Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Zaidi ya asilimia 70 ya eneo la Jimbo la Igunga lilikuwa limefunikwa na maji ya Ziwa Victoria lakini baada ya Ziwa hilo kukauka, eneo hilo limebaki kuwa ni mbuga inayojaa maji wakati wa masika hivyo kufanya ujenzi wa barabara za vijiji kuwa wa gharama kubwa sana na Halmashauri ya Wilaya ya Igunga haina uwezo wa kifedha kujenga barabara hizo. Je, kwa nini Serikali isiandae mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara za vijijini katika Wilaya ya Igunga na Wilaya nyingine nchini zenye tatizo kama hili?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake ambayo yametoa matumaini kwamba watafanyia research udongo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye swali langu la msingi, Jimbo la Igunga ni Jimbo ambalo udongo wake hauwezi kujengwa kwa kukwangua barabara lazima uweke tuta kwahiyo hela zinazotengwa kwa Halmashauri hizi hazitoshi kabisa kujenga hizi barabara.
Swali la kwanza, je, kwa nini Serikali isilete upendeleo kwenye Jimbo hili la Igunga ikasaidia kujenga barabara za vijijini?
Swa li la pili, kwa azma ya Serikali ya kuunganisha Mikoa Tanzania, kwanini Serikali isijenge kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Kolandoto kupitia Igurubi kwenda Igunga, Mbutu na kwenda mpaka Loya kwenye Jimbo la Igalula na mpaka Tura kwenye barabara ya lami itokayo Tabora kwenda Dodoma?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo swali lake la msingi linaeleleza jinsi ambavyo eneo lile linahitaji kutazamwa kwa umakini kwani udongo ule ni tofauti na maeneo mengine.
Kwanza naomba nikubaliane naye kwamba siyo kama suala la upendeleo lakini ni vizuri tutakatazama kulingana na hali ya barabara zile na naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, essence ya kuanzia TARURA, Waheshimiwa Wabunge wengi tumekuwa ni mashahidi hapa tumekuwa tukiomba barabara zetu zipandishwe hadhi zichukuliwe na TANROADS kwasababu tukiamini TANROADS inafanya kazi vizuri zaidi. Naamini kwa kuanzishwa kwa chombo hiki cha TARURA hakika barabara zetu zitatengenezwa katika kiwango ambacho kitakuwa bora zaidi. Naamini na barabara hii ya Mheshimiwa Kafumu nayo kwa kupitia TARURA na kwa sababu inahitaji kiasi kingi che fedha, fedha ambayo itatengwa na Serikali itakuwa nyingi ili kuweza kukidhi hali ya barabara hiyo.
Kuhusiana na swali lake la pili la kuunganisha barabara kutoka Kolandoto mpaka Tura ambayo kimsingi jiografia yake inaonyesha ni kwamba itakuwa ni kiungo kikubwa sana mpaka kufika Dodoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kama Serikali tulichukue, tulifanyie kazi halafu tuone namna itakayokuwa bora katika kulitekeleza.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Zaidi ya asilimia 70 ya eneo la Jimbo la Igunga lilikuwa limefunikwa na maji ya Ziwa Victoria lakini baada ya Ziwa hilo kukauka, eneo hilo limebaki kuwa ni mbuga inayojaa maji wakati wa masika hivyo kufanya ujenzi wa barabara za vijiji kuwa wa gharama kubwa sana na Halmashauri ya Wilaya ya Igunga haina uwezo wa kifedha kujenga barabara hizo. Je, kwa nini Serikali isiandae mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara za vijijini katika Wilaya ya Igunga na Wilaya nyingine nchini zenye tatizo kama hili?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa mgao wa Road Fund Serikali Kuu wanachukua asilimia 70 na Serikali za Mitaa asilimia 30 na kwa kuwa Serikali imeunda chombo cha TARURA na kama mgao utakuwa asilimia 30 zile zile na barabara zetu ni mbaya sana vijijini kule hasa Wilaya ya Mpwapwa.
Je, sasa mgao utaongezeka iwe asilimia 50 kwa 50?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi asilimia 70 na asilimia 30 ni kwa mujibu wa Sheria na Sheria hii ilitungwa na Bunge lako Tukufu. Kama haja itakuwepo kwa wakati huo tutakubaliana kiasi gani ambacho kitafaa na lengo ni kuhakikisha kwamba chombo hiki ambacho tumekianzisha TARURA kinakuwa na uwezo ili kiweze kukidhi haja iliyoanzishwa.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Zaidi ya asilimia 70 ya eneo la Jimbo la Igunga lilikuwa limefunikwa na maji ya Ziwa Victoria lakini baada ya Ziwa hilo kukauka, eneo hilo limebaki kuwa ni mbuga inayojaa maji wakati wa masika hivyo kufanya ujenzi wa barabara za vijiji kuwa wa gharama kubwa sana na Halmashauri ya Wilaya ya Igunga haina uwezo wa kifedha kujenga barabara hizo. Je, kwa nini Serikali isiandae mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara za vijijini katika Wilaya ya Igunga na Wilaya nyingine nchini zenye tatizo kama hili?

Supplementary Question 3

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na mimi kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambazo ziko kwenye Mji mdogo wa Sirari na Mji mdogo wa Nyamongo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais akiwa pale na ziko TARURA.
Unasemaje kuhusu kutupa angalau kilometa mbili za lami ili kuondoa matatizo kwenye Mji ule ambao una watu wengi Miji miwili hii ambayo ni Sirari na Nyamongo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi za Mheshimiwa Rais zimetolewa maeneno mengi na sisi sote ni mashuhuda kwamba tumeletewa taarifa kwamba uratibu utafanyika kuhusiana na ahadi zote ambzo zilitolewa na Mheshimiwa Rais na kimsingi katika kutekeleza ahadi hizo tunahitaji miaka mitano, ndani ya miaka mitano tuna wajibu wa kuhakikisha kwamba ahadi za Rais zinatekelezwa naamini katika kipindi hicho na eneo lake litatekelezwa kwa kujengewa hiyo barabara ya lami.