Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Je, ni lini Benki ya Wanawake Tanzania itaanzisha tawi lake Zanzibar kwa madhumuni ya kuwapatia huduma za kibenki na mikopo yenye riba nafuu kwa ajili ya kuwainua kiuchumi wajasiriamali wanawake wa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa katika uanzishwaji wa Benki hii ya Wanawake wa Tanzania, Wabunge wengi hususan Wanawake wakati ule walichangia mtaji ama fedha katika benki hii. Hata hivyo, Wabunge hao na wengine sasa hivi siyo Wabunge tena, hawajapewa hata shukrani hata ya kutambulika tu, hata shukurani hawajapewa. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, Wabunge hao wa wakati ule watapatiwa lini barua hiyo ya utambulisho na hata kupatiwa hisa zao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa katika majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kuwa uadilifu hapa hapana na kwamba wanataka kuteua tena Watendaji ama Maafisa mbalimbali ambao watakuwa waadilifu, ndiyo sasa imedhihirika kwamba, watendaji wa hii benki hawana uadilifu watendaji wake ndiyo maana ikafikia hapa ilipofikia. Je, uongozi na watumishi hao ambao si waadilifu wamechukuliwa hatua gani za kisheria? (Makofi)

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Dada yangu Mheshimiwa Faida Bakar kwa kazi nzuri sana ya kufuatilia masuala ya uwezeshaji wanawake kiuchumi, sio tu Zanzibar lakini pia Tanzania Bara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na swali lake la pili, hawa watumishi ambao wamekosa uadilifu wamechuliwa hatua gani. Kuanzia mwezi wa Agosti mwaka 2017 tumewapeleka katika vyombo vya usalama ikiwemo TAKUKURU na Polisi, Watumishi zaidi ya 20 akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji Magreth Chacha, kwa kukosa uaminifu na hivyo kusababisha benki kukosa hasara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni benki kupata hasara, Kiswahili kidogo kimepiga chenga. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo yamefanyika ya hovyo unakuta kuna SACCOS inakopeshwa shilingi bilioni moja, tunaifuatilia hiyo SACCOS haionekani hizo fedha zimeenda kwa nani. Kwa hiyo, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Faida kwamba tunaamini PCCB na Polisi watakamilisha uchunguzi haraka na lengo letu watumishi hawa ambao hawakuwa waaminifu waweze kwenye mbele ya vyombo vya dola na kuchukuliwa hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa nataka kumthibitishia Mheshimiwa Faida kwamba, Serikali imedhamiria kuhakikisha tunapata fedha ya kukuza mtaji wa benki, tumepewa miezi sita na BOT na nataka kuwathibitishia Waheshimiwa Wabunge kwamba, Mkurugenzi mpya ambaye tumemwajiri amefanya kazi kubwa, niseme ingawa ni Benki ya Wanawake lakini tumeajiri Mkurugenzi mwanaume ambaye ndani ya miezi mitano amefanya kazi kubwa sana ya kuhakikisha kwamba angalau hesabu za benki zinakaa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, lilikuwa ni suala la hisa, tunatambua mchango mkuwa sana wa Wabunge wa Bunge la Tisa ambao waliweza kununua hisa kwa ajili ya kuhakikisha mtaji wa benki unakua na moja ya jambo ambalo limekwama ni lile la BOT kwamba lazima tuweke vizuri suala la shareholders, halafu ndiyo tutawapa certificate zao za hisa. Kwa hiyo, suala hili pia tutalikamilisha ndani ya siku chache. Nakushukuru sana.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Je, ni lini Benki ya Wanawake Tanzania itaanzisha tawi lake Zanzibar kwa madhumuni ya kuwapatia huduma za kibenki na mikopo yenye riba nafuu kwa ajili ya kuwainua kiuchumi wajasiriamali wanawake wa Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Benki hii imekuwa ikikiuka taratibu za kibenki kwa muda mrefu sana jambo ambalo limepelekea BOT kuwapa karipio kali. Je, Serikali imejiridhisha vipi kwamba ubadilishwaji wa Menejimenti ndiyo dawa au suluhisho pekee la uendeleaji mzuri wa benki hii? Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kama alivyosema katika maelezo yake ya awali Mheshimiwa Waziri, ni kwamba baada ya kufanya mapitio ndani ya Benki yetu tukaona kwamba kulikuwa kuna upungufu, hatua ambazo tulizichukua moja ni kufanya mabadiliko ya Menejimenti na kuanzia mwezi Mei, tumeweka Mkurugenzi mpya, tumepitia mfumo wa utendaji na uongozi katika benki ile na kuajiri watumishi wapya ambao ni waadilifu, sasa hivi hatua ambazo zimechukuliwa kwa haraka na imetusaidia kuhakikisha kwamba hata ule mtaji wetu umezidi kukua na hasara kupungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naamini kabisa ndani ya muda mfupi, ndani ya mwaka huu tutakuwa tumepiga hatua nzuri na benki itarudi kwenye mstari. (Makofi)

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Je, ni lini Benki ya Wanawake Tanzania itaanzisha tawi lake Zanzibar kwa madhumuni ya kuwapatia huduma za kibenki na mikopo yenye riba nafuu kwa ajili ya kuwainua kiuchumi wajasiriamali wanawake wa Zanzibar?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri kwa kuwa benki hii ukiitazama na kwa namna ambavyo anaongea kwamba inaelekea kupata hasara ni kwamba benki hii inaweza ikafa na Serikali ilikwishaahidi kuinusuru kwa kuipatia mtaji. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya kuipatia mtaji ili benki hiyo iweze kufanya kazi?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya sharti ambalo tulipewa na Serikali, nikiimanisha Waziri wa Fedha ni kwamba tufanye forensic audit ambayo tuliifanya mwaka jana na hiyo actually ndiyo imetusaidia tukabaini upungufu ambao ulionekana, kwa hiyo na Waziri wa Fedha anatusikiliza. Naamini kwa sababu tumeshafanya forensic audit, tumeteua Bodi mpya ya Benki lakini pia tumeweka Menejimenti mpya, kwa hiyo naamini Waziri wa Fedha atatimiza ahadi ya Serikali ya kuipatia mtaji benki kama walivyoahidi mwaka 2010.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie tu Mheshimiwa Dkt. Kikwembe kwamba licha ya kuwa tunategemea kupata fedha kutoka Serikalini, lakini tayari tumeanza mazungumzo na Benki nyingine ambazo sitaki kuzitaja ziko tayari kufanya partnership na Benki ya Wanawake ili tuhakikishe kwamba huduma za Tanzania Women Bank zinatolewa pia katika Benki hiyo, kwa hiyo, tunakwenda vizuri na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pia iko tayari kuhakikisha inawezekeza katika Benki ya Wanawake, kwa sababu hii ni Benki ya wote na wanufaika wakubwa wa benki hii ni wanawake. Nakushukuru sana. (Makofi)