Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:- Serikali imetenga maeneo kadhaa kwa ajili ya uwekezaji nchi nzima:- Je, ni lini Serikali itatafuta fedha za kutosha kuweka miundombinu muhimu katika maeneo haya ili kuvutia uwekezaji?

Supplementary Question 1

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kweli nasikitika hili jibu ni la juu juu mno. Hii Wizara imeshafanya mambo mengi tunayoyajua, ningetegemea hapa ingekuwa ndio wakati Serikali ingetueleza ambayo wameshafanya na yale ambayo bado. Hata hivyo, tumeletewa taarifa ambayo mwananchi wa kawaida anayesikiliza sasa hivi wala haelewi kama Serikali imefanya chochote katika masuala ya viwanda katika maeneo maalum wakati nafahamu kuwa yameshafanyika mengi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, basi baada ya kusema hivyo nina maswali mawili ya nyongeza. Sasa katika hayo maeneo ambayo yametengwa ambayo nayafahamu kuna industrial parks, stand alones na kuna maeneo mengine ambayo ni ya Wilayani; ni mangapi ambayo mpaka sasa hivi yameshawekewa hiyo miundombinu saidizi na miundombinu wezeshi na kiasi gani ambacho tayari kinazalishwa na mapato kiasi gani nchi inapata na ajira kiasi gani kimeshazalishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuzingatia kuwa katika changamoto ambazo zinakwamisha na ambazo zimekuwa zikikwamisha kuendelezwa maeneo haya nyingi ziko katika uwezo wetu kuzitekeleza. Hiyo miundombinu inayozungumzwa ni kitu ambacho kiko kwenye uwezo wetu tukiamua. Haya masuala ya utata kati ya special economic zones na economic processing zones yanaweza kutatuliwa. Sasa ni kwa nini basi hatujakamilisha japo tuwe tuna maeneo mawili kila mwaka yanayofanyiwa kazi? Maana yameshatengwa na wananchi wamezuiwa kuyaendeleza lakini sisi hatujayafanyia chochote zaidi ya miaka 10 sasa. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nashukuru pia kwa majibu na maelezo ya Mheshimiwa Mbene. Kimsingi majibu yaliyoletwa ni majibu sahihi isipokuwa kwa maswali yake ya nyongeza naomba nimjibu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza; katika suala la uendelezaji wa maeneo hayo, ninavyofahamu ni kwamba katika uendelezaji wa miundombinu kuna miundombinu ambayo ni direct inayotokana na uwekezaji wa moja kwa moja katika eneo la economic processing zone au (SEZ); lakini pia kuna maeneo wezeshi yanayofanywa na sekta nyingine kama nishati pamoja na maji na miundombinu mingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa misingi hiyo, kwa mfano, ukisikiliza katika michango ya jana kuna uwezeshaji mkubwa uliofanyika na Serikali kwa ajili ya bomba la gesi ambalo mpaka sasa limezunguzwa kwamba itatumika takribani asilimia sita; lakini bomba hilo itakuwa tayari kuwekeza viwanda 190 vinavyotarajiwa katika Bagamoyo Economic Zone na maeneo mengine. Kwa hiyo, ni tayari Serikali imeshawekeza fedha nyingi katika miundombinu ya aina hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ukirudi pia Benjamini Mkapa pale kuna miundombinu ambayo imewekezwa na Serikali lakini pia na wadau binafsi jumla yake ni takribani bilioni thelathini na saba na ina uwezo kuajiri watu moja kwa moja 5,000 ambao wanazalisha ajira zisizo rasmi zaidi ya 12,500. Hiyo yote ni uwekezaji ambao umefanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile kwa upande wa Kigoma economic processing zone, pale tumepata mwekezaji binafsi ambaye yeye amewekeza umeme wa sola wa takribani mega watt 5 ambao uko tayari inangojewa tu kuunganishwa kwa upande wa TANESCO. Kwa hiyo kimsingi Serikali imekuwa ikiwekeza na inaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande maeneo ambayo yalitengwa katika mikoa Serikali imelipa fidia maeneo mbalimbali ikiwemo Kurasini ambayo tumelipa takribani shilingi bilioni mia moja na tatu na maeneo mengine kama Songea na Mara na mengine. Kimsingi tunachozungumza sasa hivi ni kwamba badala ya kuchukua fedha yoyote ya Serikali kuifungia katika kuilipia maeneo na wakati mwingine hao wawekezaji wanakuwa hawajajitokeza. Kwa hiyo tunachofanya sasa ni kuwashirikisha wawekezaji wenyewe ili yule anayehitaji eneo maalum basi aweze kusaidia katika kulipa fidia na kulitumia kwa malengo ambayo yanakuwa yamekusudiwa kwa win win stuation kwa upande wa Tanzania na huyo mwekezaji wetu.