Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELLE aliuliza:- Ni Sera ya Taifa kuwa na Vituo vya Afya kwa kila Kata, na wananchi katika baadhi ya Kata wamejitahidi kujenga majengo kwa ajili ya vituo hadi kufikia usawa wa renta kwa nguvu zao:- (a) Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo ya vituo vya afya vya Ikobe, Ilolangulu, Kagera na Bukandwe? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Watumishi wa Afya Wilayani Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwanza naipongeza Serikali kwa jitihada zake za kuongeza pesa katika Sekta ya Afya na kuwezesha ujenzi huu na upanuzi wa vituo viwili hivi vya Iboya na Masumbwe. Je, Serikali sasa itakuwa tayari kuruhusu bajeti ya mwaka huu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe uanze baada ya mwaka huu kuiondoa hiyo bajeti kutokana na ukomo wa bajeti kwa maana ya ceiling. Ceiling ili-burst kwa hiyo, ile hela ambayo tulikuwa tumepanga kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya iliondolewa. Je, Mwaka huu wa Fedha itaruhusiwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, yamekuwepo madai ya muda mrefu ya watumishi ya uhamisho kutoka katika Wilaya mama ya Bukombe kuja Wilaya ya Mbogwe wakiwemo Watumishi wa Idara ya Afya hawajalipwa. Je, malipo haya yatafanyika lini ili kuondoa usumbufu kwa watumishi hawa ambao wamekuwa wakidai kwa muda mrefu. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa niaba ya Serikali tunazipokea pongezi zake za dhati maana yeye mwenyewe anakiri kwamba vituo viwili kwanza kujengwa kwa milioni 400, jumla milioni 800 siyo haba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anataka kujua je, Serikali itaruhusu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya baada ya kwamba haikuwezekana kutokana na ufinyu wa bajeti. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yote Wilaya zote 64 na jana nilijibu, ambazo hatuna Hospitali za Wilaya, hospitali zinajengwa. Ninachoomba kwa kupitia Halmashauri yake ni vizuri wakatenga eneo na wao wakaanza ujenzi ili Serikali ije kukamilisha ujenzi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili anauliza kuhusiana na suala la kuwalipa Watumishi ambao walihamishwa kutoka maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Wilayani kwake, lini watalipwa. Mara baada ya uhakiki kukamilika na Mheshimiwa Rais alilisema, kati ya madeni ambayo yanatakiwa kulipwa ni pamoja na madeni ya Walimu pamoja na Watumishi wa Afya. Zoezi hili litakamilika muda si mrefu.

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELLE aliuliza:- Ni Sera ya Taifa kuwa na Vituo vya Afya kwa kila Kata, na wananchi katika baadhi ya Kata wamejitahidi kujenga majengo kwa ajili ya vituo hadi kufikia usawa wa renta kwa nguvu zao:- (a) Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo ya vituo vya afya vya Ikobe, Ilolangulu, Kagera na Bukandwe? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Watumishi wa Afya Wilayani Mbogwe?

Supplementary Question 2

MHE. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Awali ya yote niwashukuru wananchi wa Songea Mjini kwa kunichagua kuwa Mbunge na kuwawakilisha katika Bunge lako Tukufu. Pili nikishukuru Chama changu cha Mapinduzi, Chama Tawala. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tatizo lililopo katika Jimbo la Mbogwe ni sawa na tatizo ambalo lipo katika Jimbo la Songea Mjini katika ujenzi wa Vituo vya Afya hususan katika Kata tatu za Ndilimalitembo, Ruvuma na Likuyufusi ambazo wananchi wamejitolea kwa mguvu na wanahitaji msaada wa Serikali. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya katika Kata ya Ndilimalitembo, Kata ya Ruvuma na Kata ya Likuyufusi? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer


NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kumpongeza kwa ushindi wake na karibu sana Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake anataka kujua lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kukamilisha vituo vya afya katika Kata zake hizo mbili. Ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba vituo vya afya vinajengwa tena vinajengwa vingi ili kuondoa adha ya matibabu kwa wananchi kwa kutokwenda umbali mrefu kupata huduma ya matibabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeanza na vituo 205 baada ya hivi 205 kukamilika ni azma ya Serikali kuhakikisha na maeneo mengine na hasa ambayo kuna upungufu mkubwa na hasa kwa mijini kumekuwa na msongamano mkubwa sana wa wananchi kufuata huduma ya afya katika hospitali za Mikoa na Wilaya. Ni azma yetu kuhakikisha kwamba vituo vya afya vinajengwa ili kupunguza mrundikano ikiwa ni pamoja na maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge.

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELLE aliuliza:- Ni Sera ya Taifa kuwa na Vituo vya Afya kwa kila Kata, na wananchi katika baadhi ya Kata wamejitahidi kujenga majengo kwa ajili ya vituo hadi kufikia usawa wa renta kwa nguvu zao:- (a) Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo ya vituo vya afya vya Ikobe, Ilolangulu, Kagera na Bukandwe? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Watumishi wa Afya Wilayani Mbogwe?

Supplementary Question 3

MHE. EZEKIEL G. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza:
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Jimbo la Msalala kama ambavyo umesikia maeneo mengine haya mawili ambayo yameuliziwa maswali Songea Mjini na Mbogwe, wao pia wana maboma ya zahanati na vituo vya afya na bahati nzuri wenyewe wamekwenda mbali zaidi, kuna maeneo ambapo kumetajwa kwamba maboma yako kwenye lenta. Wananchi wa Jimbo la Msalala wana vituo vya afya vinne ambavyo vimekwishakamilika maboma yake, zahanati 38 ambazo zimekwishakamilika maboma yake. Maboma haya yamejengwa zaidi ya miaka mitatu na sehemu vimeanza kubomoka. Imefika mahali sasa wananchi wanagomea michango mingine wakisema kamilisheni kwanza miradi tuliyokwishaianza.
Nataka tu kujua toka Serikalini ni lini sasa Serikali na yenyewe italeta nguvu yake ambayo wastani ni kama bilioni ili kukamilisha maboma haya 42, manne ya vituo vya afya na 38 ya zahanati, Msalala?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa dhati kabisa nianze kwa kumpongeza kwa jitihada kubwa ambazo anafanya kwa wananchi wa Jimbo la Msalala, kwa ujenzi mkubwa ambao umefanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukiongea mara nyingi alichokuwa anaomba kwanza katika hizi pesa ambazo zimepatikana zikitumika zikakamilisha hayo majengo ambayo yanatakiwa kujengwa katika vituo vya afya, anataka hicho kiasi kinachobaki kipelekwe kwenye maeneo mengine. Jambo ambalo Serikalini wala hatuna ubishi nalo ni kuhakikisha kwamba jitihada za wananchi na tukibana vizuri pesa zikatumika maeneo mengine yaweze kujengwa kwa haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba tunakamilisha ujenzi wa vituo vya kutolea afya 1,845 na hivi tutavikamilisha.