Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Shamba la malisho lililopo katika Kata ya Shishiyu Wilayani Maswa linamilikiwa na Serikali lakini halitumiki ipasavyo:- Je, Serikali Kuu haioni haja ya kulirejesha shamba hilo kwa Halmashauri ya Wilaya ili lipangiwe matumizi mengine?

Supplementary Question 1

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa shamba hlili la Shishiu hakuna mifugo inayokusanywa pale na kwakuwa pia katika masterplan ya Waizara ya Mifugo wana lengo la kuzalisha mbegu na malisho kwa ajili ya mifugo ili kuweza kuboresha ufugaji wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa kuwa lengo la Wilaya ya Maswa sio kubadilisha lakini ni kuitumia kwaajili ya kuzalisha mbegu na malisho. Je, Serikali haioni umuhimu wa kufikiria upya uamuzi wake huu ili kwamba eneo hili lipewe kwa Wilaya sio kumilikisha ili waweze kutumia kwa ajili ya kuzalisha mbegu na malisho kwa ajili ya mifugo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa pia maeneo kama haya yako mengi nchini Mheshimiwa Naibu Waziri ametaja vituo 28 pia ziko Ranchi nyingi ambazo wala hazitumiki ipasavyo; je, Serikali inaonaje ikifanya vituo hivi pamoja na Ranchi kama vituo vya kujenga uwezo wafugaji wetu ili kwamba waweze kuzalisha mbegu na malisho ambayo ni changamoto kubwa kwenye nchi yetu?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki, Mbunge wa Maswa Magharibi kwa swali zuri kabisa la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, umuhimu wa maeneo haya kama nilivyoeleza katika jibu la msingi bado unabaki palepale hasa ikizingatiwa ya kwamba tunakwenda katika kipindi cha Tanzania ya viwanda na eneo nyeti kabisa hili la viwanda vya uchakataji na mazao ya mifugo ndio hasa unaoangaliwa. Ninachoweza kumshauri Mheshimiwa Mashimba Ndaki yeye na wenzake katika Halmashauri ya Maswa wanaweza kuandaa mpango mkakati na wakauwasilisha katika Wizara kwa ajili ya kutazamwa kama itawezekana kuweza kuandaa hati ya maridhiano kwa maana ya memorandam of understanding kuweza kufanya haya anayoyasema ya kuboresha bila ya kubadilisha lile lengo la msingi la kutumika kwa maeneo haya kwa ajili ya mifugo na kuongeza thamani ya mifugo yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili hili la Ranch, naomba nimwambie Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki na Waheshimiwa Wabunge wote, katika masterplan yetu ambayo inaendelea kuandaliwa ni kwamba maeneo haya tunawapa umuhimu mkubwa sana na shirika letu la Ranchi za Taifa hivi sasa tuna mpango mkubwa wa kulihuisha na lina mpango mzuri wa kuhakikisha kwamba Ranchi zetu zinakwenda kusaidia kuinua tasnia hii ya huduma za mifugo na hatimaye kuleta kipato kikubwa kwa nchi yetu. (Makofi)