Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapaleka madaktari na wauguzi katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa kuwa hali ya hospitali hiyo kwa sasa sio nzuri?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hospitali ya Manispaa ya Mpanda kwa sasa hivi inafanya kazi kama Hospitali ya Mkoa, imeelemewa kwa kiasi kikubwa na wangonjwa wanaotoka katika Halmashauri mbalimbali. Wakati tukisubiri mipango ya Serikali ya kutujengea Hospitali ya Mkoa, ni lini Serikali itatusaidia kuongeza waganga pamoja na wauguzi? Nakushukuru.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna upungufu wa wauguzi pamoja na madakatari. Nizitake Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda pamoja na Halmashauri zingine waige mfano mzuri ambao umefanywa na Halmashauri ya Handeni kwa kutumia own source ili kuweza kuwaajiri wale watumishi ambao ni muhimu sana kwa kipindi hiki wakati wanasubiri wale ambao wataajiriwa na Serikali.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapaleka madaktari na wauguzi katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa kuwa hali ya hospitali hiyo kwa sasa sio nzuri?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo lililopo Handeni linafanana kabisa na tatizo lililopo katika Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete, ina upungufu mkubwa wa madaktari na wauguzi. Je, ni lini Serikali itapeleka madaktari na wauguzi katika Hospitali ya Mkoa ambayo inategemewa na mkoa mzima?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la swali la msingi, ni kweli tunatambua kuna upungufu mkubwa wa wauguzi pamoja na madaktari na hasa katika Hospitali ya Mkoa wa Tabora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu, kwa kadri ambavyo ikama inahitajika kutokana na bajeti, ni vizuri basi niwatake Mkoa wa Tabora kwa ujumla wake waanze kwa haraka kuiga mfano mzuri wa Handeni kwa kutumia own source za kwao ili kuweza kuziba hilo pengo lililopo wakati tunasubiri bajeti iruhusu kwa ajili ya kuajiri hao wengine ambao watatoka Serikali Kuu. (Makofi)