Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. IBRAHIM MOHAMEDALI RAZA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua kwa kuwasaidia vijana walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya?

Supplementary Question 1

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini kuna kitu amekiongelea, amesema kutibu. Mimi ninavyoona kinga ni bora kuliko tiba; na kwa kuwa Serikali inawatibu vijana hawa baada ya kuathirika lakini ni bora ingewakinga wasiathirike. Je, Serikali itachukua hatua gani za haraka au madhubuti za kuwakinga vijana wake wasitumie madawa ya kulevya badala ya kuwapeleka kwenye sober house wakati wameshaathirika na kuwatibu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa scanning machine katika maeneo mbalimbali ni muhimu sana katika maeneo kama airport, bandarini na sehemu nyingine zozote. Hata hivyo, kuna maeneo mengine kama kule kwetu Pemba, juzi nimesafiri kuja huku scanning machine yake haifanyi kazi na sehemu hizi ndizo wanazopitisha vitu vyao watu hawa wabaya.
Je, Serikali itachukua hatua gani kuwanunulia mashine nyingine pale airport ya Pemba ama kuwatengenezea ile mashine ili kuepukana na matatizo haya ya kusafirisha madawa haya ya kulevya? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA): Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge ni kweli, kinga ni bora zaidi. Katika utaratibu wa kushughulikia masuala ya dawa za kulevya, hatua ambazo Serikali imezichukua zipo katika mgawanyo wa sehemu tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya kwanza tunaiita ni supply reduction, ni punguzaji wa upatikanaji wa dawa za kulevya ikiwa ndiyo sehemu ya kwanza kusaidia kumfanya
kijana huyu au mtu yeyote asipate madawa ya kulevya. Ni dhahiri kabisa kwamba baada ya Mamlaka ya Dawa za Kulevya kuanza kazi yake, kuanzia Januari mpaka Desemba, 2017 ninavyozungumza hivi sasa tayari wamefanyakazi kubwa ya kuzuia upatikanaji wa madawa ya kulevya.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa takribani kilo 196 za heroin zilikamatwa lakini takribani tani 47 za bangi zilikamatwa, tani 7 za Mirungi zilikamatwa na mashamba ya bangi hekari 542 yaliteketezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ukiyafanya haya sasa, yanasaidia kupunguza upatikanaji wa dawa za kulevya huko mtaani. Kwa hiyo, kazi ya kwanza Serikali inayofanya ni hiyo ya kusaidia hiyo kitu inaitwa supply reduction.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu cha pili tunachokifanya ni demand reduction, tunapunguza pia uhitaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, ya tatu ni harm reduction. Harm reduction sasa huyu ameshatumia dawa za kulevya hatuwezi kumuacha hivyo hivyo ndiyo maana sasa tunakuja na tiba lakini vilevile kumsaidia mtu huyu aweze kurudi katika hali yake ya kawaida.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa ninavyozungumza mamlaka imefanya kazi yake vizuri sana, hata katika uagizaji wa methadone hapa nchini tumetoka katika kiwango cha kawaida cha kilo 120 mpaka kilo 300, maana yake nini? Maana yake ni kwamba dawa za kulevya sasa hivi mtaani hazipatikani, kwa hiyo, hawa waathirika wanapata tabu kubwa ndiyo maana wanakwenda kutibiwa katika vituo vyetu ambavyo tumeviweka kwa ajili ya kuwatibu waraibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali inalitambua hilo na ndiyo maana tumekuja na hiyo mikakati tofauti tofauti kuhakikisha kwamba dawa za kulevya hazipatikani na tunawalinda vijana wetu.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Napenda kuongezea kwenye swali la pili la Mheshimiwa Faida Bakar kwamba kwa mujibu wa taarifa tulizonazo kutoka Zanzibar Airport Authority (ZAA), scanner ya Pemba inafanya kazi vizuri kabisa na inafuatiliwa kila siku na kila wakati. Scanners zote za viwanja vyetu vya ndege tunazifuatilia mara kwa mara, ahsante sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu yote yaliyotolewa na Naibu Mawaziri kuhusu suala hili, tunatambua umuhimu mkubwa wa kuhakikisha viwanja vyetu vyote vya ndege scanner zinafanya kazi na hizo ndizo zinazoweza kutusaidia kudhibiti tatizo la uingizaji wa dawa za kulevya.
Kwa hiyo, naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge kama kuna tatizo kwenye scanner ya Zanzibar basi tutafanya utafiti wa kina ili ndani ya Serikali tuzungumze ili scanner hiyo iweze kufanya kazi na tuweze kuendelea kudhibiti tatizo hilo la dawa za kulevya. (Makofi)

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. IBRAHIM MOHAMEDALI RAZA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua kwa kuwasaidia vijana walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa naibu Spika, mwaka jana tumeshuhudia Serikali yetu ikijaribu kupunguza tatizo la utumiaji wa madawa ya kulevya kwa kuwataja hadharani watumiaji na wauzaji jambo lililosaidia kupunguza lakini siyo kumaliza tatizo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee. Nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshuhudia mwaka jana Serikali yetu ikijaribu kupunguza tatizo la utumiaji wa madawa ya kulevya kwa kuwataja hadharani watumiaji na wauzaji lakini jambo hili halikumaliza tatizo bali ilipunguza tu, suala hili bado lipo tena kwa wingi zaidi na wanaoathirika ni vijana wa Kitanzania ambao ni nguvu kazi ya nchi. Je, ni lini sasa Serikali itaona umuhimu wa kujenga rehab zitakazotambulika ili kumaliza janga hili? Nashukuru.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda nichukue fursa hii kumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Halima Bulembo kwa namna ambavyo anawapigania vijana wa Taifa letu la Tanzania, lakini amekuwa mstari wa mbele kutetea maslahi ya vijana. (Makofi)
Mheshimiwa naibu Spika, ni kweli tunafahamu kwamba moja kati ya njia ya kuwarudisha waathirika wa dawa za kulevya katika hali yao ya kawaida ni pamoja na kuwa na sober houses nyingi na rehabilitation centers ambazo zitawasaidia kuwarudisha kururdi katika hali yake ya kawaida. Ndiyo maana katika majibu yangu ya msingi nimesema, moja kati ya mkakati ambao tunao ni uanzishwaji wa tiba ambao inaitwa occupational therapy ambao lengo lake kubwa ni kumsaidia muathirika huyu wa dawa za kulevya kurudi katika hali yake ya kawaida.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika utaratibu huo, waathirika wote wa dawa za kulevya ambao watapelekwa katika vituo vyetu mbalimbali watafundishwa stadi mbalimbali za kazi ili baadaye akirudi asirejee katika matumizi ya dawa za kulevya. Katika mpango wetu huo, Serikali tunaanza utoaji wa tiba hiyo katika kituo ambacho kinajengwa hapa Dodoma katika eneo la Itega. Hali kadhalika tunafanya kazi pia na taasisi na wadau mbalimbali katika kuhakikisha kwamba tunawasaidia vijana wetu wa Kitanzania wasipate madhara zaidi ya matumizi ya dawa za kulevya.

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. IBRAHIM MOHAMEDALI RAZA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua kwa kuwasaidia vijana walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya?

Supplementary Question 3

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa vijana wengi wanaopelekwa katika sober houses wanalipishwa kiasi fulani cha fedha ili waweze kujikimu kwa vyakula. Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka kuwasaidia kwa sababu kuna baadhi ya jamii hazina uwezo wa kuwasaidia watoto wale? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA NA VIJANA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli sober houses nyingi zinamilikiwa na watu binafsi na waathirika hawa wa dawa za kulevya wamekuwa wakilipishwa. Mpango wa Serikali ni kuandaa utaratibu sasa ambapo na sisi tutatengeneza sober houses za kwetu ili kufanya huduma hii ipatikanike kwa urahisi na kila mmoja ambaye hana uwezo wa kumpeleka katika sober house za private aweze kupata tiba hii na imsaidie kurudi katika hali ya kawaida.