Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 1

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza kabisa namshukuru Waziri wa Wizara hiyo kwa sababu alifika na alifanya kazi mpaka saa mbili usiku na akanyeshewa na mvua alifika Ibaga. Pia Waziri aliacha maagizo ya kwamba umeme uende nyumba kwa nyumba usivuke na nguzo ziletwe zaidi ya 20. Nguzo zilizokuja ni 20 na umeme umekwishawaka lakini umetengeneza ubaguzi kwa sababu ziko taasisi za dini hazijapata, misikiti na baadhi ya wananchi. Kwa hiyo, umeme umewaka lakini bado umeleta matatizo. Je, ni lini agizo la Waziri litatekelezwa la kuongeza nguzo, umeme uwake katika maeneo hayo ili tatizo hilo liwe limekwisha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wa Mkalama wako tayari kutekeleza sera ya viwanda inayoasisiwa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Je, yupo tayari baada ya Bunge kutembelea na kuwathibitishia wananchi kuwaka kwa umeme kupitia REA III kwa Vijiji vya Mwanga, Kidarafa, Kikonda, Ipuli, Isanzu na maeneo mengine ya Mkalama ambayo yana uzalishaji mkubwa? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Allan Kiula kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia utekelezaji wa miradi hii, nimepokea shukrani za Mheshimiwa Waziri wangu kwa ziara yake. Napenda nisisitize agizo lake la Mheshimiwa Waziri la kuagiza kwamba, zifike nguzo za kutosha katika maeneo ambayo miradi Awamu ya Pili haikukamilika katika Mkoa wa Singida litekelezwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtaarifu kwamba, katika utaratibu huo mkandarasi mpya ambaye amepewa kazi ya kukamilisha miradi ambayo iliachwa na Mkandarasi wa awali Spencon, tumemwelekeza kwamba, maeneo yote nguzo zifike kwa wakati na ni nyingi na wananchi wote wa maeneo yale ambao wamekaa muda mrefu kusubiria umeme wa REA Awamu ya Pili wapatiwe huduma na pasiwepo kitongoji ambacho kimerukwa wala taasisi za jamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili; umekuwa utaratibu wa Wizara yetu kwa kuwa, tunatambua miradi hii inatekelezwa vijijini kufanya ziara, wilaya kwa wilaya, kata kwa kata na kijiji kwa kijiji ambako miradi inatekelezwa. Kwa hiyo, nimuahidi kwamba, ziara katika Mkoa wa Singida katika maeneo aliyoyataja ikiwemo Ipali, Mwanga na Isanzu itafanyika kama ambavyo ilivyokuwa kawaida ya Wizara yetu. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 2

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la REA linahusu pia, Kata ya Soga, Kibaha Vijijini ambapo katika Kijiji cha Zogowale umeme ulifika kwa ajili ya ku-pump maji mpaka umefika Shule ya Waamuzi, Sekondari. Wananchi wa Kijiji cha Msufini walihamasishwa kutoa mazao na kutoa ardhi kwa ajili ya kupitisha umeme wa REA, huu ni mwaka wa tatu na hiyo kazi haijafanyika. Je, Wizara ina mpango gani kuhakikisha wale wananchi ambao wameshatoa mimea yao na wametoa ardhi zile nguzo za umeme zipite mpaka ufike Msufini pale Kata ya Soga na vijiji vya karibu?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na napenda nimshukuru Mheshimiwa Mbunge mwenzangu wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani. Nimthibitishie maeneo aliyoyataja Zogowale na hapo Kijiji cha Msufini kwamba, maeneo haya yamezingatiwa katika Mradi wa Peri Urban ambapo kwa kweli Serikali baada ya kuona kuna maeneo ni vijiji ambavyo vimekuwa na ongezeko la makazi na vimekuwa vikubwa, Serikali ikaja na Mradi wa Peri Urban ambao ni nje ya REA Awamu ya Tatu. Kwa hiyo, nimtaarifu na nimthibitishie vijiji hivyo vipo katika mradi huu Mpya wa Peri Urban ambako kazi ilitangazwa na mchakato wa kumtafuta mkandarasi sasa unaendelea. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 3

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, tatizo la REA II katika vijiji vingi umeme umepita bila kugusa maeneo ya wananchi. Je, nini Kauli ya Serikali kwamba, vijiji vyote ambavyo vilipitiwa na REA II na haujafika kwa wananchi vinarekebishwa ili wananchi waendelee kupata umeme kuliko umeme umepita katika vijiji lakini haujawagusa wananchi?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Julius kwa swali lake zuri na kwa kuwa, swali lake limejielekeza kwamba, utekelezaji wa miradi ya REA II kwamba kuna baadhi ya wananchi hawakufikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimtaarifu pamoja na Bunge lako Tukufu kwamba Serikali baada ya kuliona hilo kwamba, kuna maeneo yanatakiwa yafikiwe na miundombinu ya umeme ilikuja na mradi mpya densification, maana yake ujazilizi. Mradi huu unajielekeza kwenye maeneo ambako miundombinu ya umeme mkubwa imepita, lakini zipo kaya, vipo vitongoji, zipo taasisi za kijamii ambazo hazijafikiwa, kwa hiyo, huu mradi wa densification ambao umeanza kwa majaribio Mikoa Nane ikiwemo Mkoa wa Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Mara, Songwe, Iringa pamoja na Pwani umeonesha mafanikio na katika maeneo hayo kazi zinaendelea na wamefikia hatua sasa ya kufunga transformer.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mradi huu ambao umelenga vijiji 305 na kuunganisha wananchi elfu 53, kwa kuwa, Serikali imeona mradi huu una mafanikio mradi, nataka nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, hii densification sasa itaendelea na mikoa mingine. Hata sasa Mshauri Mwelekezi yuko katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kutathmini na kuona namna ambavyo tutatekeleza mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimtaarifu tu Bunge lako kwamba, kwa kweli, wananchi wasiwe na wasiwasi, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli itakamilisha miradi hiyo.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 4

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri sambamba na Waziri mwenye dhamana wamekuwa mara kadhaa wakijibu maswali hapa na kuahidi kwamba, visiwa vidogo vyote nchi nzima vitapatiwa umeme wa solar. Sasa ningependa kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, ni lini umeme wa solar utakwenda katika Visiwa vya Jibondo, Chole, Juani na Bwejuu? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Dau, Mbunge wa Mafia kwa swali lake zuri na tunatambua Mafia nako ni Wilaya ambayo ina visiwa vingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nisisitize kwamba, hii miradi tunayosema, huu mradi kabambe wa REA awamu ya tatu tunaoutekeleza, vijiji ambavyo vimetamkwa 7,873 vinahusisha pia na vijiji ambavyo tunaviita off grid. Kwa hiyo, nimthibitishie mchakato wa kuwapata Wakandarasi wanaopeleka umeme katika maeneo ambayo si rahisi kufika miundombinu ya kawaida unaendelea. Kwa mfano, Mkuranga kuna visiwa ambavyo tulipeleka umeme kupitia REA hii na utaratibu unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo niseme siyo Mafia tu, lakini katika maeneo mbalimbali ambayo ni magumu kufikika kwa miundombinu ya kawaida, mradi huu wa REA Awamu ya Tatu ambapo vipindi vyake ni hii 2017/2018, 2018/2019 na 2019/2020 vijiji hivyo vitapatiwa. Hakuna kijiji ambacho kitaachwa kwa sababu tu ya mazingira yake. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 5

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Tatizo lililoko Iramba Mashariki halina tofauti na tatizo lililoko Singida Kaskazini, Manyoni Magharibi, pamoja na Jimbo la Ikungi. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka umeme kwa vijiji vilivyobaki ambavyo vilikuwa katika mpango wa REA II, ukizingatia sasa tuko mpango wa REA III, ili wananchi wa maeneo hayo waweze kunufaika na Sera ya Viwanda? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nampongeza sana Mheshimiwa Aisharose kwa swali lake zuri. Naomba nimtaarifu tu katika maeneo ambayo ameyataja, Singida Kaskazini, Manyoni Magharibi, Ikungi, Mkandarasi ambaye anaenda kufanya kazi hizi zilizoachwa na Mkandarasi Spencon ameshateuliwa ambaye ni Emek Engineering and Dynamic na System Company Limited. Kwa hiyo, wako katika mchakato wa kumalizia tu masuala ya manunuzi ya kutoa Performance Bond, lakini kazi itaanza muda siyo mrefu na kwamba vijiji vyote ambavyo viliachwa awamu ya pili vitapatiwa umeme. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 6

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona niulize swali dogo la nyongeza. Matatizo yaliyopo Iramba Mashariki yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo Wilaya ya Ngara. Vijiji vingi vya Wilaya ya Ngara, hasa Tarafa ya Lulenge, havina umeme. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika vijiji hivyo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niungane nawe kuwapongeza Wabunge Viti Maalum na Wabunge wote ambao kwa kweli Bunge zima hili leo ni ushuhuda kwamba, limekuwa likifuatilia miradi ya nishati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Oliver kwa swali lake zuri ameuliza kwamba, Vijiji vya Wilaya ya Ngara ni lini vitapatiwa nishati ya umeme. Nataka nimjibu kwamba, kama ambavyo tumekuwa tukitoa taarifa ndani ya Bunge lako na si taarifa tu kwamba labda ni porojo ni kweli, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli inatekeleza huu mradi kabambe wa kupeleka umeme katika vijiji vilivyosalia 7,873.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe pia ni shahidi. Jana wakati tunahitimisha taarifa ya Kamati yetu ya Nishati na Madini, Mheshimiwa Waziri wangu wa Nishati alitoa taarifa kuwashwa kwa umeme katika vijiji 24 katika utaratibu huu wa REA awamu ya tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wilaya ya Ngara Mkandarasi yupo anafanya kazi. Ameanza zile kazi za awali za upembuzi na kadhalika lakini kwa sasa Wakandarasi wote nchi nzima wana-mobilise vifaa na wengine wako site wanaendelea na kazi mbalimbali. Nataka nilitibitishie Bunge, ile awamu ya kwanza ambavyo ni vijiji 3,559 tumesema mpaka Juni, 2019 viwe vimekamilika halafu tunaanza safari nyingine ya kumalizia vijiji vingine. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 7

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Kigoma ni Mikoa ambayo haijafaidika na miradi ya REA Awamu ya Tatu kwa sababu ya walioomba tenda kugombania tenda na kushtakiana Mahakamani. Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua huo mgogoro ili wananchi wa Mikoa hiyo waweze kupata huduma ya REA awamu ya tatu?

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Kakoso kwa swali lake zuri. Nichukue fursa hii kuwapa pole na kuwaomba radhi wananchi wa Mikoa ya Kigoma na Katavi, lakini ameuliza Serikali ina mpango gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimtaarifu suala hili lipo Mahakamani. Kwa kuwa, Mahakama ni chombo pekee ambacho kinatoa haki, sisi kama Serikali ya Awamu ya Tano tutasikiliza maamuzi ya Mahakama, kwa hiyo mgogoro huu utatatuliwa na Mahakama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwambie kwa kuwa, Mamlaka ya Manunuzi (PPRA) hawakuwa na kipingamizi katika suala la mchakato, Wakala wetu wa Nishati Umeme Vijijini (REA) wameanza mchakato wa kumpata mkandarasi mpya, lakini kama yatatokea maamuzi mengine ya Mahakama tutaendelea kuyaheshimu, lakini kwa mpango ndani ya Wizara tunaamini kuanzia Machi 2018 Mkandarasi mpya atapatikana. Ahsante sana.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina shida kubwa ya Nishati ya Umeme licha ya mpango wa REA II na REA III kuwepo nchi nzima:- (a) Je, ni lini miradi iliyokuwa chini ya REA II itakamilika baada ya kutekelezwa katika Kata ya Ibega, Mwangeza na Mpambala? (b) Je, ni lini REA III itaanza Mkalama hasa ikizingatiwa mikoa yote imepata wakandarasi?

Supplementary Question 8

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Mji wa Tunduma uko mpakani mwa Zambia na Tanzania na ni Mji ambao unahudumia Mataifa zaidi ya Nane yanaotumia Mpaka wa Tunduma, lakini kumekuwa na tatizo kubwa sana la umeme kukatika mara kwa mara na kusababisha usalama wa wageni pamoja na Wakazi wa Mji wa Tunduma kuwa hatarini. Je, ni lini Serikali itaweka umeme wa uhakika, kama ambavyo wenzetu wa Zambia pale ng’ambo walivyoweka umeme wa uhakika? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii na napenda nimshukuru Mheshimiwa Frank kwa swali lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme Wilaya ya Tunduma ipo katika Mkoa wa Songwe, Mkoa ambao awali ulikuwa Mkoa mmoja wa Mbeya, kwa hiyo line zote zinazopeleka umeme katika Mkoa mpya wa Songwe zinatokana na Mkoa wa Mbeya. Kwa hiyo ni wazi njia ndefu ya kupeleka umeme katika Mkoa wa Songwe inasababisha kukatikakatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali kwa sasa pia ni kujenga Sub Station kubwa Tunduma ili kuwezesha upatikanaji wa umeme vizuri. Kwa sasa pia kuna mpango wa kujenga line ya kV 400 ambayo inaanzia maeneo ya Tunduma mpaka Mbeya inaenda mpaka Sumbawanga kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji wa umeme katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge Serikali ya Awamu ya Tano inatambua hilo tatizo, lakini mipango hii ipo na itatekelezeka na baada ya muda umeme utakuwa ume-stabilize katika Mkoa Mpya wa Songwe. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)