Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tabia sugu ya wazazi hasa wababa kutelekeza watoto na kuwaachia akina mama walee watoto hao peke yao.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kudumu wa kuyapa nguvu Madawati ya Jinsia na Mabaraza ya Usuluhishi katika kata zetu ili waweze kuweka sheria ngumu ambayo itawafanya wababa hawa wasiweze kutelekeza watoto wao? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali ina mpango gani wa kuzileta Bungeni Sheria za Ustawi wa Jamii ili tuweze kuzibadilisha kama siyo kuziondoa zile za zamani ili ziweze kuendana na hali ya maisha ya sasa? Nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga kwa maswali yake mazuri, lakini vilevile kuwa mtetezi mzuri wa haki za watoto. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba Serikali imeandaa na kuzindua Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili wa Jinsia dhidi ya akina Mama na Watoto wa mwaka 2017/2018 na utaisha mwaka 2020/2021. Sambamba na hilo, utekelezaji wake umeshaanza kwani hivi tunavyoongea sasa hivi tumezindua madawati 417 katika vituo vyetu vyote vya polisi ambavyo vinasimamia masuala yote yanayohusiana na ukatili wa kijinsia kwa akina mama na watoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, sasa tunakwenda mbali zaidi na kwamba tunaanzisha Kamati za Ulinzi wa wanawake na watoto ambapo Maafisa Ustawi wa Jamii, Maafisa Maendeleo ya Jamii na Wajumbe wa Mabaraza watakuwa ni sehemu ya mkakati huo, kuwajengea uwezo, kuwapa elimu kusimamia haki za wanawake na watoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri katika swali lako la pili kwamba viwango vya sasa haviendani na hali halisi, sasa hivi tu katika mchakato wa kuandaa Sheria mpya ya Ustawi wa Jamii ambayo itazingatia hali ya sasa.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 2

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa hakuna shaka yoyote chanzo kikuu cha ongezeko la watoto hawa ni kutokana na wanaume wanaoshindwa kutimiza wajibu wao na kuwaachia ulezi wanawake peke yao. Katika Bunge lililopita nilishuhudia binafsi hapa Bungeni wanawake wakileta watoto waliotelekezwa na Waheshimiwa Wabunge. (Kicheko/ Makofi/Vigelegele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, kupitia Waziri wa Afya, yuko tayari kutoa wito kwa wanawake wote waliotelekezewa watoto na Waheshimiwa Wabunge wawalete hapa na wakabidhiwe majukumu yao? (Kicheko/ Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, shida siyo kuzaa, shida ni matunzo na kulea na mimi nitoe rai kwa wanaume wote pamoja na sisi Waheshimiwa Wabunge kuhakikisha kwamba tunashiriki kikamilifu katika matunzo na malezi ya watoto. Hata hivyo, nataka tujielekeze zaidi katika mfumo wa sheria na kutengeneza mfumo endelevu. Sheria yetu inatutaka twende katika Ofisi za Ustawi wa Jamii katika Halmashauri zetu badala ya kuwaleta watoto hawa wote hapa Bungeni. (Kicheko)

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii na mimi nipate kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kumekuwa na tatizo la watoto wa mitaani hasa kwenye miji mikubwa kwa mfano, Arusha, Mwanza, Dar es Salaam na kadhalika na watoto hawa wamekuwa wakitumiwa kwenye masuala ya uhalifu kama madawa ya kulevya na kadhalika. Je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha watoto hawa wanarudi shuleni na kupata angalau malezi bora? (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali tunakiri tumekuwa na tatizo hilo na moja ya jambo ambalo tumelifanya kwanza ni kubaini idadi ya watoto katika hii miji mikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika takwimu tulizokuwa nazo sasa hivi katika Mikoa ya Mwanza, Dar es Salaam, Iringa, Mbeya, Dodoma na Arusha tuliweza kubaini watoto 7,748 ambapo 6,365 walibainika kwamba wanashinda mitaani na kurudi nyumbani na watoto 1,383 hushinda na kulala mitaani. Pamoja na juhudi hizo, Serikali kati ya mwezi Julai, 2017 mpaka Novemba, 2017 tuliweza kuwaunganisha watoto 952 na kuwarejesha katika familia zao.

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 4

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 8 Septemba, 2016 niliuliza swali kama hili na nikatoa utafiti nikampa Naibu Waziri ambao ulionesha Serikali ya Tanzania haijui tatizo la watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Baada ya kusikiliza majibu ya Serikali, nalazimika kusema kwamba bado Serikali haijalijua kwa undani suala la watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
Je, ni lini sasa Serikali itaamua kufanya utafiti na kuja kutupa namba sahihi ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu nchini? (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema kwamba Serikali haijui takwimu sahihi na hapa katika majibu yangu ya swali la nyongeza ambalo lilikuwa limeulizwa na Mheshimiwa Maryam Msabaha nimetoa takwimu naomba nizirudie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mikoa sita ambayo tumefanya ukaguzi kwa maana ya Mkoa wa Mwanza, Dar es Salaam, Iringa, Mbeya, Dodoma na Arusha tumebaini watoto 7,748 kati yao 6,365 walikuwa wanashinda mitaani na kurudi majumbani na watoto wengine 1,383 hushinda na kulala mitaani.
Katika hawa watoto Mheshimiwa Halima Bulembo 952 tumeweza kuwarudisha na kuwaunganisha na familia zao. Kwa hiyo, naomba nimalizie kwa kusema kwamba Serikali inatambua tatizo hilo na imeshachukua hatua.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 5

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya ukatili na unyanyasaji mkubwa wa watoto wa kike ni wa kuwanyima fursa ya kurudi shuleni pale ambapo wanapata ujauzito kwa kuzingatia mazingira mbalimbali ambayo yanapelekea watoto wetu wa kike kupata mimba wakiwa watoto wadogo. Sasa ninatambua kwamba kipindi cha Serikali ya Awamu ya Nne ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na cabinet yake, kuna initiative mbalimbali walizozifanya hali iliyopelekea kuanza utekelezaji wa re-entry policy, kwamba mtoto anapata mimba, anapata fursa ya kurudi shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilitaka tu Serikali iniambie, kwa kuzingatia kwamba kama viongozi, tuna wajibu wa kujali mustakabali wa mtoto wa kike; na kwa kuzingatia kwamba katika nchi yetu kuna mazingira mengi ambayo nikiyataja hapa siwezi kuyamaliza, yanayopelekea mtoto huyu kushindwa kusoma na kushindwa kuzuia hivyo vishawishi ama kushindwa kukabiliana na nguvu kubwa za nje ambazo zinamzidi uwezo wake wa akili; ni lini sasa Serikali itafanya utekelezaji wa ile kazi kubwa ambayo mlifanya katika kipindi cha miaka 10 iliyopita mpaka kipindi cha awamu ya Mheshimiwa Jakaya kilipoisha? (Makofi). Mheshimiwa Mwenyekiti, nahitaji kujua utekelezaji tu.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kulikuwa na maandalizi ya re-entry policy lakini utekelezaji wake sasa umepitwa na wakati kutokana na maagizo ambayo yametolewa na Serikali kwamba mtoto ambaye amepata ujauzito hataruhusiwa kurudi tena katika shule ambayo alikuwa anasoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maagizo haya hayajamzuia mtoto wa kike ambaye amepata ujauzito kutoendelea na masomo. Naomba tuelewane vizuri, imezuia mtoto wa kike kurudi shule ambayo alikuwa anasoma, lakini haijazuia mtoto wa kike kuendelea na masomo. Kwa hiyo, ndani ya Serikali tunajaribu njia mbadala ya kuhakikisha kwamba watoto hawa ambao wamepata ujauzito wanaendelea na masomo.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa maelezo yake mazuri kuhusiana na suala la watoto ambao wanapata ujauzito kurudi shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema ni kwamba Serikali imekwishaeleza kwamba mwanafunzi anayepata ujauzito hawezi kurudi shuleni, lakini mwanafunzi huyo anaweza akaendelea na masomo kwa kupitia njia mbadala ambazo tuna vituo vya elimu, zipo Taasisi zetu za Elimu ya Watu Wazima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, msimamo wa Serikali ni kwamba mwanafunzi hawezi kurudi shuleni lakini anaweza akapata masomo kupitia njia mbalimbali ambazo Serikali inazitoa. (Makofi)

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 6

MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa suala la kutelekezwa kwa watoto ni jambo ambalo wanawake/ Wabunge hatuwezi kulifumbia macho; ili kupata uhakika na ukweli kuhusu watoto wanaotelekezwa na Waheshimiwa Wabunge wanaume, kwa nini tusifungue Kituo cha Ustawi wa Jamii hapa ili kuweka mambo sawa? Ahsante. (Kicheko/ Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, inaonekana suala la utelekezaji wa watoto hapa Bungeni ni changamoto kubwa sana. Naomba nirudie majibu yangu ya msingi kwamba sheria ya mtoto imeweka utaratibu mzuri tu wa kushughulikia mashauri ambayo yanahusu utelekezwaji ama watoto kutopata matunzo vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kusisitiza kwamba madawati yetu ya Halmashauri katika ngazi ya Halmashauri yatumike katika masuala haya.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 7

MHE. RITTA A. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna baadhi ya wazazi au walezi hasa katika Majiji kwa mfano Jiji la Dar es Salaam wamekuwa wakiwatumia watoto wadogo kuomba omba hata kule kwenye magari, tumekuwa tukishuhudia na nimeona katika jibu la msingi Mheshimiwa Waziri amesema kwamba wazazi kama hao wanatakiwa wachukuliwe sheria/ hatua, kwa sababu watoto hawa wanakosa haki yao ya msingi na wakati elimu ni bila malipo.
Je, ni nani sasa anawachukulia hatua wale wazazi au walezi ambao wanawatumia watoto katika kuomba omba kwenye magari?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto ya mwaka 2008 mtoto hana haki zake kama tano. Mtoto ana haki ya kuishi, kuendelezwa, kulindwa, kushirikishwa na pia mtoto hana haki ya kutobaguliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba mtoto kama nilivyoainisha katika haki zake za msingi, ni jukumu la kwetu sisi wazazi, walezi, jamii na Serikali katika ngazi ya Mitaa na Serikali Kuu kuhakikisha kwamba mtoto anapata haki zake zote hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kabati alikuwa ameelekeza swali lake katika Mkoa wa Dar es Salaam, tuna mikakati mbalimbali ambayo tunaendelea nayo kuhakikisha kwamba watoto wale wa mitaani wanapata haki zao stahili pamoja na kuondolewa katika mitaa.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la ongezeko la watoto wa mtaani katika miji na majiji mengi hapa nchini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sheria zitakazoibana jamii kuwa na wajibu wa kulea watoto hawa badala ya kuwaachia majukumu Mashirika yasiyo ya Kiserikali?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nilitaka kufahamu kutokana na maswali yaliyokuwa yanaulizwa, Mheshimiwa Mbunge aliyeketi muda siyo mrefu ameongea kuhusu Waheshimiwa Wabunge kutelekeza watoto. Sasa nilitaka kuuliza, Waheshimiwa Wabunge hawa wanatelekeza watoto kwa Waheshimiwa Wabunge wenzao ama nje ya Wabunge? (Kicheko)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, inaonekana suala la kutelekeza watoto katika Bunge limekuwa ni kubwa sana. Hili nalirudisha katika kiti chako sasa uweze kuangalia utaratibu mzuri wa kuweza kulishighulikia. (Kicheko)