Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA (K.n.y MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Shughuli kubwa za kiuchumi kwa wananchi wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika ni uvuvi lakini nyavu zimekuwa zikikamatwa na kuchomwa moto. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia wavuvi hao nyenzo au vifaa vya kisasa vya uvuvi?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Ninaswali moja la nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba ina hakikisha wavuvi hawa wanapata sokola uhakika baada ya kuhamasisha uzalishaji kwa kuhakikisha kwamba kuna jengwa kiwanda cha kuchakata minofu ya samaki katika ukanda wa Lake Tanganyika na hasa ukizingatia kwamba kuna specie ya kipekee katika Ziwa Tanganyika ya samaki anayeitwa migebuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Serikali ina mkakati gani kuhakikisha viwanda vinajengwa katika ukanda ule? (Makofi)

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI:Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa uvuvi katika Ziwa Victoria tumejenga mwalo wa kisasa pale Kibirizi ambapo mwalo ule tumeuwekea vifaa vyote muhimu ambavyo samaki akivuliwa anaweza kutunzwa hata kwa zaidi ya wiki mbili. Yote haya ni kuwafanya wavuvi wanapovua samaki kabla hawajafika sokoni wasiharibike yaani waweze kupata soko kabla hawajaharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais tumejenga pale mradi mkubwa sana wa ziadi ya takriban shilingi bilioni mbili zimetumika kwa ajili ya kutengeneza mwalo ule.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hili la pili linalokuja ni la kujenga viwanda sasa kwa sababu tayari tumeshapata mwalo mzuri ambapo samaki wanapokelewa na kutunzwa. Kinachofuata sasa ni maandalizi ya kujenga kiwanda ili tuweze kuchakata samaki katika ukanda ule na tutafanya hivyo. (Makofi)

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA (K.n.y MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Shughuli kubwa za kiuchumi kwa wananchi wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika ni uvuvi lakini nyavu zimekuwa zikikamatwa na kuchomwa moto. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia wavuvi hao nyenzo au vifaa vya kisasa vya uvuvi?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB M. VULLU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya wavuvi wa Uvinza haina tofauti sana na hali ya wavuvi wa Ukanda wa Pwani ya Mkoa wa Pwani. Naomba nizungumzie hasa Kisiwa cha Mafia ambapo wanawake wengi wanajitahidi kulima kilimo cha mwani si kwa wao tu kwa mtazamo wa nje kwamba kinawapatia mapato lakini pia kilimo cha mwani kinasaidia kukuza samaki kuzaliana, kutunza mayai na hata kuhifadhi mazingira bora ya bahari. Kilimo hicho kinalimwa kwa shida sana,
Je, ni lini Serikali itahakikisha inawapatia nyenzo kama viatu, kamba na vifaa vingine vya kulimia mwani ili wananchi hao waweze kulima vizuri? (Makofi)

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, tumefanya vizuri sana Zanzibar katika kilimo cha mwani hasa kwa kuwatumia wataalam wetu hawa wa COSTECH pamoja na IMS. Tutapeleka wataalam wetu hawa katika eneo hili analolizungumza Mheshimiwa Mbunge ili waweze kwenda kuwafundisha wakulima wetu wanaolima zao la mwani ambalo tunalipendekeza sana sasa hivi kwa wakulima na kulipigania lifanyike kwa ajili ya kuongeza thamani za zao hilo na kujipatia kipato.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo eneo hilo ambalo wakulima wanalima kwa shida tunatahakikisha kwamba tunaelekeza nguvu huko kuhakikisha wafugaji wale tunawapa mafunzo, tunawaonesha soko na vilevile tunawaunganisha kimtaji ili kuhakikisha kwamba zao hilo wanalilima vizuri zaidi kwa sababu lina soko la uhakika duniani. (Makofi)

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA (K.n.y MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Shughuli kubwa za kiuchumi kwa wananchi wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika ni uvuvi lakini nyavu zimekuwa zikikamatwa na kuchomwa moto. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia wavuvi hao nyenzo au vifaa vya kisasa vya uvuvi?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Na mimi naomba nimuulize Naibu Waziri swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Ziwa Tanganyika kulikuwa na uharamia, wale wavuvi walikuwa wakivamiwa na maharamia kutoka nchi za jirani na kuwapokonya nyavu zao na hata mitumbwi yao. Je, Serikali imedhibiti vipi maharamia hawa katika Ziwa Tanganyika?(Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba wavuvi wetu wa Ziwa Tanganyika na hata wavuvi katika Ziwa Victoria wamekuwa wakivamiwa na maharamia.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie kwamba Serikali imepata taarifa hizi na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimejipanga ipasavyo kuhakikisha wavuvi wetu wanalindwa ili waweze kufanya shughuli zao za uvuvi kama kawaida bila ya hofu yoyote.