Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Chuo cha Ufundi (VETA):- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa niipongeze Serikali kwa mpango wake wa kujenga chuo kila Mkoa. Kwa kuwa vijana wengi Mkoa wa Simiyu hawana kazi na ukosefu wa ajira unasababisha vijana wengi kujiingiza kwenye vitendo vya uhalifu. Namwomba Naibu Waziri anihakikishie, ni lini sasa huo ujenzi utaanza Mkoani Simiyu ili vijana wajifunze ujuzi waweze kujiajiri wenyewe waondokane na umaskini? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, kwamba kwa namna tulivyopangilia tutajitahidi tusitoke nje ya mipango yetu, ujenzi unatakiwa uanze Februari mwaka kesho.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi hicho wakati tunasubiri chuo kikamilike, tunaendelea kuwasihi vijana wa Simiyu na wengine wa Tanzania waendelee kuachana na uhalifu kwa sababu inawezekana isiwe tiba ya changamoto iliyopo.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Chuo cha Ufundi (VETA):- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 2

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Elimu ya ufundi ni muhimu ili kuwawezesha vijana wetu kuajiriwa au kujiajiri. Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Lushoto?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye swali la msingi, Serikali kwa sasa ina mpango wa kujenga vyuo 43 katika Wilaya mbalimbali hapa nchini, tayari tumeanza taratibu katika wilaya saba.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni kwamba Wilaya zote nchini katika wakati mmoja au mwingine zinakuwa na Vyuo vya VETA. Kwa hiyo, hata kwake Mheshimiwa Mbunge, Lushoto, kwa vyovyote vile ni sehemu ya Tanzania na ipo katika mipango hii. Naomba tu avute subira kama Waheshimiwa Wabunge wengine vilevile nitakapowaeleza, kwa sababu Serikali imedhamiria kwamba itaendelea kujenga vyuo hivi kadri ya fedha zitakavyopatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimwombe Mheshimiwa Mbunge pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine kwamba inakuwa ni rahisi zaidi Serikali kuingiza mikono yake au jitihada kama wananchi wenyewe wamehamasika. Kwa hiyo, pale tunapoona wananchi wenyewe wameanza kujichangisha na kuhamasika inakuwa ni rahisi hata Wizara kutumia fedha ambazo zinapatikana kusaidia.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Chuo cha Ufundi (VETA):- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi.Pamoja na Serikali kuendelea kujenga vyuo katika Mikoa na Wilaya, tuna tatizo kubwa sana la Walimu wa Vyuo vya VETA, kwa sababu tuna chuo kimoja tu cha Morogoro ambacho ndicho kinachotoa Walimu. Je, Serikali inatusaidiaje kuhakikisha kwamba Vyuo hivi vya VETA vinavyojengwa na vilivyopo ambavyo vina tatizo kubwa sana la Walimu vinakuwa na Chuo kingine cha Walimu ili kuweza kutatua tatizo la wanafunzi, watoke pale wakiwa wamekamilika? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama anavyosema kwamba kuna changamoto ya kuwapata Walimu wa Vyuo vya VETA. Nimhakikishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mkakati wa kuhakikisha kwamba elimu ya ufundi inapatikana nchini kwa wingi na ubora zaidi ni pamoja na kuhakikisha kwamba tunakuwa na Walimu wa kutosha. Kwa hiyo, katika mikakati ya Wizara kuna mkakati wa kuhakikisha kwamba Walimu pia wanapatikana.