Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Prosper Joseph Mbena
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini
Primary Question
MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- (a) Je, kwa nini Serikali haina utaratibu wa kuwachukua wagonjwa wa akili wanaoranda randa barabarani na mitaani na kuwapeleka kwenye hospitali za wagonjwa wa akili kupatiwa matibabu? (b) Je, Serikali inafahamu idadi ya wagonjwa wa akili waliopo barabarani na mitaani kwenye wilaya za nchi yetu ambao wanahitaji huduma ya matibabu na inatoa maelekezo gani kwa Waganga Wakuu wa Wilaya kuhusu kuwahudumia wagonjwa hao?
Supplementary Question 1
MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na rai aliyoitoa kwa wahusika. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa tatizo hili linaonekana kuongezeka nchini; je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba Hospitali Maalum ya wagonjwa wa akili nchini yaani hospitali ya Mirembe inawezeshwa kiutaalam na vifaa ili kuweza kukabili tatizo hili?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kuwahakikisha kwamba hospitali zote za Wilaya pamoja na za Mikoa zinapatiwa angalau Daktari mmoja ambaye ni mtaalam wa mambo ya akili ili kuweza kutoa huduma ya karibu kwa wananchi? Ahsante.
Name
Dr. Faustine Engelbert Ndugulile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigamboni
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuifanyia maboresho Hospitali ya Rufaa ya Mirembe. Hivi tunavyoongea tunakamilisha ukarabati ambao umetugharimu zaidi ya milioni 976 na itaongeza kupanua wigo sana kuiboresha hospitali yetu ili kutoa huduma nzuri na za ziada. Sambamba na hilo tumeendelea kuongeza Wataalam na kutoa mafunzo kwa wataalam walioko ili waweze kutoa huduma bora na zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili alitaka kujua, je, tuna mkakati gani wa kupeleka wataalam katika ngazi za mikoa na wilaya. Katika utaratibu wetu wa sasa ngazi ya rufaa katika masuala ya afya ya akili ni ngazi ya mikoa hili tunalifahamu na tuko katika mchakato wa kuhakikisha kwamba tunawajengea uwezo Madaktari ili tuweze kupata Madaktari Bingwa wa Afya ya Akili kuweza kutoa huduma hizo katika ngazi ya rufaa ya Mikoa.
Name
Halima Abdallah Bulembo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- (a) Je, kwa nini Serikali haina utaratibu wa kuwachukua wagonjwa wa akili wanaoranda randa barabarani na mitaani na kuwapeleka kwenye hospitali za wagonjwa wa akili kupatiwa matibabu? (b) Je, Serikali inafahamu idadi ya wagonjwa wa akili waliopo barabarani na mitaani kwenye wilaya za nchi yetu ambao wanahitaji huduma ya matibabu na inatoa maelekezo gani kwa Waganga Wakuu wa Wilaya kuhusu kuwahudumia wagonjwa hao?
Supplementary Question 2
MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo wagonjwa wote wa akili wanaranda mitaani hata miongoni mwetu tunaweza kuwa wapo wagonjwa wa akili. Kwenye nchi za wenzetu wamefanya utafiti wa wagonjwa wa akili nchi kama Marekani, Uingereza na Australia, tafiti zao zinasema katika kila watu wanne kuna mgonjwa mmoja mwenye tatizo la akili. Je, ni lini sasa nchi yetu itamua kufanya utafiti kama huu ili kubaini tuna wagonjwa wangapi wa akili nchini? (Makofi)
Name
Dr. Faustine Engelbert Ndugulile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigamboni
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Halima Bulembo kwamba, siyo wagonjwa wote wa akili wanarandaranda mitaani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa tafsiri ya afya ya Shirika la Afya Duniani inasema kwamba being health is not just merely absence of disease is mental, physical and social well-being. Sasa siyo kwamba tu unapokuwa na mwili umeathirika ndiyo unaweza ukasema kwamba wewe umeathirika. Kwa hiyo, katika suala la afya ya akili, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba si kila mtu anayerandaranda mitaani ndiyo mwenye ugonjwa wa akili, hata sisi inawezekana kama nilivyokuwa nimesema, katika swali langu la msingi, tunakadiria kwamba asilimia moja ya Watanzania wana matatizo ya akili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo ya akili naomba niendelee kutoa maelezo tuna matatizo mengi sana ya akili. Kuna sonona ambayo ni depression, kuna schizophrenia, kuna mania, obsessive complusive disorder, kuna mlolongo mkubwa sana ambao ni mpana sana na ambao kwa kweli hatuwezi tukafanya utafiti wa moja kwa moja kuweza kubaini katika jamii, ila tunaweza tukalifanya kwa wale ambao wanafika katika vituo vyetu vya afya na wale ambao tunaweza kuwabaini katika jamii. (Makofi)
Name
Susan Anselm Jerome Lyimo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- (a) Je, kwa nini Serikali haina utaratibu wa kuwachukua wagonjwa wa akili wanaoranda randa barabarani na mitaani na kuwapeleka kwenye hospitali za wagonjwa wa akili kupatiwa matibabu? (b) Je, Serikali inafahamu idadi ya wagonjwa wa akili waliopo barabarani na mitaani kwenye wilaya za nchi yetu ambao wanahitaji huduma ya matibabu na inatoa maelekezo gani kwa Waganga Wakuu wa Wilaya kuhusu kuwahudumia wagonjwa hao?
Supplementary Question 3
MHE. SUSAN J. A. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Naibu Waziri, amekiri kwamba sasa hivi kuna magonjwa mengi ya akili na sasa hivi linaongezeka hili la vyuma kukaza watu wamekuwa na stress sana. Pamoja na kwamba Hospitali ya Mirembe ndiyo Hospitali ya Kuu na inafanyiwa maboresho na tunakubaliana kwamba magonjwa haya yamekuwa mengi na kwa maana hiyo jamii nzima ina haya magonjwa. Je, wana utaratibu gani kuhakikisha kwamba kwenye vituo huko mikoani, wilayani, wanaviboresha ili kuweza kuwasaidia hawa watu wenye matatizo ya magonjwa ya afya ya akili? (Makofi)
Name
Dr. Faustine Engelbert Ndugulile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigamboni
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Magonjwa ya akili yanasababishwa na mambo mengi ikiwa ni pamoja na kurithi kijenetiki lakini vilevile matumizi ya vilevi mbalimbali, changamoto na stress za maisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ambazo Serikali inazifanya; moja ni kama tulivyosema tumeboresha huduma katika hospitali yetu ya Rufaa ya Mirembe. Sambamba na hilo tumeendelea kujenga uwezo katika hospitali zetu za Rufaa za Kanda na tumesema tutakwenda mbali zaidi na kwenda kuboresha katika hospitali zetu za Rufaa za Mikoa, sambamba na hilo kuweka mifumo mizuri ya Rufaa kutokea ngazi ya dispensari hadi katika hospitali yetu ya Mirembe. (Makofi)