakini mpaka sasa walimu hawa hawajapandishwa daraja hata mara moja. Je, ni nini majibu ya Serikali? Nashukuru. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Innocent Bashungwa kwa kazi anazozifanya ikiwemo ushauri wa mara kwa mara anaoutoa kwa Serikali na sisi tunaupokea na pongezi alizotoa kwa Mheshimiwa Rais, tutamfikishia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ameshukuru kuhusu annual increment, sasa ameuliza ni lini Serikali itapandisha mishahara. Utaratibu huu ambao ulikuwa umesimama kwa kipindi kifupi cha miaka kama miwili hivi kupisha uhakiki wa watumishi, zoezi ambalo limefanywa kwa umahiri na weledi mkubwa, baada ya kuwa tumelikamilisha sasa tutaingia kwenye awamu ambayo tutaboresha maslahi ya watumishi ikiwemo mishahara yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu walimu ambao hawajapandishwa daraja kwa muda mrefu. Mimi napenda nikiri kwamba Serikali haijapandisha daraja kuanzia kipindi cha mwaka 2016 hadi 2017, lakini kuanzia mwaka huu wa fedha, matayarisho yanaendelea huko mengi kwa ajili ya kuwapandisha madaraja ikiwemo kuwapandisha wale ambao walistahili kupandishwa tarehe 01 Julai, 2016 na wale ambao walistahili kupandishwa moja mwezi wa saba mwaka 2017 watapandishwa kwa pamoja kwa mserereko. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Wilaya ya Karagwe ina walimu ambao bado wanadai malimbikizo ya mishahara, walimu hawa hupandishwa madaraja bila ya kurekebishiwa mishahara yao kitu ambacho kimekuwa ni kero kubwa kwa walimu wa Karagwe na maeneo mengine nchini. (a) Je, Serikali inawaambia nini walimu hawa na imefikia wapi kutatua kero zao? (b) Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakikisha Teachers Service Commission (TSC) inapata rasilimali watu na fedha ili iweze kutetea maslahi ya walimu nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na changamoto nyingi zilizokuwa zinakabiri kundi hili la walimu, moja ya changamoto kubwa inayokabili kundi la walimu ni mazingira magumu ya kufanyia kazi. Na kwa kuwa hivi sasa Serikali yetu inatekeleza mpango kabambe wa vituo vya afya kwa nchi nzima, je ni kwa nini Serikali isione umuhimu sasa wa kushirikiana na jamii, Halmashauri na Serikali Kuu ili kuona ni namna gani kwa kila Halmashauri katika mwaka wa fedha tunajenga nyumba kadhaa za walimu hasa mazingira yale ya vijijini ili walimu waweze kufanya kazi zao katika mazingira mazuri. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Zacharia Issaay kwa swali lake zuri na ninaomba sasa kumjibu kwamba Serikali inakubaliana kwamba kuna maeneo ambayo kweli yana mazingira magumu hasa maeneo ambayo yapo mbali na Makao Makuu ya Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo hayo yanahitaji mkakati maalum, na kama tulivyoeleza katika mipango mingi ya Serikali, ni kwamba tunaomba sana ushiriki wa jamii katika kuhakikisha kwamba kunakuwa na miundombinu ambayo inavutia walimu waendelee kukaa katika maeneo hayo na miundombinu hiyo ni pamoja na nyumba za walimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili natoa wito kwamba halmashauri zote ziweke kipaumbele kwenye maeneo ambayo yapo mbali zaidi na halmashauri kwa kutenga kwanza fedha/mapato ya ndani kabla hatujapeleka sisi kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya kukamilisha maboma. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Wilaya ya Karagwe ina walimu ambao bado wanadai malimbikizo ya mishahara, walimu hawa hupandishwa madaraja bila ya kurekebishiwa mishahara yao kitu ambacho kimekuwa ni kero kubwa kwa walimu wa Karagwe na maeneo mengine nchini. (a) Je, Serikali inawaambia nini walimu hawa na imefikia wapi kutatua kero zao? (b) Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakikisha Teachers Service Commission (TSC) inapata rasilimali watu na fedha ili iweze kutetea maslahi ya walimu nchini?

Supplementary Question 3

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa madaraka ya Wakuu wa Mikoa ambayo ipo kisheria si kushusha vyeo walimu ambao wamekuwa wakifundisha watoto wetu katika mazingira magumu. Hata hivyo hili limekuwa likijitokeza sasa baadhi ya Wakuu wa Mikoa akiwemo Mkuu wangu wa Mkoa wa Manyara kuwashusha vyeo walimu kwa kisingizo cha kwamba eti wamefelisha wakati watoto wanafeli kwa sababu ya mazingira magumu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nifahamu nini tamko la Serikali juu ya Wakuu hao wa Mikoa akiwemo wa Mkoa wa Manyara ambaye ameshusha Simanjiro, Kiteto na Babati Vijijini na anaendelea na ziara kuendelea kuwashusha walimu vyeo, nini kauli ya Serikali? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo inaeleweka ni kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ndio wasimamizi wakuu wa shughuli zote za Serikali katika Wilaya na Mikoa yao. Kwa hiyo, kama inatokea masuala yanayohusu uzembe au utoro wanayo mamlaka ya kutoa maelekezo kwa mamlaka za nidhamu ambazo ni TSC. Mamlaka ya nidhamu TSC inaanzia katika eneo la shule, shuleni pale Mwalimu Mkuu mwenyewe ni mwakilishi wa TSC. Kwa hiyo, kama yeye mwenye ndio anakuwa anaongoza katika kuonyesha uzembe labda na utoro, hiyo lazima hatua ziweze kuchukuliwa. Lakini mambo mengine ambayo pengine yanaonesha kwamba labda kuna mambo ambayo yamevuka mpaka, tutayafanyia uchunguzi maalumu, ahsante sana.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Wilaya ya Karagwe ina walimu ambao bado wanadai malimbikizo ya mishahara, walimu hawa hupandishwa madaraja bila ya kurekebishiwa mishahara yao kitu ambacho kimekuwa ni kero kubwa kwa walimu wa Karagwe na maeneo mengine nchini. (a) Je, Serikali inawaambia nini walimu hawa na imefikia wapi kutatua kero zao? (b) Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakikisha Teachers Service Commission (TSC) inapata rasilimali watu na fedha ili iweze kutetea maslahi ya walimu nchini?

Supplementary Question 4

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Pamoja na tatizo la malimbikizo ya mishahara ya walimu na kupandishwa madaraja bila kurekebishiwa mishahara yao kuna tatizo kubwa la walimu la muda mrefu ambalo ni ahadi ya Serikali karibu miaka sita sasa kwamba walimu wangepewa posho ya kufundishia yaani teaching allowance. Ni mara kadhaa Serikali imekua na kigugumizi hapa Bungeni na imekuwa haina jibu. Madaraja hayo au teaching allowance hiyo wamekuwa wakipewa Wakuu wa Shule na Waratibu wa Elimu tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuiuliza, je, Serikali ina mkakati gani wa ziada kuhakikisha kwamba ahadi waliyoiweka mwaka 2012 kwamba watawapatia walimu posho ya kufundishia (teaching allowance) sasa itakuwa imepatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inajipanga kwa mambo mengi na ahadi zetu ni nyingi ambazo bado tunaendelea kuzitekeleza na hii ahadi ambayo anaisema Mheshimiwa Mbunge, nayo tutaitekeleza mara tutakapokuwa vizuri kifedha.

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Wilaya ya Karagwe ina walimu ambao bado wanadai malimbikizo ya mishahara, walimu hawa hupandishwa madaraja bila ya kurekebishiwa mishahara yao kitu ambacho kimekuwa ni kero kubwa kwa walimu wa Karagwe na maeneo mengine nchini. (a) Je, Serikali inawaambia nini walimu hawa na imefikia wapi kutatua kero zao? (b) Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakikisha Teachers Service Commission (TSC) inapata rasilimali watu na fedha ili iweze kutetea maslahi ya walimu nchini?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, walimu wa shule zote za Wilaya ya Songea walisimamishwa wakati Wilaya zingine wamepandiswa madaraja na maslahi yao yameongezeka, walimu wa Songea Vijijini hawakufanyiwa hivyo kwa sababu taarifa kutoka kwa Mkurugenzi zilichelewa kuifikia Wizara. Suala hili limefuatiliwa kwa miaka miwili sasa na walimu hawa hawajapata stahiki zao mpaka sasa.
Je, Serikali inatoa tamko gani kwa walimu waliopo Songea, kwa maana ya Songea Vijijini na Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kuhusu madai na malalamiko yao? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna kesi za aina mbalimbali, na hata jana nilipata kesi inayofanana na hiyo kutoka kwa Mheshimiwa Kanyasu. Nimewaelekeza wataalam wetu wafanye tathmini maeneo mbalimbali yenye changamoto, nikifahamu kwamba lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba watumishi wetu wanafaya kazi kwa amani. Maeneo mengine wamefanya vizuri, maeneo mengine bado hawajafanya vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimewaelekeza wataalam wangu waweze kufanya kufanya tathmini maeneo mbalimbali yenye changamoto ili tuwasaidie watumishi wote ambao wana changamoto mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuweze kubaini utendaji wa kazi wa baadhi ya watu tuliowapa mamlaka. Wale wataonekana kwamba wamekuwa ni kikwazo basi ni vyema tukaweza tukawachukulia hatua za kinidhamu kwa sababu katika njia moja au nyingine wanaweza wakasababisha Serikali ikalaumiwa kumbe kutokana na uzembe wa watu wachache.
Kwa hiyo jambo hili tumelichukua na toka jana timu yangu inafanyia kazi jambo hilo kwa sababu lilitoka vile vile katika Mkoa wa Geita. Maeneo mbalimbali kuna kesi kama hizo, kwa hiyo Serikali tunaichukulia yote kwa ujumla wake na kuyafanyia kazi. (Makofi)

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Wilaya ya Karagwe ina walimu ambao bado wanadai malimbikizo ya mishahara, walimu hawa hupandishwa madaraja bila ya kurekebishiwa mishahara yao kitu ambacho kimekuwa ni kero kubwa kwa walimu wa Karagwe na maeneo mengine nchini. (a) Je, Serikali inawaambia nini walimu hawa na imefikia wapi kutatua kero zao? (b) Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakikisha Teachers Service Commission (TSC) inapata rasilimali watu na fedha ili iweze kutetea maslahi ya walimu nchini?

Supplementary Question 6

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ilihamisha walimu 210 kwa wakati mmoja, lakini mpaka sasa hivi walimu wale hawajalipwa stahili zao.
Je, ni lini walimu wale wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto watalipwa pesa zao za uhamisho?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza tulichukue hilo tujue kwa nini kwa sababu kuna fedha maalum tulizitoa kwa EPforR kwa ajili ya kuhakikisha walimu wanahamishwa katika maeneo mbalimbali na stahili zao zinapatikana. Kesi kama hiyo tumeshaanza kuishughulikia katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ambako nadhani kuna maeneo mbalimbali imejitokeza kesi kama hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaangalia nature ya uamisho huo ulikuwaje na kwa nini watu walikuwa hawajalipwa, na kama walikuwa hawajalipwa ikiwa tayari Serikali ilishatoa pesa kwa EPforR tutaangalia nini tufanye.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Shekilindi naomba tulichukue hilo kama Serikali kwa concern ya eneo la Lushoto pamoja na maeneo mbalimbali ambayo yatakuwa na kesi kama hiyo. Tutaweza kuratibu vizuri jinsi gani ya kuondoa tatizo hili ambalo hatimaye kama nilivyosema awali tunataka walimu waweze kuhama kwenye maeneo ya kazi wakiwa wamefanya kazi kwa amani kama inavyokusudiwa. (Makofi)