Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Primary Question

MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawatambua rasmi dereva bodaboda au bajaji kuwaandikia mikataba, kuwekewa akiba na kulipiwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na waajiri wao kwani vijana hao wameshajiajiri kwa zaidi ya asilimia 15 - 25 kwenye kila Wilaya au Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naomba niulize swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini bado wamiliki wa vyombo hivi hawajawapa mikataba waendesha bajaji na bodaboda, matokeo yake wanakubaliana kwa maneno kwamba baada ya mwaka mmoja chombo hiki kitakuwa chako kwa kiasi fulani cha fedha lakini ikifika miezi saba au nane anamnyang’anya kile chombo na kumpa mtu mwingine.
Je, Serikali iko tayari kusimamia zoezi la kukabidhiwa mikataba waendesha pikipiki na wakamatwe waendesha pikipiki waulizwe mkataba aliokupa mwajiri wako uko wapi ili kuwashinikiza wamiliki hawa kutekeleza hii sheria?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA): Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo hili aliloliulizia Mheshimiwa Mbunge la mikataba hapa lazima tuweke vizuri na ieleweke. Mikataba aliyokuwa anazungumzia Mheshimiwa Mbunge ni mkataba wa umiliki wa pikipiki hasa baada ya kuwa kuna makubaliano kati ya mwenye chombo na yule dereva ambaye amepewa chombo hicho.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Serikali, mkataba ambao tuna uwezo wa kuusimamia wa kwanza kabisa ni mkataba wa ajira ambao upo kwa mujibu wa sheria, kifungu cha 14 cha Sheria Na. 6 ya mwaka 2004 ambacho kimeelezea vyema namna ambavyo kila mwajiriwa anapaswa kupewa mkataba.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ambalo kalizungumzia Mheshimiwa Mbunge, ni makubaliano ambayo yamekuwa yakifanyika kati ya waendesha vyombo na wamiliki wa vyombo ambapo utaratibu katika maeneo mengi ni kwamba yule mmiliki anampatia muda muendesha chombo akisharejesha fedha yake basi baadaye chombo kile kinabaki kuwa cha yule dereva.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hilo, nitoe tu wito wa kwamba makubaliano hayo yanaingiwa na pande mbili; mmiliki na mwendesha chombo, ikitokea namna yoyote ambayo haki ya mwendesha chombo huyu inadhulumiwa basi vyombo vya sheria vipo na tuwaombe watu hawa ambao wananyanyasika katika eneo hilo waende kulalamika na hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya hao ambao wanakiuka utaratibu na makubaliano ambayo wameshaingia hapo awali.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawatambua rasmi dereva bodaboda au bajaji kuwaandikia mikataba, kuwekewa akiba na kulipiwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na waajiri wao kwani vijana hao wameshajiajiri kwa zaidi ya asilimia 15 - 25 kwenye kila Wilaya au Halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru. Pamoja na mikataba ya bodaboda na bajaji, mikataba ni fursa za hawa vijana kufanya kazi katika miji. Sera ya MKURABITA ni mkakati wa kurasimisha biashara za wanyonge ziwe rasmi. Bodaboda na bajaji hizi baada ya mikataba hii wanapata tabu sana kufanya biashara katika miji na hasa kwenye barabara kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutambua na kuwajali wafanyabiashara wadogo wadogo, lakini Mamlaka za Halmashauri bado zinazuia vijana hawa wasifanye biashara kwa uhakika na kuwatia hasara sana. Yako malalamiko, madalali wanaokamata bajaji na bodaboda wanaruhusu bodaboda zao tu ziingie mjini.
Je, Serikali sasa kwa kutambua sera MKURABITA wanaonaje sasa hili jambo liruhusiwe na hawa vijana wapate uhalali wa kufanya biashara katika miji yetu? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, haya mambo yanatofautiana, ni case by case Mikoa kwa Mikoa na Wilaya kwa Wilaya, lakini Mheshimiwa Zungu ame-raise jambo la msingi sana. Naomba Ofisi yangu ilichukue jambo hili kwa ajili ya kuliwekea utaratibu mzuri tuangalie jambo gani lifanyike katika eneo gani ili mradi tufikie muafaka kwa ajili ya vijana wetu. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawatambua rasmi dereva bodaboda au bajaji kuwaandikia mikataba, kuwekewa akiba na kulipiwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na waajiri wao kwani vijana hao wameshajiajiri kwa zaidi ya asilimia 15 - 25 kwenye kila Wilaya au Halmashauri?

Supplementary Question 3

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa vyombo hivi vya usafiri bodaboda na bajaji vimekuwa vikisababisha ajali nyingi na wananchi wengi wanapoteza maisha, lakini kwa hali ilivyo sasa wamiliki wanakatia bima ndogo ambayo haim-cover yule anayeendesha na yule abiria wake. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukaa na wamiliki wa bodaboda wakatie bima kubwa (comprehensive) ili kuwalinda wananchi wetu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake ilikuwa ni kwamba Serikali haioni umuhimu wa kukaa ili kutengeneza mfumo mzuri ambao utasaidia na hawa ambao ni abiria lakini vilevile na hawa ambao wanaendesha vyombo hivi kuwa katika hali ya usalama. Limeletwa wazo na sisi kama Serikali tunalichukua kuona utaratibu mzuri ambao utasaidia katika kuondoa adha hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa kuongezea si tu katika bima tutakwenda mbali zaidi kuwataka pia na hawa waajiri ambao wanawaajiri hawa vijana wajiunge na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kwa maana ya WCF ili inapotokea tatizo lolote la muendesha bodaboda huyu basi na yeye awe katika sehemu nzuri ya kuweza kupata utaratibu ambao umewekwa na WCF kwa maana ya kuweza kumshughulikia katika matatizo ambayo yanatokana na magonjwa au ulemavu kutokana na shughuli ambayo wanaifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumjulisha Mheshimiwa Gekul kwamba suala hili tunalichukua lakini tutakwenda mbali zaidi kusisitiza kwamba na hawa wanakuwa katika utaratibu huo mzuri.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawatambua rasmi dereva bodaboda au bajaji kuwaandikia mikataba, kuwekewa akiba na kulipiwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na waajiri wao kwani vijana hao wameshajiajiri kwa zaidi ya asilimia 15 - 25 kwenye kila Wilaya au Halmashauri?

Supplementary Question 4

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, sote tunafahamu kwamba biashara ya bodaboda imekuwa ni sehemu kubwa sana ya ajira kwa vijana, lakini naomba tu kufahamu ukichukulia Jimbo la Nyamagana peke yake zipo bodaboda takribani 6,700 lakini vijana hao wenye uwezo wa kujiajiri ni asilimia 30% peke yake, ni nini mkakati wa Serikali kutumia walau fedha za Mfuko wa Vijana na Fedha za Uwezeshaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu waweze kukopeshwa na fedha hizi watumie kama sehemu ya ajira yao ili kuepusha migogoro na waajiri wao na mikataba isiyokuwa rafiki kwao? Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mabula kwa kazi kubwa anayofanya kupambania vijana wa Nyamagana hasa vijana wamachinga na bodaboda amekuwa akifanya kazi hii vizuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ni nini katika hili? Ni kweli tunatambua kwamba asilimia kubwa ya vijana wangependa kumiliki pikipiki hizi ziwe mali yao lakini kikubwa ambacho kinawakwamisha ni upatikanaji wa mikopo ya masharti nafuu, lakini vilevile na fedha kuweza kununulia vifaa hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali hatua ya kwanza ambayo tumekuwa tukiifanya ni kuhamisisha vikundi vya vijana kwanza wakae pamoja, wajisajili then baada ya pale sisi chini Ofisi ya Waziri Mkuu tunalo Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ambalo linaratibu zaidi ya mifuko 19 ambayo inatoa mikopo na inatoa na ruzuku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, rai yangu ni kuwaomba Waheshimiwa Wabunge ambao naamini kila Mbunge hapa kwake ana bodaboda ambao wana mahitaji haya kwanza kuwahamasisha kukaa katika vikundi, wajisajili na baadae tutawasaidia kuwaunganisha na mifuko mbalimbali na taasisi za kifedha ili waweze kupata mikopo ya aina mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ziko programu nyingi ambazo zinafanyika sasa hivi ambapo yule mwendesha bodaboda ana-deposit kiasi kidogo tu katika taasisi ya fedha na anakabidhiwa chombo chake na anakuwa anafanya kazi kurudisha taratibu taratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge wote, najua ni kilio cha Wabunge wengi hakikisheni kwamba mnahamasisha uundaji wa vyama vya bodaboda na baadaye Ofisi ya Waziri Mkuu, sisi tutafanya kazi ya kuwasaidia kuratibu kwa maana mifuko gani inaweza kusaidia kuwezesha makundi haya.