Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Kasi ya usambazaji umeme vijijini ni kubwa, lakini katika baadhi ya maeneo, miundombinu inayotumika hasa nguzo hairidhishi. Je, Serikali inaweza kutuambia ni viwango gani (standards) vinavyotumika katika utafutaji wa nguzo hizo?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, wasiwasi wangu katika swali langu la msingi ni viwango vya miundombinu hii hasa nguzo. Wamesema kwamba TANESCO wana zoezi la kukagua nguzo kabla ya matumizi. Swali langu liko hapa: wanachukua hatua gani wanapogundua kwamba nguzo hizi ziko chini ya viwango? Ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Juma Othman Hija, kwa swali lake la nyongeza. Kama ambavyo jibu langu la msingi limesema, Shirika la TANESCO hufanya ukaguzi kwanza wa vifaa hivi kabla havijatumika kwenye miradi hii. Kwa hiyo, endapo inagundulika nguzo hizi hazina ubora, nguzo hukataliwa na wanaotekeleza miradi miradi hiyo huelekezwa kutimiza vigezo na hasa vile viwanda ambavyo vinatengeneza hizi nguzo. Ahsante sana.

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:- Kasi ya usambazaji umeme vijijini ni kubwa, lakini katika baadhi ya maeneo, miundombinu inayotumika hasa nguzo hairidhishi. Je, Serikali inaweza kutuambia ni viwango gani (standards) vinavyotumika katika utafutaji wa nguzo hizo?

Supplementary Question 2


MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Chilonwa, Vijiji vya Bwawani, Kata ya Kamanchali na Vijiji vya Mlebe, Kata ya Msamalo nguzo zilikuwa zimeshapelekwa kwa ajili ya kuweka umeme na mashimo yakachimbwa, lakini baadae nguzo hizi zikaja kuhamishwa.
Je, Serikali ina mpango gani sasa kuona umuhimu wa kuvipa vipaumbele vijiji hivi ambavyo vilikuwa vimeshapelekewa nguzo na kuondolewa ili katika awamu ya tatu visije vikawa vijiji vya mwisho tena? Ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Makanyaga, Mbunge wa Jimbo la Chilonwa kwa swali lake zuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakiri kwamba ni kweli vipo baadhi ya vijiji ambavyo vilipelekewa miundombinu ya hizi nguzo, lakini baadae zikahamishwa kwa kuwa havikuwepo kwenye mpango wa utekelezaji wa kupeleka umeme vijijini REA Awamu ya Pili. Nimdhibitishie kwamba kwenye hii REA Awamu ya Tatu ambayo inaendelea kwa round hii ya kwanza, vile vijiji vyote ambavyo kwa bahati mbaya, kwamba vilipelekewa nguzo halafu zikaondolewa, miradi hiyo itatekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba vijiji vyote nchi nzima vitapata miundombinu ya umeme kwa kipindi hiki ambacho kinaendelea. Ahsante sana.