Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Elimu ya ufundi ni muhimu ili kuwawezesha vijana kuajiriwa na kujiajiri:- • Je, nchi yetu ina vyuo vingapi vya Ufundi Stadi vya Umma? • Je, kuna vyuo vingapi visivyo vya Umma? • Je, hivi vyote vina uwezo wa kudahili vijana wangapi kwa mwaka?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Serikali iliahidi kwamba maeneo yenye vyuo vya wananchi (FDCs) itaviongezea uwezo ili viweze kutoa elimu ya ufundi kwa ufanisi zaidi. Je, ni lini Serikali sasa itatimiza hiyo azma katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi, Njombe Mjini? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ujenzi wa Vyuo vya VETA nchini unasuasua sana na Jimbo la Njombe Mjini lina shule 11 za sekondari, kuanzisha fani ya ujenzi ama umeme gharama yake ni nusu ya gharama ya kujenga maabara ya kemia ama ya baiolojia. Je, Serikali ipo tayari kuzifanya Shule za Sekondari Mgola na Luhololo kuwa shule za Sekondari za Ufundi kwa fani mbili kwa majaribio (pilot project)?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu jitihada za Serikali katika kuboresha Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDCs); naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara tayari imepata ufadhili wa kuweza kukarabati vyuo 30 kati ya 55 tulivyonavyo vya wananchi. Lengo ni kuhakikisha kwamba vyuo hivi vinarudi katika utendaji bora zaidi, vilevile ikiwezekana waendelee kutoa elimu ya ufundi kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Chuo chake cha Njombe Mjini nimweleze tu kwamba ni fursa imejitokeza kwamba tayari tumepata dola milioni 120 kwenye mradi unaoitwa Education and Skills for Productive Jobs (ESPJ), fedha hizi zinapatikana lakini kwa ushindani. Kwa hiyo hata Chuo chake cha Njombe Mjini inabidi washindane kuomba fedha hizi ili Wizara iweze kuja kufanya tathmini na kuangalia kama ni chuo ambacho kinahitaji kukarabatiwa, ni fursa ambayo ipo. Kwa hiyo nimweleze tu kwamba fedha zipo tutatangaza muda sio mrefu ili waweze kuziomba.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna mpango wa kurejesha vyuo vyote 55 vya wananchi virudi katika hali yake ya zamani, viwe vyuo vizuri ili viendelee kusaidia kutoa mafunzo katika maeneo mbalimbali ya elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni kuhusiana…
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na Shule zake za Sekondari za Mgola na Luhololo kuruhusiwa kuwa shule za ufundi hili linajadilika. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge kama wao kama Njombe Mjini wanakubali zibadilike kuwa shule za ufundi sisi tuko tayari kama Wizara tufanye majadiliano na kwa hakika itawezekana. (Makofi)

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Elimu ya ufundi ni muhimu ili kuwawezesha vijana kuajiriwa na kujiajiri:- • Je, nchi yetu ina vyuo vingapi vya Ufundi Stadi vya Umma? • Je, kuna vyuo vingapi visivyo vya Umma? • Je, hivi vyote vina uwezo wa kudahili vijana wangapi kwa mwaka?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Maswali Namba 75 na swali Na 76 yanafanana lakini Mheshimiwa Naibu Waziri katika majibu yake ambayo ni mazuri sana amesema kwamba palipo na wananchi na kama wamehamasika na wameshajitolea kuanza kazi za ujenzi wa vyuo kama hivi, Serikali iko tayari kuweza kuwapa mkono.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bunge lililopita, Serikali iliwakubalia wananchi wa Wilaya ya Busega kutenga eneo kwa ajili ya kuanzisha Chuo cha Ufundi Stadi (VETA). Je, wazo hili la Serikali bado liko palepale au limebadilika?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema mwenyewe, kama tayari kuna ahadi thabiti ya Serikali kuhusiana na chuo chake cha VETA Busega, leo hii haiwezi ikabadilika. Kwa hiyo, tuendelee na majadiliano tokea tulipoacha kutoka kwa wenzetu ili tuone namna bora ya kutekeleza ahadi hiyo. (Makofi)

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Elimu ya ufundi ni muhimu ili kuwawezesha vijana kuajiriwa na kujiajiri:- • Je, nchi yetu ina vyuo vingapi vya Ufundi Stadi vya Umma? • Je, kuna vyuo vingapi visivyo vya Umma? • Je, hivi vyote vina uwezo wa kudahili vijana wangapi kwa mwaka?

Supplementary Question 3

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru sana kwa kuniona. Kwa kuwa, hivi karibuni Serikali kupitia Waziri Jafo ilitangaza kwamba au ilitoa agizo kila mkoa utengeneze viwanda 100 na kwa kuwa vyuo hivi vya ufundi ni muhimu sana. Je, ni lini Serikali itaanza kutoa ruzuku kama ilivyokuwa ikiahidi mara kwa mara kwenye vile vyuo ambavyo ni vya wananchi, kule kwangu kuna vyuo vya Mawelas, KVTC, Imani ili azma hiyo ya Serikali iweze kutimia haraka? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza katika moja kati ya majibu yangu leo, kwa kuanzia tunaanza na ukarabati kabla hatujaanza kufikiria kutoa ruzuku tunaanza kwanza na ukarabati, kama nilivyosema tumepata Dola milioni 120 tunaanza kukarabati vyuo 30 kwanza kati ya 55.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Komu achukulie kama ni hatua mojawapo kufikia hicho anachotaka ili vyuo vyake viweze kushindania fursa hii ya kukarabatiwa; baadaye sasa vikishakuwa katika hali nzuri ya kuchukua wanafunzi ndiyo tuanze kufikiria masuala mengine kama ruzuku. Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.